bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 28
Acts 28
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 27
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
1
Tulipokwisha kuponyoka kufa, ndio wakati tulijua kwamba kisanga kile tulichokuwa ndani yake kinaitwa Melita.
2
Wenyeji wa kule wakatutendea mema sana. Mvua ilikuwa imeanza kunyesha na kulikuwa baridi, kwa hiyo watu wale wakatukongea moto na kutukaribisha sisi wote.
3
Paulo akatwaa lundo ya kuni, na alipokuwa akiiweka ndani ya moto, nyoka akatoka katikati ya ile lundo kwa sababu ya kivukuto na kujizingia kwa mukono wake.
4
Wale wenyeji wa kule walipoona nyoka yule anajizingia kwa mukono wake wakasemezana: “Hakika mutu huyu ni mwuaji, kwa maana ijapokuwa alipona katika hatari ya bahari, kufuatana na azabu ya haki ya Mungu, kufa kwake kunatimia.”
5
Lakini Paulo akamukungutia yule nyoka katika moto wala hakumuzuru hata kidogo.
6
Nao watu wale walingojea kuona ikiwa atavimba mukono au ataanguka mara moja na kufa. Lakini kisha kungoja muda murefu na kuona kwamba hakupata hasara yoyote, wakabadilisha mawazo yao hata wakasema kwamba yeye ni mumoja wa miungu.
7
Karibu na pale kulikuwa mashamba ya mukubwa wa kisanga, aliyeitwa Publio. Mutu yule akatukaribisha kwa upendo na kutupangisha ndani ya nyumba yake kwa muda wa siku tatu.
8
Baba ya Publio alikuwa amelala kwa ajili ya kuwezwa na ugonjwa wa homa na wa kuhara damu. Paulo akaenda kumwangalia, akamwombea na kuweka mikono juu yake, naye akapona.
9
Na kufuatana na jambo hilo, wagonjwa wengine waliokaa katika kisanga kile wakakuja, nao wakaponyeshwa vilevile.
10
Watu wakatuheshimu sana, na wakati tulipoondoka kwa njia ya chombo kwa kuendelea wakatupatia vitu vyote tulivyohitaji kwa safari yetu.
11
Kulipopita miezi mitatu, tukasafiri katika chombo kimoja kilichobaki katika kisanga kile kwa kungojea wakati wa baridi kali upite kwanza. Chombo kile kilikuwa chenye kutoka Alesanduria. Na juu yake kulikuwa michoro ya sanamu za mapacha ya miungu.
12
Tulipofika Sirakuse, tukakaa kule kwa muda wa siku tatu.
13
Kutoka kule tukazunguka pembenipembeni ya bahari hata tukafika katika muji Regio. Kesho yake upepo usiokuwa mukali ukaanza kuvuma tokea kusini, na kwa mwendo wa siku mbili tukafika katika muji Puteoli.
14
Kule tukakuta wandugu waamini, nao wakatualika tukae pamoja nao kwa muda wa juma moja. Ni vile tulivyosafiri hata kufika Roma.
15
Wandugu waamini wa Roma waliposikia habari zetu wakakuja kutuona kwenye Soko la Apio na wengine kwenye Tiretaberne. Paulo alipowaona, akamushukuru Mungu na kutiwa tena moyo.
16
Tulipofika Roma, Paulo akapewa ruhusa ya kujilipia nyumba ya kupanga ambamo atakaa pamoja na askari mumoja mwenye kumuchunga.
17
Kulipopita siku tatu, Paulo aliwaita wakubwa wa Wayuda waliokaa kule. Na walipokwisha kukusanyika akawaambia: “Wandugu, mimi nilifungwa kule Yerusalema na kutolewa kwa Waroma ijapokuwa sikufanya kosa lolote juu ya taifa letu wala kuvunja desturi za babu zetu.
18
Nao walipokwisha kunisambisha, walitaka kunifungua kwa sababu hawakuniona na kosa linalonipasa kuuawa.
19
Lakini nilipoona kwamba Wayuda wanakataa shauri lile, ilinilazimisha kuomba nisambishwe na Mufalme wa Roma. Na katika haya yote sikukuwa na mashitaki yoyote juu ya taifa langu.
20
Basi ni kwa sababu hii nimewaita kusudi tuonane na niseme nanyi, kwa maana ninafungwa na munyororo huu kwa ajili ya tumaini ambalo Waisraeli wanakuwa nalo.”
21
Wakamwambia: “Sisi hatukupokea barua juu yako toka Yudea, wala ndugu Muyuda aliyefika huku kwa kutupasha habari, wala kusema ubaya juu yako.
22
Lakini tungependa kusikia mawazo yako kwa maana tunajua kwamba fasi zote watu wanapinga dini hii unayofuata.”
23
Halafu wakapanga siku ya kukutana na Paulo. Na siku ile watu wengi zaidi wakamufikia pahali alipopanga. Na tangu asubui mpaka magaribi Paulo akawaelezea mambo mengi na kutoa ushuhuda juu ya habari za Ufalme wa Mungu. Alitaka wasadiki habari za Yesu akitaja maneno ya Sheria ya Musa na ya vitabu vya manabii.
24
Wamoja wakasadiki maneno yaliyosemwa, lakini wengine hawakuyaamini.
25
Nao walipokuwa wakiondoka bila kupatana, Paulo akaongeza kuwaambia maneno haya tu: “Roho Mutakatifu alikuwa na sheria ya kusema hivi kwa babu zenu kwa njia ya nabii Isaya:
26
Uwaendee watu hawa na kuwaambia: Kusikia mutasikia, lakini hamutafahamu. Kuangalia mutaangalia, lakini hamutatambua.
27
Maana mioyo ya watu hawa imegeuka kuwa migumu, wameziba masikio yao na wamefunga macho yao. Isingekuwa hivi, wangeona na macho yao, wangesikia na masikio yao, wangefahamu na mioyo yao, na wangegeukia kwangu na ningewaponyesha.
28
“Na kwa kumaliza, basi mujue kwamba habari ya wokovu huu wa Mungu imetumwa kutangazwa kwa watu wa mataifa mengine, nao wataisikia!” [
29
Paulo alipokwisha kusema maneno haya, Wayuda wakaenda wakibishana sana wao kwa wao.]
30
Paulo akakaa miaka miwili katika nyumba aliyokuwa akijilipia yeye mwenyewe. Alikaribisha watu wote waliokuja kumwona.
31
Alihubiri habari za Ufalme wa Mungu na kuwafundisha watu juu ya Bwana Yesu Kristo bila woga na bila kuzuizwa.
← Chapter 27
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28