bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 19
Acts 19
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 18
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 20 →
1
Wakati Apolo alipokuwa Korinto, Paulo akasafiri akipitia katika inchi ya vilima na kufika Efeso. Kule akakuta wanafunzi wamoja;
2
akawauliza: “Ninyi mulipokea Roho Mutakatifu wakati mulipoamini?” Nao wakamujibu: “Hapana! Hatujasikia hata kidogo kwamba kuko Roho Mutakatifu.”
3
Halafu Paulo akawauliza: “Basi mulibatizwa kwa ubatizo gani?” Wakamujibu: “Tulibatizwa kwa ubatizo wa Yoane.”
4
Paulo akawaambia: “Yoane aliwabatiza wale waliogeuka toka zambi zao na kuwaambia Waisraeli kwamba wamwamini yule atakayekuja nyuma yake, naye ndiye Yesu.”
5
Waliposikia maneno haya, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
6
Paulo akaweka mikono yake juu yao, na Roho Mutakatifu akashuka juu yao, nao wakaanza kusema kwa luga na kutabiri.
7
Wote walikuwa kadiri ya watu kumi na wawili.
8
Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akiingia katika nyumba ya kuabudia na kuhubiri watu kwa uhodari. Akabishana nao juu ya habari za Ufalme wa Mungu, akitaka wazisadiki.
9
Lakini wamoja wakakuwa na mioyo migumu hata wakakataa kuamini, wakaanza kusema vibaya juu ya Njia ya Bwana mbele ya mukutano. Kwa hiyo Paulo akajitenga nao, akaenda na wanafunzi peke yao. Na kila siku alibishana na watu katika chumba cha kufanyia usomi cha mutu mumoja aliyeitwa Tirano.
10
Mambo haya yakaendelea kwa muda wa miaka miwili hata Wayuda na Wagriki wote waliokaa katika jimbo la Azia wakasikia neno la Bwana.
11
Mungu akaendelea kufanya miujiza ya ajabu kwa njia ya Paulo.
12
Na hata watu walitwaa vitambaa na nguo zilizogusa mwili wa Paulo, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakapona na pepo wakatoka ndani yao.
13
Na kulikuwa Wayuda wamoja waliotangatanga huku na huko kwa kufukuza pepo. Watu wale wakajaribu vilevile kutaja jina la Bwana Yesu, wakiwaambia vilevile pepo: “Ninawaamuru muondoke kwa jina la Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo.”
14
(Waliofanya hivi walikuwa wana saba wa Sikewa, Kuhani Mukubwa mumoja wa Wayuda.)
15
Lakini yule pepo akawajibu: “Ninamujua Yesu na ninamufahamu Paulo, lakini ninyi ni nani?”
16
Na yule mutu aliyekuwa na pepo ndani yake akawarukia, akawashinda wote nguvu na kuwatendea vibaya hata wakakimbia toka nyumba yake wakiwa uchi na wakijaa vidonda.
17
Wakaaji wote wa Efeso, Wayuda na Wagriki wakajua habari hii. Halafu wote wakashikwa na woga na wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
18
Wengi kati ya wale walioamini walikuja kuungama na kutangaza waziwazi mambo waliyofanya.
19
Na watu wengi kati ya wale waliofanya mambo ya uchawi wakaleta vitabu vyao vya uganga na wakavichoma mbele ya watu wote. Bei ya vitabu vile ilipohesabiwa, ikafikia vikoroti vya feza elfu makumi tano.
20
Ni hivi neno la Bwana lilivyoendelea kuenea fasi zote kwa uwezo wake na kuzidi kuonekana kuwa lenye nguvu.
21
Nyuma ya mambo yale, Paulo alikusudia kwenda Yerusalema, akipitia katika inchi ya Makedonia na katika jimbo la Akaya. Akasema: “Nikisha kufika kule, ni lazima niende Roma vilevile.”
22
Halafu akawatuma wawili kati ya wasaidizi wake, Timoteo na Erasto watangulie kwenda Makedonia. Yeye mwenyewe akabaki tena kwa muda katika jimbo la Azia.
23
Katika siku zile kulitokea fujo kubwa kwa ajili ya Njia ya Bwana.
24
Kulikuwa fundi mumoja wa kufua feza, jina lake Demetrio. Alikuwa akitengeneza sanamu ndogo za feza zinazofanana na hekalu la mungu muke Artemi. Na kwa njia ile aliwapatia wafundi faida kubwa.
25
Yeye alikusanya wale wafundi wote pamoja na watu wengine waliofanya kazi sawasawa na ile na kuwaambia: “Wandugu, munajua kwamba sisi tunapata mali mengi kwa njia ya kazi hii.
26
Sasa ninyi wenyewe munaona na kusikia namna huyu Paulo anayofanya. Amekwisha kuwavuta na kuwaonya watu wengi, si hapa Efeso tu, lakini ni karibu katika jimbo lote la Azia. Anasema kwamba miungu inayotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
27
Hivi kunakuwa hatari, na si kwa kazi hii yetu kuzarauliwa tu, lakini vilevile hekalu la mungu mukubwa muke, Artemi, litahesabiwa kuwa kitu bure. Na tena utukufu wake utapunguka, yeye anayeabudiwa na watu wote wa Azia na dunia nzima!”
28
Watu wale waliposikia maneno haya, wakajaa na hasira na kuanza kulalamika wakisema: “Artemi wa Waefeso atukuzwe!”
29
Fujo ikajaa katika muji wote. Wale watu wakawakamata wanainchi wa Makedonia, Gayo na Aristarko waliokuwa wakisafiri pamoja na Paulo. Nao wote pamoja wakawapeleka kwa haraka katika nyumba ya makutano.
30
Paulo alitaka kujionyesha mbele ya lile kundi la watu, lakini wanafunzi wakamukataza.
31
Hata wakubwa wamoja wa jimbo la Azia, waliokuwa warafiki zake wakamutumia ujumbe wakimusihi kwamba asiingie ndani ya nyumba ile.
32
Wakati ule, mukutano ulikuwa umejaa fujo kwa sababu watu wamoja walikuwa wakilalamika na kusema hivi na wengine hivi, na wengi kati yao hawakujua hata ni kwa sababu gani walikusanyika.
33
Watu wamoja katika mukutano wakaeleza mambo yaliyotokea kwa Alesanduro, yeye aliyesukumwa na Wayuda kwenda kusema mbele ya watu. Basi Alesanduro akainua mukono kwa kuwanyamazisha watu, kwa maana alitaka kujitetea mbele yao.
34
Lakini walipotambua kwamba yeye ni Muyuda, wakalalamika wote pamoja kwa muda wa saa mbili, wakisema: “Artemi wa Waefeso atukuzwe!”
35
Kwa mwisho katibu mukubwa wa muji akawatuliza watu, akisema: “Ninyi wanainchi wenzangu wa Efeso, watu wote wanajua kwamba ni wakaaji wa Efeso ndio wanaoshugulika na kulinda hekalu la mungu Artemi na sanamu yake iliyoshuka toka mbinguni.
36
Basi kwa maana hakuna anayeweza kukana maneno haya, ni lazima mutulie, wala musifanye kitu chochote kwa haraka.
37
Kwa maana mumewaleta watu hawa hapa, ingawa hawakuiba vitu vya hekalu, wala kumutukana mungu wetu.
38
Basi ikiwa Demetrio na wafundi wenzake wanakuwa na mashitaki juu ya mutu fulani, tuko na tribinali na wakubwa wako pale. Wanaweza kupeleka mashitaki yao kule!
39
Na kama mukiwa na neno lingine, litakatwa katika mukutano ulioruhusiwa.
40
Kwa maana kufuatana na mambo yaliyotukia leo, tunaweza kushitakiwa kwamba tumeleta fujo. Tena hakuna neno tunaloweza kusema kwa kueleza sababu ya kufanya mukutano huu.”
41
Kisha kusema maneno haya, akaaga mukutano.
← Chapter 18
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 20 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28