bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 6
Acts 6
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 7 →
1
Katika siku zile, kufuatana na jinsi hesabu ya wanafunzi wa Yesu ilivyokuwa ikizidi kuongezeka, kulitokea manunguniko kati ya Wayuda waliosema Kigriki na Wayuda waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigriki walinungunika kwa sababu wajane wao walisahauliwa wakati wa kugawanya vifaa vya kila siku.
2
Kwa hiyo wale mitume kumi na wawili wakafanya mukutano wa kundi lote la wanafunzi, na kuwaambia: “Haifai sisi tuache kuhubiri Neno la Mungu kwa ajili ya kushugulika na kazi ya kugawanya vyakula.
3
Hivi wandugu, muwachague wanaume saba kati yenu wenye ushuhuda muzuri, wenye kujazwa na Roho Mutakatifu na wenye hekima, kusudi tuwaweke kwa kazi hii.
4
Na sisi kwa ngambo yetu tutajitolea kwa kuomba Mungu na kuhubiri neno lake.”
5
Kundi lote likapendezwa na shauri hilo. Nao wakawachagua watu hawa: Stefano, mutu mwenye imani sana na aliyejazwa na Roho Mutakatifu, Filipo, Porokoro, Nikanora, Timoni, Permena na Nikolao, mutu wa Antiokia aliyekuwa amegeuka zamani kufuata dini ya Kiyuda.
6
Kisha wakawaweka mbele ya mitume, nao wakaomba na kuweka mikono juu yao.
7
Basi Neno la Mungu likazidi kuenea katika Yerusalema na hesabu ya wanafunzi ikaongezeka sana kule na makuhani wengi wakaamini.
8
Stefano alijaliwa sana na neema ya Mungu na alikuwa na uwezo mwingi, naye alifanya maajabu na vitambulisho vikubwa katikati ya watu.
9
Lakini kukatokea watu wamoja waliopingana na Stefano. Watu hawa walikuwa wa nyumba ya kuabudia iliyojulikana kwa jina la “Wenye Uhuru.” Nao walitoka katika inchi ya Kurene na ya Alesanduria, na kutoka jimbo la Kilikia na la Azia. Watu hawa wakaanza kubishana na Stefano
10
lakini hawakuweza kumushinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya Roho Mutakatifu aliyemwongoza kusema.
11
Halafu wakawashawishi watu wamoja kusudi waseme kwamba wamemusikia Stefano akisema maneno ya kumutukana Musa na Mungu.
12
Basi wakawachochea watu, wazee, na walimu wa Sheria. Nao wakamufikia Stefano, wakamukamata na kumupeleka mbele ya Baraza Kubwa.
13
Kisha wakaleta washuhuda wa uongo waliosema: “Mutu huyu hachoki na kusema maneno ya kutukana hili hekalu letu takatifu pamoja na Sheria ya Musa!
14
Kwa maana tumemusikia akisema kwamba huyu Yesu wa Nazareti ataharibu hekalu hili na kugeuza desturi tulizopokea toka kwa Musa.”
15
Na wote waliohuzuria katika lile Baraza wakamukazia Stefano macho, wakaona uso wake unafanana sawa na uso wa malaika.
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 7 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28