bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 20
Acts 20
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 21 →
1
Fujo ilipokwisha, Paulo akawakusanya wanafunzi na kuwatia moyo. Kisha akaagana nao, akasafiri kwenda Makedonia.
2
Alipita katika inchi ile akiwaambia wanafunzi maneno mengi ya kuwatia moyo. Kisha akaenda Ugriki,
3
na kukaa kule kwa muda wa miezi mitatu. Alipokuwa tayari kuvuka na chombo kwenda katika inchi ya Suria, akapata habari kwamba Wayuda walimufanyia shauri baya. Kwa hiyo akakusudia kurudia, akipitia Makedonia.
4
Na hawa ndio watu waliokwenda pamoja naye: Sopateri mwana wa Piro, wa muji Beroya; Aristarko na Sekundo, wa muji Tesalonika; Gayo, wa muji Derbe; nao Timoteo, Tikiko na Trofimo, wa jimbo la Azia.
5
Watu hawa wakatutangulia kwenda Troa, nao wakatungojea kule.
6
Lakini nyuma ya sikukuu ya Mukate Usiotiwa Chachu, sisi tukaondoka katika muji Filipi kwa njia ya chombo. Na kisha safari ya siku tano tukawakuta Troa, nasi tukakaa kule kwa muda wa siku saba.
7
Siku ya kwanza ya juma, tulikuwa tunakusanyika kwa kumega mukate. Paulo akasemezana na watu na kuendelea kuwahubiria mpaka katikati ya usiku, kwa sababu alikusudia kuondoka kesho yake.
8
Na kulikuwa taa nyingi katika chumba cha gorofi tulichokusanyika ndani yake.
9
Kijana mumoja, aliyeitwa Eutiko, alikuwa akiikaa kwenye dirisha. Na kwa muda ule murefu Paulo alipofundisha, Eutiko akaanza kusinziasinzia na kwa mwisho akawezwa na usingizi na akaanguka chini toka kwenye gorofi ya tatu. Walipomunyanyua alikuwa amekwisha kufa.
10
Paulo akashuka chini, akajilaza juu yake na kumukumbatia akasema: “Musilie kwa maana angali muzima!”
11
Kisha Paulo akapanda juu tena kwenye gorofi, akamega mukate na kuukula. Akaendelea kuhubiri kwa muda murefu mpaka saa za mapambazuko, na kisha akaondoka.
12
Watu wakarudi na yule kijana, akiwa muzima nao wakafarijiwa sana.
13
Sisi tulitangulia tukaingia ndani ya chombo na kusafiri kwenda Asosi. Kule tulipaswa kumutwaa Paulo sawa alivyotuagiza, kwa maana alikuwa amekusudia kwenda kule kwa miguu.
14
Alipokuwa Asosi, tukamwingiza ndani ya chombo na kwenda pamoja naye mpaka Mitilene.
15
Kesho yake tukaondoka kule kwa njia ya chombo na kufika kwenye kisanga cha Kio, na kesho kutwa tukafika kwenye kisanga cha Samosi. Na siku iliyofuata tukafika Mileto.
16
Paulo alikuwa amekusudia kupita Efeso kwa chombo pasipo kuezeka kule, kusudi asikawie katika jimbo la Azia. Kwa maana alikuwa na haraka ya kufika Yerusalema mbele ya siku ya Pentekoste kama ikiwezekana.
17
Toka Mileto, akatuma ujumbe Efeso kwa kuwaita wazee wa kanisa.
18
Nao walipofika, akawaambia: “Ninyi munajua namna nilivyoishi wakati wote nilipokuwa pamoja nanyi, tangia siku ile ya kwanza nilipofika katika jimbo la Azia.
19
Nilimutumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi na katika majaribu niliyopata kwa ajili ya mashauri mabaya Wayuda waliyonifanyia.
20
Munajua kwamba sikuwaficha hata neno moja lenye kuwafalia ninyi, lakini niliwahubiri na kuwafundisha katika mikutano na katika nyumba zenu.
21
Nimewaonya Wayuda wa mataifa mengine kwamba wanapaswa kumugeukia Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.
22
Basi sasa kwa kuwa ninalazimishwa na Roho Mutakatifu, nitakwenda Yerusalema pasipo kujua mambo yatakayonitokea kule.
23
Lakini kitu kimoja ninachojua tu, ni kwamba katika kila muji Roho Mutakatifu ananihakikishia kwamba vifungo na mateso vinaningojea.
24
Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.
25
“Nilikuwa nikizungukazunguka kati yenu ninyi wote nikitangaza Ufalme wa Mungu. Lakini sasa, ninajua kwamba hakuna hata mumoja atakayeniona tena.
26
Ndiyo maana ninahakikisha mbele yenu leo kwamba mimi sitabeba lazima ya damu ya hata mumoja wenu atakayepotea.
27
Ni vile kwa sababu niliwatangazia mupango wote wa Mungu pasipo kuwaficha kitu.
28
Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.
29
Ninajua kwamba nyuma ya kuondoka kwangu, imbwa wakali wa pori wataingia katikati yenu, nao hawatahurumia kundi lile.
30
Na hata kati yenu kutatokea watu watakaotoa mafundisho ya kupotosha wengine kusudi wawavute waamini kuwafuata.
31
Kwa sababu hii mujiangalie, mukikumbuka kwamba kwa muda wa miaka mitatu, usiku na muchana, sikuchoka kumwonya kila mumoja wenu kwa machozi.
32
“Basi sasa ninawaweka chini ya ulinzi wa Mungu na wa neno lake la neema linaloweza kuwajenga katika imani na kuwapa urizi pamoja na watu wake wote watakatifu.
33
Mimi sikutamani feza, zahabu, wala nguo ya mutu yeyote.
34
Ninyi wenyewe munajua namna nilivyotumika kwa mikono yangu mimi peke kwa kupata vitu vyote ambavyo mimi pamoja na wenzangu tulihitaji.
35
Katika mambo hayo yote niliyofanya, nimewaonyesha mufano kwamba tunapaswa kusumbuka vile na kazi kwa kuwasaidia wasiojiweza, tukikumbuka maneno haya Bwana Yesu mwenyewe aliyosema: ‘Ni heri kutoa kuliko kupewa.’ ”
36
Paulo alipokwisha kusema maneno haya, akapiga magoti pamoja nao wote na kuomba.
37
Na wote walilia sana wakimukumbatia na kumubusu.
38
Walihuzunika zaidi kwa sababu aliwaambia kwamba hawatamwona tena. Wakamusindikiza mpaka kwenye chombo.
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 21 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28