bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 4
Acts 4
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 5 →
1
Petro na Yoane walipokuwa wangali wakisema mbele ya watu, makuhani, mukubwa wa walinzi wa hekalu pamoja na Wasadukayo wakafika.
2
Wao walichukizwa sana kwa sababu wale mitume wawili walikuwa wakiwafundisha watu na kutangaza kwao kwamba Yesu alifufuka, nao ufufuko wake unahakikisha kwamba wafu watafufuka.
3
Kwa hiyo wakawakamata na kuwatia katika kifungo mpaka kesho yake kwa maana ilikuwa imekwisha kuwa magaribi.
4
Lakini wengi kati ya watu waliosikia mafundisho ya Petro na Yoane wakaamini. Kadiri ya watu elfu tano wakaongezeka katika kundi la waamini.
5
Kesho yake, wasimamizi wa Wayuda, wazee na walimu wa Sheria wakakusanyika Yerusalema.
6
Kulikuwa vilevile Kuhani Mukubwa Anasi, Kayafa, Yoane, Alesanduro na watu wengine wote wa ukoo wa Kuhani Mukubwa.
7
Wakasimamisha Petro na Yoane mbele yao na kuwauliza: “Ni kwa uwezo gani au kwa jina la nani ninyi mumefanya jambo lile?”
8
Halafu Petro akiwa amejazwa na Roho Mutakatifu, akawajibu: “Ninyi wasimamizi wa watu, nanyi wazee:
9
Sisi tunasambishwa leo juu ya wema tuliomutendea mutu huyu aliyekuwa kiwete na juu ya namna alivyoponyeshwa.
10
Kwa hiyo, ninyi wote pamoja na Waisraeli wote mujue vizuri kwamba mutu huyu anayesimama mbele yenu akiwa muzima kabisa, ni kwa uwezo wa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, yule muliyemutundika juu ya musalaba, lakini Mungu amemufufua.
11
Yeye ndiye Maandiko Matakatifu yanayosema hivi juu yake: ‘Jiwe lililokataliwa na ninyi wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.’
12
“Hivi hakuna anayeweza kuokolewa kwa njia ya mutu mwingine yeyote, kwa maana katika dunia nzima hakuna jina lingine lolote watu walilopewa lenye uwezo wa kuwaokoa.”
13
Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.
14
Lakini kufuatana na vile walivyomwona mutu yule aliyeponyeshwa akisimama pale pamoja nao, wakakosewa na la kusema.
15
Basi wakawaamuru watoke katika Baraza Kubwa na kwenda inje, nao wakaulizana shauri wao kwa wao,
16
wakisema: “Tutafanya nini na watu hawa? Wakaaji wote wa Yerusalema wanajua kwamba wameonyesha vitambulisho, nasi hatuwezi kukana jambo lile.
17
Lakini kwa kuzuiza habari za jambo lililotokea zisisambae zaidi kati ya watu, tuwakataze kwa ukali wasiendelee tena kusema na mutu yeyote wakitaja jina la Yesu.”
18
Kisha wakawaita tena na kuwakataza kabisa kusema na kufundisha kwa jina la Yesu.
19
Lakini Petro na Yoane wakawajibu: “Muamue ninyi wenyewe, ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumutii Mungu?
20
Kwa maana sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”
21
Kisha wale wakubwa wa baraza wakawakataza tena kwa ukali na kuwaachilia kwenda. Hawakupata njia ya kuwaazibu kwa maana watu wote walikuwa wakimusifu Mungu kwa ajili ya jambo lile lililotendeka.
22
Naye yule mutu aliyeponyeshwa kwa njia ya kitambulisho hiki, alikuwa na umri wa miaka zaidi ya makumi ine.
23
Petro na Yoane walipofunguliwa wakarudi kwa wenzao na kuwaelezea maneno yote wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu waliyowaambia.
24
Nao waliposikia habari hii, wote wakamwomba Mungu kwa nia moja, wakisema: “Ee Bwana, ni wewe uliyeumba mbingu, dunia na bahari na vitu vyote vinavyokuwa ndani yao.
25
Ni wewe uliyesema maneno haya kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa kinywa cha mutumishi wako babu yetu mukubwa Daudi: ‘Kwa nini mataifa wanafanya fujo, na kwa nini watu wanafanya mipango ya ovyo?
26
Wafalme wanajikusanya, wakubwa wanafanya shauri wapate kumwasi Bwana, naye Kristo aliyemuchagua.’
27
“Ndiyo, ni kweli mufalme Herode, naye mutawala Pontio Pilato walikusanyika katika muji huu pamoja na Waisraeli na watu wa mataifa mengine kwa kufanya shauri baya juu ya mutumishi wako mutakatifu Yesu, uliyemuchagua kuwa Kristo.
28
Hivi walitimiza mambo uliyokuwa umekusudia tangu zamani kwa uwezo wako na kwa mapenzi yako.
29
Na sasa Ee Bwana, angalia vitisho vyao. Basi utuwezeshe sisi watumishi wako tupate kutangaza neno lako kwa uhodari kabisa.
30
Utumie nguvu zako kwa kuponyesha watu, kwa kufanya maajabu na vitambulisho kwa uwezo wa jina la mutumishi wako mutakatifu Yesu.”
31
Walipokwisha kuomba, nafasi ile walipokuwa wakikusanyika ikatikisika. Nao wote wakajazwa na Roho Mutakatifu na kuanza kutangaza Neno la Mungu kwa uhodari.
32
Kundi lote la waamini walikuwa na roho moja na nia moja. Hakuna hata mumoja wao aliyehesabia mali yake kuwa yake mwenyewe, lakini walishirikiana katika vitu vyote.
33
Nao mitume walishuhudia ufufuko wa Bwana Yesu kwa uwezo mukubwa, na Mungu akawabariki wote sana.
34
Hakuna hata mutu mumoja kati ya wanafunzi aliyekuwa mukosefu. Kwa maana wale waliokuwa na mashamba au nyumba waliziuzisha na kuleta feza waliyopata
35
kwa mikono ya mitume. Nao walizigawanya kwa watu wote kufuatana na mahitaji ya kila mumoja.
36
Na kulikuwa Mulawi mumoja muzaliwa wa kisanga cha Kipuro, jina lake Yosefu. Mitume walimwita kwa jina lingine la Barnaba, maana yake “Mwenye kutia moyo.”
37
Mutu huyu aliuzisha shamba alilokuwa nalo, na kuleta feza alizopata kwa mikono ya mitume.
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 5 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28