bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 15
Acts 15
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 16 →
1
Watu wamoja walishuka toka Yudea kwenda Antiokia, nao wakaanza kuwafundisha wandugu waamini kwamba hawawezi kuokoka ikiwa hawatahiriwi sawa vile inavyoagizwa katika Sheria ya Musa.
2
Basi Paulo na Barnaba wakapingana na kubishana nao vikali sana juu ya jambo hili. Na kwa hiyo wandugu waamini wakaagiza Paulo na Barnaba pamoja na watu wengine kati yao waende Yerusalema kusemezana na mitume na wazee wa kanisa la kule juu ya maneno yale.
3
Kanisa liliwapatia vitu walivyohitaji kwa ajili ya safari ile, nao wakapita katika inchi ya Foinikia na katika Samaria. Na kule wakaeleza namna watu wa mataifa mengine walivyomugeukia Mungu. Habari hii ikafurahisha sana wandugu waamini wote.
4
Walipofika Yerusalema, wakakaribishwa na kanisa pamoja na mitume na wazee, nao wakawaelezea mambo yote Mungu aliyofanya kwa njia yao.
5
Lakini wanafunzi wamoja waliokuwa katika chama cha Wafarisayo wakasimama na kusema: “Sherti watu wa mataifa mengine walioamini watahiriwe na kuagizwa wafuate Sheria ya Musa.”
6
Halafu mitume na wazee wa kanisa wakakusanyika kusudi wachunguze neno hili.
7
Mabishano yalipoendelea, Petro akasimama na kusema: “Wandugu zangu, munajua kwamba Mungu alinichagua pale zamani kati yenu kusudi nihubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine wapate kuisikia na kuamini.
8
Naye Mungu anayejua mafikiri ya mutu, alihakikisha kwamba amewakubali watu wa mataifa mengine kwa njia ya kuwapatia Roho Mutakatifu sawa vile alivyotupatia sisi.
9
Yeye hakufanya ubaguzi kati yetu na wao; ametakasa mioyo yao kwa sababu walimwamini.
10
Basi sasa, kwa nini munataka kumupima Mungu kwa kuwabebesha muzigo ambao wala babu zetu, wala sisi wenyewe hatukuweza kuubeba?
11
Haipaswi kuwa vile, kwa maana sisi na wao vilevile tunaamini kwamba sisi wote tunaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu.”
12
Basi mukutano wote ukabaki kimya ukisikiliza maelezo ya Barnaba na Paulo juu ya vitambulisho na maajabu yote Mungu aliyofanya kwa njia yao katikati ya watu wa mataifa mengine.
13
Nao walipomaliza kusema, Yakobo akajibu, akisema: “Wandugu zangu, munisikilize!
14
Simoni anatoka kutuelezea namna Mungu alivyowashugulikia watu wa mataifa mengine pale mbele kusudi ajichagulie wamoja kati yao kuwa watu wake wa pekee.
15
Na jambo hilo linapatana na maneno haya ya manabii yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu:
16
‘Nyuma ya mambo haya nitarudi, nitaimarisha tena ufalme wa Daudi, nitausimamisha tena sawa wanavyojenga tena nyumba iliyoanguka,
17
kusudi watu wote wengine wamugeukie Bwana, watu wa mataifa yote wapate kuwa watu wangu wa pekee.
18
Ni vile Bwana anavyosema, yeye aliyejulisha mambo haya tangu zamani za kale.’ ”
19
Yakobo akaendelea kusema: “Ni kwa sababu hii, mimi ninaona kwamba haifai tuwasumbue watu wa mataifa mengine wanaomugeukia Mungu.
20
Lakini inafaa tuwaandikie kwa kuwaambia kwamba wajitenge na vitu vilivyochafuliwa kwa kutambikia sanamu, waepuke uasherati na wasikule nyamafu wala damu.
21
Kwa maana tangu zamani Sheria ya Musa inasomwa kila siku ya Sabato katika nyumba za kuabudia na kuhubiriwa katika kila muji.”
22
Halafu mitume na wazee wakakata shauri pamoja na kanisa lote la Yerusalema kwamba wachague watu wamoja kati yao na kuwatuma kwenda Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Wakachagua Yuda aliyeitwa vilevile Barisaba, pamoja na Sila. Watu hawa wawili walihesabiwa na wandugu waamini kuwa wenye heshima sana.
23
Nao wakawatuma na barua iliyoandikwa hivi: “Sisi mitume na wazee wa kanisa na wandugu zenu, tunawasalimu ninyi wandugu zetu waamini wa mataifa mengine munaokuwa katika muji wa Antiokia na katika jimbo la Suria na la Kilikia.
24
Tumesikia kwamba watu fulani waliotoka huku kwetu pasipo ruhusa yetu wamewasumbua ninyi na maneno na kuwatia katika wasiwasi.
25
Kwa sababu hii sisi tumekata shauri kwa nia moja, tukapatana kuchagua watu wamoja na kuwatuma kwenu. Watu hawa watawafikia pamoja na wapendwa wetu, Barnaba na Paulo,
26
waliotoa maisha yao kwa ajili ya kumutumikia Bwana wetu Yesu Kristo.
27
Ni hivi tunawatuma kwenu Yuda na Sila, nao watawaelezea waziwazi kwa kinywa maneno haya tunayowaandikia.
28
Kwa maana kutokana na shauri la Roho Mutakatifu na shauri letu wenyewe tumeamua kwamba hatutawabebesha muzigo mwingine muzito kupita mapaswa haya ya lazima:
29
musikule vyakula vilivyotolewa kwa kutambikia sanamu; musikule damu wala nyamafu; na muepuke uasherati. Mutafanya vema kama mukijitenga na mambo haya. Salamu kwenu.”
30
Kisha kuagana, wale wajumbe wakaondoka na kwenda Antiokia. Kule wakakusanya kundi lote la waamini, wakawapa barua ile.
31
Nao walipoisoma wakafurahi kwa ajili ya maneno ya kuwatia moyo yaliyoandikwa ndani yake.
32
Na kufuatana na vile Yuda na Sila walivyokuwa manabii, wakawaonya kwa maneno mengi na kuwajenga moyo.
33
Kisha kukaa kule kwa muda, wandugu waamini wakawaaga na kuwatakia amani wakawaruhusu kurudi kwa wale waliowatuma. [
34
Lakini Sila akaona vizuri kubakia kule.]
35
Naye Paulo na Barnaba wakabakia Antiokia, na kule wao pamoja na watu wengine wengi walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.
36
Nyuma ya siku chache, Paulo akamwambia Barnaba: “Turudi sasa kwa kuwaangalia wandugu waamini katika miji ambamo tulihubiri neno la Bwana, kusudi tuone kama wako katika hali gani.”
37
Barnaba alitaka waende pamoja na Yoane, aliyeitwa vilevile Marko.
38
Lakini Paulo hakuona vizuri kwenda naye kwa sababu alikuwa ameachana nao katika inchi ya Pamfilia, akikataa kuendelea nao katika kazi.
39
Kwa hiyo Paulo na Barnaba wakabishana vikali hata wakatengana. Barnaba akaondoka pamoja na Marko, wakaingia ndani ya chombo na kwenda katika kisanga cha Kipuro.
40
Naye Paulo akachagua kwenda na Sila, nao wandugu waamini walipokwisha kuwaombea neema kwa Mungu, wakaondoka.
41
Akapita katika jimbo la Suria na Kilikia, na kule akayatia makanisa nguvu.
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 16 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28