bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 24
Acts 24
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 23
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 25 →
1
Kulipopita siku tano, Kuhani Mukubwa Anania akaenda Kaisaria pamoja na wasimamizi wamoja wa watu na mutetezi mumoja wa sheria aliyeitwa Tertulo. Nao wakafika mbele ya liwali Feliki kwa kumushitaki Paulo.
2
Walipomwita Paulo, Tertulo akaanza kumushitaki, akisema: “Muheshimiwa Feliki, kwa njia yako tumepata amani ya kweli. Na kwa uongozi wako umeleta mabadiliko mengi mazuri kwa ajili ya taifa hili.
3
Kwa yote hatutasahau mambo hayo yote kila wakati na kila fasi, nasi tunakushukuru sana.
4
Lakini, sababu sitaki kukupotezea wakati murefu, ninakusihi usikilize kwa wema wako maneno tutakayosema kwa kifupi.
5
Tumetambua kwamba mutu huyu ni wa hatari sana, ameanzisha fujo kati ya Wayuda wote katika dunia. Tena yeye ni mukubwa wa chama cha Wanazareti.
6
Naye alijaribu kuchafua hekalu, lakini tukamukamata. [Tulitaka kumuhukumu kufuatana na Sheria yetu,
7
lakini jemadari Lusia alijitokeza na kumwondoa kati yetu kwa kinguvu.
8
Kisha akaamuru kwamba wale wanaomushitaki wakuje kwako.] Na wewe mwenyewe utaweza kumusambisha mutu huyu, na kufahamu vizuri mambo yale tunayomushitakia.”
9
Wayuda wakamwunga mukono, wakisema kwamba maneno yale yote ni ya kweli.
10
Kisha liwali akamufanyia Paulo alama kwa kumuruhusu kusema, naye akasema: “Ninajua kwamba wewe umekuwa mwamuzi wa taifa hili tangia miaka mingi. Sababu hii sina wasiwasi kwa kujitetea mbele yako.
11
Kama unavyoweza kuhakikisha wewe mwenyewe, hakujapita zaidi ya siku kumi na mbili tangu nilipoenda Yerusalema kwa kumwabudu Mungu.
12
Watu hawa hawakunikuta ndani ya hekalu wala ndani ya nyumba za kuabudia, wala nafasi ingine katika muji nikibishana na mutu au nikisukuma watu kufanya fujo.
13
Nao hawawezi kuhakikisha maneno wanayonishitakia sasa.
14
Lakini ninakubali mbele yako kwamba ninamutumikia Mungu wa babu zetu nikifuata Njia ile wanayosema kwamba ni ya uongo. Mimi ninaamini maneno yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria na katika vitabu vya manabii.
15
Ninatumaini toka kwa Mungu sawa vile watu hawa wanavyotumaini, kwamba watu wema na wabaya wote watafufuliwa.
16
Kwa sababu hii ninajikaza siku zote kuishi maisha safi bila kuhukumiwa na zamiri yangu mbele ya Mungu na mbele ya watu.
17
“Nyuma ya kupitisha miaka mingi mbali na muji, nilirudi kule Yerusalema kuwaletea watu wa taifa langu musaada wa mali na kumutolea Mungu sadaka.
18
Na wakati ule nilipokuwa nikifanya mambo hayo, walinikuta katika hekalu, nami nilikuwa nimekwisha kufanya ibada ya kutakaswa. Sikukuwa na kundi la watu wala kuleta fujo.
19
Lakini Wayuda wamoja waliotoka katika jimbo la Azia walikuwa pale, na ni hao ndio wangepaswa kuja mbele yako kunishitaki ikiwa wako na neno lolote juu yangu.
20
Au watu hawa wanaokuwa hapa waseme kosa waliloniona nalo wakati niliposambishwa mbele ya Baraza Kubwa.
21
Neno moja tu nililosema kwa sauti nilipokuwa nikisimama ni hili: ‘Ninahukumiwa leo kwa sababu ninatumaini kama wafu watafufuliwa.’ ”
22
Halafu Feliki, aliyekuwa akifahamu vizuri mambo yanayoelekea Njia ya Bwana, akaamuru maneno yale yarudiliwe, akisema: “Nitakata maneno yenu wakati jemadari Lusia atakapokuja.”
23
Kisha akamwamuru yule mukubwa wa jeshi kwamba wamulinde Paulo katika kifungo wakimwachia uhuru kidogo, na wasiwazuize warafiki zake kumusaidia.
24
Nyuma ya siku chache, liwali Feliki akakuja pamoja na muke wake Drusila, aliyekuwa Muyuda. Akaamuru wamwite Paulo, naye akasikiliza maneno aliyosema juu ya kumwamini Kristo Yesu.
25
Lakini Paulo alipokuwa akihubiri juu ya haki, juu ya kujizuiza na juu ya siku ya hukumu ya Mungu itakayokuja, Feliki akaogopa na kumwambia: “Kwa sasa unaweza kujiendea. Nitakuita tena nitakapopata wakati.”
26
Vilevile alikuwa akitazamia kwamba Paulo atamupatia feza. Ni kwa sababu hii alimwita kila mara kwa kuzungumuza naye.
27
Kulipopita miaka miwili, Porkio Festo akamukomboa Feliki kama liwali. Na kwa sababu Feliki alitaka kujipendekeza kwa Wayuda, akamwacha Paulo katika kifungo.
← Chapter 23
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 25 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28