bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 3
Acts 3
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 4 →
1
Siku moja, na saa tisa ya muchana, Petro na Yoane walienda katika hekalu kwa wakati wa maombi.
2
Karibu na mulango mumoja wa hekalu unaoitwa “Muzuri,” kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa kiwete tangia kuzaliwa kwake. Kila siku walimubeba na kumuweka kwenye mulango huo kusudi aombe musaada kwa watu waliokuwa wakiingia katika hekalu.
3
Yule kiwete alipowaona Petro na Yoane wakiingia ndani ya hekalu, akawaomba musaada.
4
Petro na Yoane wakamukazia macho, naye Petro akamwambia: “Utuangalie!”
5
Yule kiwete akawaangalia, akitumainia kupata kitu fulani toka kwao.
6
Lakini Petro akamwambia: “Sina mali yoyote, lakini nitakupa kile ninachokuwa nacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ninakuamuru simama utembee!”
7
Halafu Petro akamushika mukono wa kuume na kumusimamisha. Na pale pale miguu na vifundo vya miguu yake vikakaza kwa nguvu;
8
akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Kisha akaingia pamoja nao ndani ya hekalu akitembea, akirukaruka na kumusifu Mungu.
9
Watu wote waliokuwa mule walimwona akitembea na kumusifu Mungu.
10
Walipotambua kwamba yeye ndiye yule kiwete aliyekuwa akiikaa na kuombaomba musaada kwenye mulango wa hekalu unaoitwa “Muzuri,” wakashikwa na hofu na kushangaa sana na mambo yale yaliyomutokea.
11
Mutu huyo hakutaka kuachana na Petro na Yoane. Kwa hiyo watu wote wakashangaa sana na kukimbilia kwenye baraza la hekalu wanaloita La Solomono.
12
Petro alipoona maneno yale, akawaambia watu: “Wanainchi wenzangu Waisraeli, sababu gani munashangazwa na jambo hili? Sababu gani munatukazia macho? Munafikiri kwamba mutu huyu amepata kutembea kutokana na uwezo wetu sisi wenyewe au kwa haki yetu mbele ya Mungu?
13
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.
14
Yeye alikuwa Mutakatifu na Mwenye Haki, lakini mukamukana, mukataka Pilato awafungulie mwuaji.
15
Halafu mukamwua yule anayekuwa asili ya uzima, lakini Mungu amemufufua. Na sisi ni washuhuda wa jambo hilo.
16
Mutu huyu munayemujua na kumwona amepata tena nguvu kwa uwezo wa jina la Yesu, kwa njia ya kuaminia jina hili. Yeye amepona kabisa sawa vile ninyi wote munavyojionea, kwa njia ya kumwaminia Yesu.
17
“Sasa wandugu zangu, ninajua kwamba ninyi na wakubwa wenu mumemutendea Yesu hayo yote pasipo kujua nini munayofanya.
18
Lakini ni hivi Mungu alivyotimiza maneno aliyotangaza tangu zamani kwa kinywa cha manabii wote kwamba Masiya wake atateswa.
19
Basi mugeuke toka katika zambi, mumurudilie Mungu, kusudi awasamehe zambi zenu.
20
Hivi Bwana atawaletea nyakati za kutulizwa, naye atawatumia Masiya, ndiye Yesu, aliyechaguliwa tangu zamani kwa kuwaokoa.
21
Yeye anapaswa kubaki mbinguni mpaka zitakapotimia zile nyakati Mungu atakapotengeneza vitu vyote sawa vile alivyosema tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake watakatifu.
22
Kwa maana Musa alisema: ‘Bwana Mungu wenu atawatumia ninyi nabii anayekuwa sawa mimi, toka katika taifa lenu. Nanyi mutasikiliza mambo yote nabii yule atakayowaambia.
23
Na mutu yeyote atakayekataa kumusikiliza nabii yule, atatengwa mbali na taifa la Mungu na kuuawa.’
24
Na manabii waliosema tangia Samweli na wale waliomufuata, wote walitangaza mambo haya yanayotokea siku hizi.
25
Ahadi Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwenu. Vilevile agano Mungu alilofanya na babu zenu ni kwa ajili yenu, wakati alipomwambia Abrahamu: ‘Kwa njia ya wazao wako watu wote wa dunia watabarikiwa.’
26
Hivi Mungu alimutuma mutumishi wake kwa ajili yenu kwanza, kusudi awabariki ninyi, akimugeuza kila mumoja wenu toka katika njia zake mbaya.”
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 4 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28