bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 26
Acts 26
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 27 →
1
Agripa akamwambia Paulo: “Sasa unaweza kueleza maneno yako.” Basi Paulo akanyoosha mukono na kuanza kujitetea, akisema:
2
“Mufalme Agripa, ninafurahi sana kusimama mbele yako leo kwa kujitetea juu ya mambo yote Wayuda waliyonishitakia.
3
Ninafurahi zaidi kwa sababu wewe unajua sana desturi zote za Wayuda na mabishano yao yote. Basi ninakuomba unisikilize kwa uvumilivu.
4
“Wayuda wote wanajua maisha yangu tangu mwanzo wa ujana wangu. Wanajua namna nilivyoishi kati ya taifa langu katika Yerusalema.
5
Wamenijua tangu zamani na kama wakitaka wanaweza kushuhudia kwamba nilikuwa mushiriki wa chama cha Wafarisayo, kinachotia mukazo sana juu ya kushika desturi za dini yetu.
6
Na sasa ninasimama hapa kuhukumiwa kwa sababu ninatumainia ile ahadi Mungu aliyotoa kwa babu zetu.
7
Makabila yetu kumi na mawili wanamwabudu Mungu usiku na muchana, kwa maana wanatumaini kuona utimilifu wa ile ahadi. Na ni kwa sababu ya tumaini lile, Ee mufalme, Wayuda wananishitaki.
8
Kwa sababu gani ninyi munazani kwamba haiwezekani kwa mutu kusadiki kwamba Mungu anawafufua wafu?
9
“Kweli mimi mwenyewe niliwaza kwamba nilipaswa kufanya yote ninayoweza kwa kupinga jina la Yesu wa Nazareti.
10
Na ni vile nilivyofanya katika Yerusalema. Nilipata mamlaka toka kwa wakubwa wa makuhani; nami nikawatia watu watakatifu wengi wa Mungu katika kifungo. Na wakati walipowaua mimi nilikubali kwamba wanastahili kuuawa.
11
Mara nyingi niliwaazibu katika nyumba za kuabudia na kuwashurutisha wakane imani yao. Niliwakasirikia kupita kipimo, hata nikaenda kuwatesa katika miji ya inchi za kigeni.
12
“Basi kufuatana na kusudi, nikaenda katika muji Damasiki kwa amri na mamlaka ya wakubwa wa makuhani.
13
Ee mufalme, nilipokuwa katika njia, ilipotimia saa sita ya muchana, nikaona mwangaza unaotoka mbinguni unaopita mwangaza wa jua. Mwangaza ule ukanizunguka pamoja na wenzangu waliosafiri nami.
14
Sisi wote tukaanguka chini, na nikasikia sauti iliyoniambia hivi katika luga ya Kiebrania: ‘Saulo, Saulo, kwa sababu gani unanitesa? Unajiumiza bure kama ngombe anayepiga teke kwenye chongo ya fimbo ya mwenyeji wake.’
15
Halafu nikauliza: ‘Wewe ni nani, Bwana?’ Na Bwana akajibu: ‘Mimi ni Yesu, unayemutesa.
16
Lakini sasa inuka usimame wima. Nimekutokea kusudi nikuweke kuwa mutumishi wangu. Wewe utatoa ushuhuda juu yangu; utawaelezea watu mambo uliyoona leo na yale nitakayokuonyesha nyuma.
17
Nitakuokoa toka mikono ya taifa lako la Waisraeli na ya watu wa mataifa mengine. Ninakutuma kwao
18
kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’
19
“Kwa sababu hii, Ee mufalme Agripa, mimi nikafanya sawa nilivyoagizwa katika maono yale yaliyotoka mbinguni.
20
Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.
21
Ni kwa sababu ya maneno hayo Wayuda walinikamata ndani ya hekalu na kutaka kuniua.
22
Lakini kwa ulinzi wa Mungu ningali muzima hata leo. Nami ninatoa ushuhuda kwa wadogo na wakubwa, wala sisemi maneno mengine yanayokuwa mbali na yale manabii na Musa waliyosema kwamba yatatokea.
23
Wao walitangaza kwamba Kristo anapaswa kuteswa na kuwa wa kwanza kufufuka kati ya wote waliokufa, naye atahubiri kwa Wayuda na kwa watu wa mataifa mengine kwamba kwa njia ya kuokolewa wataweza kuishi katika mwangaza.”
24
Paulo alipokuwa akijitetea vile, Festo akamwambia kwa sauti kubwa: “Wewe Paulo, uko na wazimu! Elimu yako nyingi imekuvuruga kichwa.”
25
Paulo akamujibu: “Muheshimiwa Festo, mimi si mwenda-wazimu. Maneno ninayosema ni ya kweli nayo ni ya maana.
26
Mufalme Agripa anajua vizuri mambo yale yaliyotokea. Nami ninaweza kusema mbele yake pasipo woga kwa maana ninajua hakika kwamba hakuna hata jambo kati ya hayo asilofahamu, kwa sababu hayakufanyika kwa uficho.
27
Ee Mufalme Agripa, unaamini maneno manabii waliyosema? Ninajua kama unayaamini!”
28
Naye Agripa akamwambia Paulo: “Unazani kwamba kwa wakati kidogo utaweza kunivuta kuwa mukristo?”
29
Paulo akajibu: “Ikiwa wakati kidogo au wakati murefu, ninamwomba Mungu, si juu yako wewe mwenyewe tu, lakini hata hawa wote wanaonisikiliza leo wapate kuwa sawa mimi, lakini wasifikie tu kutiwa katika kifungo!”
30
Halafu mufalme, liwali, Berenike na wote wengine walioikaa pamoja nao wakasimama.
31
Nao walipokwisha kuondoka wakasemezana: “Mutu huyu hakutenda neno linalomupasa kuuawa wala kufungwa.”
32
Agripa akamwambia Festo: “Mutu huyu angeweza kufunguliwa, kama isingekuwa ameomba maneno yake yakatwe na Mufalme wa Roma.”
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 27 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28