bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 16
Acts 16
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 17 →
1
Paulo akafika Derbe na Listra, ambako kulikuwa mwanafunzi mumoja aliyeitwa Timoteo. Mama yake alikuwa Muyuda, naye alikuwa ameamini lakini baba yake alikuwa Mugriki.
2
Nao wandugu waamini wa Listra na wa muji Ikonio walitoa ushuhuda muzuri juu ya Timoteo.
3
Paulo alitaka Timoteo amusindikize katika safari zake. Kwa hiyo akamutahiri kwa sababu ya Wayuda waliokaa katika pande zile, kwa maana wote walijua kwamba baba yake alikuwa Mugriki.
4
Na katika miji yote ambamo walipita walitangaza kwa wanafunzi yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee wa kanisa la Yerusalema, wakiwaomba wayashike.
5
Hivi makanisa yakaendelea kukomaa katika imani, nayo hesabu ya wanafunzi iliongezeka siku kwa siku.
6
Paulo na wale waliomusindikiza wakapita katika inchi ya Furigia na ya Galatia kwa sababu Roho Mutakatifu alikuwa amewakataza wasihubiri Neno la Mungu katika jimbo la Azia.
7
Nao walipofika katika wilaya ya Misia, wakajaribu kwenda katika jimbo la Bitinia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
8
Kwa hiyo wakapita Misia, wakatelemuka mpaka wakafika katika muji Troa.
9
Na ilipokuwa usiku akapata maono. Akaona mutu mumoja wa inchi ya Makedonia akisimama mbele yake akimusihi akisema: “Vuka, ufike kwetu Makedonia, utusaidie.”
10
Na pale pale kisha kupata maono yale, tukajitayarisha kwenda Makedonia, kwa maana tulitambua hakika kwamba Mungu alituita kwenda kuhubiri Habari Njema kule.
11
Basi tukasafiri ndani ya chombo kutoka Troa na kwenda mara moja mpaka Samotirake, na kesho yake tukafika Neapoli.
12
Kutoka kule tukafika mpaka Filipi, muji mukubwa wa inchi ya Makedonia uliokuwa chini ya utawala wa Waroma. Nasi tukakaa katika muji ule kwa muda wa siku chache.
13
Siku ya Sabato ilipotimia tukatoka ndani ya muji ule na kwenda karibu na muto mumoja, kwenye nafasi tulipozania kuwa ya kufanyia maombi. Tukaikaa na kusemezana na wanawake waliokusanyika pale.
14
Na kati ya wanawake wale kulikuwa mwanamuke mumoja aliyeitwa Ludia, wa muji Tuatera. Yeye alikuwa muchuuzi wa nguo nyekundu za bei kali na mwenye kuogopa Mungu. Mwanamuke yule akatusikiliza kwa maana Bwana alimufungua moyo kusudi apate kufuata kabisa maneno Paulo aliyosema.
15
Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.
16
Siku moja tulipokuwa tukienda kule kwenye nafasi ya kufanyia maombi, tukakutana na mujakazi mumoja. Yule mwanamuke alikuwa na pepo wa kuaguza ndani yake. Na kwa njia ya uaguzi ule aliwatajirisha wabwana wake.
17
Mwanamuke yule akaendelea kumufuata Paulo na sisi, akilalamika akisema: “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Mukubwa. Wanawatangazia ninyi namna gani munavyoweza kuokolewa.”
18
Naye akafanya hivi kwa muda wa siku nyingi. Na kwa mwisho Paulo akachukizwa naye. Basi akageuka na kumwambia yule pepo: “Ninakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, utoke ndani yake!” Na saa ile ile yule pepo akatoka ndani yake.
19
Halafu wabwana wa yule mujakazi wakaona kwamba hawataweza tena kupata mali kutoka kwa yule aliyekuwa kitumaini chao. Kwa hiyo wakakamata Paulo na Sila, wakawakokota na kuwapeleka mbele ya wakubwa kwenye nafasi ya makutano.
20
Walipowafikisha kwa watawala wa Waroma, wakasema: “Watu hawa ni Wayuda, nao wanaleta fujo katika muji wetu.
21
Wanafundisha desturi ambazo sisi Waroma tunakatazwa kukubali na kufuata.”
22
Basi kundi la watu waliokuwa pale wakawashambulia Paulo na Sila, nao watawala wakaamuru wawavue nguo kwa kinguvu na kuwapiga fimbo.
23
Walipokwisha kuwapiga sana, wakawatia ndani ya kifungo na kumwagiza mulinzi wa kifungo awachunge kabisa.
24
Na kufuatana na agizo lile, akawatia katika chumba cha ndani kabisa na kuwafungia miguu juu ya vipande vya miti kusudi ibaki imepanuka.
25
Na katikati ya usiku, Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za sifa, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
26
Kwa rafla kukatokea tetemeko kubwa la inchi hata misingi ya nyumba ya kifungo ikatikisika. Na pale pale milango yote ikafunguka na minyororo ya wafungwa wote ikakatika.
27
Mulinzi akaamuka, naye alipoona kwamba milango ilikuwa wazi, akachomoa upanga wake kusudi ajiue, kwa sababu aliwaza kama wafungwa wametoroka.
28
Lakini Paulo akalalamika kwa nguvu akisema: “Usijiue, kwa maana sisi wote tuko hapa!”
29
Basi yule mulinzi akaomba wamuletee taa, akarukia mbio ndani, akajitupa mbele ya Paulo na Sila, akitetemeka kwa hofu.
30
Kisha akawapeleka inje na kuwauliza: “Wabwana wangu, inanipasa kufanya nini kusudi nipate kuokolewa!”
31
Nao wakajibu: “Umwamini Bwana Yesu, nawe utaokolewa pamoja na watu wote wa nyumba yako.”
32
Halafu wakamwelezea neno la Bwana pamoja na watu wote wa nyumba yake.
33
Saa ile ile ya usiku mulinzi wa kifungo akawatwaa na kuwasafisha vidonda, naye akabatizwa pale pale na watu wake wote.
34
Kisha akapeleka Paulo na Sila ndani ya nyumba yake na kuwapatia chakula. Yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake walifurahi sana kwa sababu wamemwamini Mungu.
35
Na kesho yake kulipokucha, watawala wakatuma watumishi wamoja kwa yule mulinzi wa kifungo kwa kumwambia: “Uwafungue wale watu.”
36
Yule mulinzi wa kifungo akamwelezea Paulo habari ile akimwambia: “Wakubwa wametuma habari kwamba mufunguliwe. Basi sasa mutoke na kujiendea na amani.”
37
Lakini Paulo akawaambia wajumbe: “Wametupiga mbele ya watu wote bila kutusambisha, ijapokuwa sisi ni wanainchi wa Roma, na kisha wakatutia ndani ya kifungo. Na sasa namna gani wanataka kututosha kwa uficho? Haiwezekani! Wao wenyewe wafike kutufungua!”
38
Wale wajumbe wakarudi na kuwapasha wakubwa maneno yale. Nao waliposikia kwamba Paulo na Sila ni wanainchi wa Roma, wakaogopa sana.
39
Basi wakakuja, wakawabembeleza, wakawapeleka inje ya kifungo na kuwasihi watoke katika muji ule.
40
Paulo na Sila walipotoka ndani ya kifungo, wakaenda kwa Ludia. Nao walipokwisha kuonana na wandugu na kuwatia moyo, wakaondoka.
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 17 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28