bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 12
Acts 12
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 13 →
1
Katika siku zile mufalme Herode akaanza kutesa watu wamoja wa kanisa.
2
Akaamuru Yakobo, ndugu ya Yoane, auawe kwa upanga.
3
Basi, alipoona kwamba jambo lile liliwapendeza Wayuda, akaamuru Petro afungwe vilevile. (Mambo haya yalitokea kwa wakati wa sikukuu ya Mukate Usiotiwa Chachu.)
4
Alipokwisha kumukamata Petro, na kumutia katika kifungo, akamuweka chini ya ulinzi wa vikundi vine vya waaskari waliogomboana wane kwa wane. Naye alikusudia kumusambisha mbele ya watu nyuma ya sikukuu ya Pasaka.
5
Basi Petro akabaki akichungwa katika kifungo, lakini kanisa likaendelea kumwombea kwa Mungu pasipo kuchoka.
6
Usiku, mbele ya kutimia kwa siku Herode aliyotaka kumusambisha mbele ya watu, Petro alikuwa amelala ndani ya chumba katikati ya waaskari wawili. Alikuwa amefungwa na minyororo miwili, nao walinzi walikuwa wakichunga mulango wa kifungo.
7
Kwa rafla malaika wa Bwana akatokea na mwangaza ukajaa ndani ya chumba kile. Malaika akamutikisa Petro na kumwamusha, akimwambia: “Simama upesi!” Nayo minyororo ikaanguka toka kwenye mikono yake.
8
Kisha malaika akamwambia: “Funga mukaba na uvae viatu vyako.” Petro akafanya vile, naye malaika akamwambia tena: “Vaa koti yako na kunifuata.”
9
Petro akamufuata mpaka inje ya kifungo. Lakini hakutambua kwamba mambo yale malaika aliyofanya yalikuwa ya kweli; alizani kwamba amepata maono.
10
Wakapita kikundi cha kwanza cha waaskari na cha pili, na kufikia kwenye mulango wa chuma wa kuingilia ndani ya muji. Ule mulango ukajifungua wenyewe mbele yao, nao wakatoka inje na kuendelea katika barabara moja. Na kwa rafla yule malaika akamwacha.
11
Petro alipotambua kwamba mambo yaliyotokea ni ya kweli akasema: “Sasa ninajua hakika kwamba Bwana alimutuma malaika wake kuniokoa katika mikono ya Herode na katika mabaya yote Wayuda waliotaka kunitendea.”
12
Alipokwisha kufahamu mambo yale yaliyotokea, akaenda kwa Maria, mama ya Yoane aliyeitwa Marko. Watu wengi walikuwa wamekusanyika mule, wakiomba.
13
Petro alipiga hodi kwenye mulango wa inje, mujakazi mumoja aliyeitwa Roda akakuja kwenye mulango.
14
Naye akatambua sauti ya Petro akafurahi sana hata kwa pahali pa kufungua mulango akarudi mbio kuwapasha wengine kwamba Petro anasimama mbele ya mulango.
15
Nao wakamwambia: “Uko na wazimu!” Lakini akakaza kusema kwamba ni kweli. Basi wakasema: “Ni malaika wake.”
16
Kwa wakati ule Petro akaendelea tu kupiga hodi. Walipofungua mulango wakamwona, na kushangaa.
17
Naye akawanyamazisha kwa kunyoosha mukono, kuwaelezea namna Bwana alivyomwondoa katika kifungo. Akawaambia tena: “Muwaelezee Yakobo na wandugu wengine waamini habari hizi.” Kisha Petro akaondoka na kwenda nafasi ingine.
18
Kulipokucha, waaskari wakapigwa na hofu sana. Wakaanza kuulizana: “Jambo gani lililomupata Petro?”
19
Herode akaomba wamutafute, lakini hawakumwona. Kwa hiyo kisha kusambisha wale walinzi, akaamuru wauawe. Halafu Herode akaondoka Yudea kwenda katika muji Kaisaria na kukaa kule kwa muda.
20
Herode alikuwa amechunga hasira sana juu ya watu wa muji Tiro na wa Sidona. Lakini wakapatana kwa nia moja kwa kumwendea. Kwanza wakasikilizana na Balasto, aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya mufalme. Kisha wakaomba mapatano ya amani kwa mufalme Herode, kwa sababu inchi yao ilitegemea inchi ya mufalme huyo kwa kupata chakula.
21
Halafu kwa siku ile iliyopangwa, Herode akavaa nguo zake za kifalme, akaikaa katika kiti chake cha kifalme na kuwatolea watu hotuba.
22
Nao watu wakalalamika wakisema: “Hii ni sauti ya Mungu, wala si ya mutu.”
23
Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.
24
Lakini Neno la Mungu likaendelea mbele na kuenea fasi nyingi.
25
Barnaba na Saulo walipomaliza kazi yao, wakarudi toka Yerusalema, wakiwa pamoja na Yoane, aliyeitwa vilevile Marko.
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 13 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28