bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 22
Acts 22
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 23 →
1
“Wandugu zangu na wababa zangu, musikilize yale ninayotaka kusema kwa kujitetea mbele yenu.”
2
Walipomusikia akisema nao katika luga ya Kiebrania, wakanyamaza zaidi. Halafu Paulo akasema:
3
“Mimi ni Muyuda, nimezaliwa Tarso, katika jimbo la Kilikia, lakini nililelewa katika muji huu wa Yerusalema. Mimi nilikuwa mwanafunzi wa Gamalieli, na alinifundisha namna ya kufuata kabisa Sheria ya babu zetu. Nikajitolea kabisa kwa kutumikia Mungu kama vile ninyi wote munavyofanya leo.
4
Mimi niliwatesa hata kuwaua watu waliofuata Njia ya Bwana. Niliwakamata wanaume na wanawake na kuwatupa katika kifungo.
5
Hata Kuhani Mukubwa pamoja na baraza lote la wasimamizi wa watu wanaweza kushuhudia kwamba ninasema kweli. Nilipata hata barua toka kwao iliyoandikwa kwa ajili ya wandugu Wayuda wa Damasiki. Nikaenda kule kusudi niwafunge waamini waliokuwa kule na kuwaleta mpaka Yerusalema wapate kuazibiwa.
6
“Nilipokuwa katika safari karibu kufika Damasiki, yapata saa sita ya muchana, kwa rafla mwangaza mukubwa toka mbinguni ukanizunguka.
7
Nikaanguka chini, nikasikia sauti ikiniambia: ‘Saulo, Saulo, kwa sababu gani unanitesa?’
8
Nami nikauliza: ‘Wewe ni nani, Bwana?’ Na Bwana akanijibu: ‘Mimi ni Yesu wa Nazareti unayemutesa.’
9
Watu waliokuwa pamoja nami wakaona mwangaza ule, lakini hawakusikia sauti ya yule aliyekuwa akinisemesha.
10
Nikauliza: ‘Bwana, nifanye nini?’ Naye Bwana akanijibu: ‘Simama, uende Damasiki, na kule watakuambia mambo yote Mungu anayokuagiza kufanya.’
11
Na kwa kuwa nilikuwa sioni tena kwa sababu ya ukali wa ule mwangaza, wenzangu wakanishika mukono na kuniongoza mpaka nikafika Damasiki.
12
“Kule Damasiki kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Anania, mutu aliyeogopa Mungu na mwenye kushika Sheria yetu. Aliheshimiwa sana na Wayuda wote waliokaa kule.
13
Yeye akanifikia, akasimama karibu nami na kuniambia: ‘Ndugu yangu Saulo, upate kuona tena!’ Na saa ile ile nikapata kuona na kuweza kumwona.
14
Kisha akasema: ‘Mungu wa babu zetu amekwisha kukuchagua wewe kusudi ujue mapenzi yake. Anataka umwone Mwenye Haki, na kumusikia akisema kwa kinywa chake mwenyewe.
15
Kwa maana utatoa ushuhuda wake kwa watu wote, utasema juu ya mambo yale uliyoona na kuyasikia.
16
Basi sasa, unangojea nini? Simama ubatizwe na kuondolewa zambi zako, ukiomba kwa jina la Bwana.’ ”
17
“Nilipokuwa nimekwisha kurudia Yerusalema, na nilipokuwa nikiomba katika hekalu, nikapata maono.
18
Nikamwona Bwana, naye akaniambia: ‘Fanya haraka uondoke upesi katika muji huu Yerusalema kwa sababu watu wake hawatakubali ushuhuda utakaoutoa juu yangu.’
19
Nami nikajibu: ‘Bwana, watu hawa wanajua wazi kwamba nilikuwa nikipitapita katika nyumba za kuabudia kwa kuwafunga na kuwapiga wale wanaokuamini.
20
Na wakati watu walipomwua Stefano, aliyetoa ushuhuda juu yako, mimi mwenyewe nilikuwa pale, nami nilikuwa nimekubaliana nao juu ya kuuawa kwake. Na zaidi ya ile ni mimi niliyechunga nguo za wale waliomwua.’
21
Halafu Bwana akaniambia: ‘Kwenda, kwa maana nitakutuma mbali kwa watu wa mataifa mengine.’ ”
22
Makutano walimusikiliza Paulo mpaka aliposema maneno yale. Kisha wakasema kwa nguvu: “Mumuteketeze mutu huyu! Mumwue, kwa maana hastahili kuishi!”
23
Wakalalamika sana, wakatupatupa nguo zao na kurusha mavumbi juu.
24
Yule mukubwa wa jeshi akaamuru waaskari wamupeleke Paulo katika upango wao. Akaamuru vilevile wamupige fimbo, kusudi apate kujua sababu gani watu walilalamika vile kwa ajili yake.
25
Lakini walipokwisha kumufunga Paulo na kamba kusudi wamupige, yeye akamwambia jemadari mumoja aliyekuwa pale: “Sheria inawaruhusu kumupiga mwanainchi wa Roma, ingawa hajahukumiwa bado?”
26
Yule jemadari aliposikia maneno hayo akaenda kwa yule mukubwa wa jeshi kwa kumupasha na kumwuliza: “Unataka kufanya nini? Mutu huyu ni mwanainchi wa Roma!”
27
Basi jemadari akamwendea Paulo kumwuliza: “Uniambie ukweli, wewe ni mwanainchi wa Roma?” Paulo akamujibu: “Ndiyo.”
28
Halafu mukubwa wa jeshi akasema: “Mimi nilinunua haki ya kuwa mwanainchi wa Roma kwa feza nyingi.” Paulo akamwambia: “Mimi ni mwanainchi wa Roma kwa kuzaliwa.”
29
Mara moja wale waliotaka kumusambisha kwa kumupiga fimbo wakamwacha. Yule mukubwa wa jeshi akaogopa alipotambua kwamba Paulo ni mwanainchi wa Roma, na kwamba alikuwa anamufunga na minyororo.
30
Kesho yake, jemadari alitaka kujua mashitaki kamili ya Wayuda juu ya Paulo. Kwa hiyo akamufungua na kuamuru wakubwa wa makuhani pamoja na Baraza Kubwa wafanye mukutano. Kisha akamuleta Paulo na kumusimamisha mbele yao.
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 23 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28