bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 17
Acts 17
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 18 →
1
Wakaendelea na safari yao, wakapita katika muji wa Amfipoli na wa Apolonia, na wakafika Tesalonika. Kule kulikuwa nyumba ya kuabudia ya Wayuda.
2
Na sawa ilivyokuwa desturi, Paulo akaingia katika nyumba ile. Kwa muda wa siku tatu za Sabato zilizofuatana juma kwa juma, akabishana na watu waliokuwa mule, akitumia Maandiko Matakatifu.
3
Aliwaelezea na kuwaonyesha wazi kwamba Kristo alipaswa kuteswa na kufufuka. Akawaambia: “Huyu Yesu ninayemuhubiri kwenu ndiye Kristo.”
4
Wamoja kati ya Wayuda wakasadiki na kujiunga pamoja na Paulo na Sila. Vilevile kundi kubwa la Wagriki walioogopa Mungu pamoja na wanawake wengi wenye heshima wakasadiki.
5
Lakini Wayuda wakajaa na wivu, hata wakakusanya watu wamoja wa ovyo ovyo waliowakuta kwenye nafasi za makutano, na kufanya kikundi. Kisha wakafanya fujo katika muji wote. Wakashambulia nyumba ya Yasoni, wakiwatafuta Paulo na Sila kusudi wawapeleke mbele ya watu.
6
Kwa kuwa hawakuwapata, wakamupeleka Yasoni pamoja na wandugu waamini wengine mbele ya wakubwa wa muji. Wakalalamika wakisema: “Watu hawa walifanya fujo fasi zote na sasa wamefika huku.
7
Naye Yasoni amewakaribisha kwake! Hawa wote wanatembea kinyume cha amri za Mufalme wa Roma wakisema kwamba kuna mufalme mwingine anayeitwa Yesu.”
8
Maneno haya yakafazahisha kundi la watu pamoja na wakubwa wa muji.
9
Wakubwa wa muji walipokwisha kumulipisha Yasoni na wenzake feza, wakawaachilia kwenda.
10
Mara moja ilipokuwa usiku, wanafunzi wakawasindikiza Paulo na Sila waende Beroya. Nao walipofika kule, pale pale wakaingia katika nyumba ya kuabudia ya Wayuda.
11
Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.
12
Basi Wayuda wengi kati yao wakaamini pamoja na wanawake wengi Wagriki wenye heshima, na hesabu yenye kutosha ya wanaume vilevile.
13
Lakini Wayuda wa muji wa Tesalonika wakapata habari kwamba Paulo anahubiri Neno la Mungu vilevile katika muji Beroya. Kwa hiyo wakaenda kule, wakaanza kufanya fujo kati ya makundi ya watu na kuwachochea.
14
Halafu pale pale, wandugu waamini wakamusindikiza Paulo mpaka kwenye kivuko, lakini Sila na Timoteo wakabaki Beroya.
15
Nao wale waliomwongoza Paulo wakamufikisha mpaka katika muji wa Atene. Kisha wakarudi Beroya wakiwa wameagizwa na Paulo kwamba wawaambie Timoteo na Sila wamufuate upesi.
16
Paulo alipokuwa akingojea Sila na Timoteo kule Atene, moyo wake ukavunjika sana kuona namna muji ule ulivyojaa sanamu za miungu.
17
Alikuwa akibishana na Wayuda katika nyumba ya kuabudia pamoja na watu wa mataifa mengine walioogopa Mungu. Vilevile alibishana kila siku na watu aliowakuta kwenye nafasi ya makutano.
18
Walimu wamoja wa kikundi cha Waepikurio na cha Wastoiko, wakaanza kubishana na Paulo. Wamoja wao wakauliza: “Huyu katetea anataka kusema nini?” Wengine wakasema: “Anaonekana kuwa muhubiri wa miungu ya kigeni.” Walisema hivi kwa sababu Paulo alikuwa akihubiri juu ya Yesu na jinsi alivyofufuka.
19
Halafu wakamukamata Paulo, na kumupeleka mbele ya Baraza Kubwa inayoitwa “Areopago,” wakamwuliza: “Unaweza kutujulisha maana ya mafundisho haya mapya unayotoa?
20
Kwa maana unatuelezea mambo ya kigeni. Basi tunataka kujua maana yake.”
21
(Haya yote ni kwa kuwa wazaliwa wa Atene pamoja na wageni walioishi kati yao, wanapitisha wakati wao wote kwa kueleza na kusikiliza habari mupya mupya.)
22
Halafu Paulo akasimama mbele ya Areopago na kusema: “Ninyi wakaaji wa Atene, ninaona kwamba ninyi ni watu munaopenda sana mambo yote ya dini.
23
Kwa maana nilipokuwa nikipitapita katika muji wenu nilichunguza nafasi zenu za kuabudia, nikaona hata mazabahu mamoja ambako waliyochora maandiko haya: ‘Kwa ajili ya mungu asiyejulikana.’ Basi yule munayemwabudu pasipo kumujua ndiye mimi ninayemuhubiri kwenu sasa.
24
Mungu aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, yeye anayekuwa Bwana wa mbingu na dunia, hakai ndani ya hekalu zilizojengwa na watu.
25
Yeye hahitaji kushugulikiwa na watu, kama vile angekuwa na lazima ya musaada fulani. Kwa maana yeye ndiye anayewapa watu wote pumzi ya uzima, pamoja na vitu vyote wanavyohitaji.
26
Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.
27
Mungu alitaka watafute kumujua, na kama ikiwezekana wamutambue hata ikiwa kama kwa njia ya kupapasa. Na kweli yeye hayuko mbali na kila mumoja wetu,
28
maana ‘kwa uwezo wake tunaishi, tunatenda na kuendelea kuwa.’ Ni sawa na maneno ya watunga mashairi wamoja wa kwenu waliosema: ‘Sisi vilevile tuko watoto wake.’
29
Basi kwa kuwa sisi tuko watoto wa Mungu, tusiwaze kwamba anafanana na sanamu ya zahabu au ya feza au ya jiwe, iliyochorwa kwa ufundi na akili ya watu.
30
Mungu hahesabu tena nyakati zile watu walipokuwa katika ujinga, lakini sasa anatangaza kwa watu wote, na nafasi zote kwamba wageuke toka zambi zao.
31
Kwa maana amekwisha kupanga siku atakapohukumu dunia kwa haki, kwa njia ya mutu mumoja, yule aliyemuweka kwa kazi ile. Naye amehakikisha mambo hayo kwa kumufufua mutu yule.”
32
Nao waliposikia Paulo akisema juu ya ufufuko, wamoja wakamuchekelea na wengine wakasema: “Tutakusikiliza tena ukisema juu ya habari hii siku ingine.”
33
Ni vile Paulo alivyoachana nao.
34
Ingawa vile watu wamoja walijiunga naye na kuamini. Kati yao kulikuwa Dionisio, mumoja wa Baraza Kubwa inayoitwa Areopago, pamoja na mwanamuke mumoja aliyeitwa Damari na watu wengine vilevile.
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 18 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28