bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 10
Acts 10
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 9
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 11 →
1
Katika muji Kaisaria, kulikuwa mutu mumoja jina lake Kornelio. Yeye alikuwa mukubwa wa kundi la waaskari lililoitwa “Kundi la Italia.”
2
Yeye alikuwa mwenye kuogopa Mungu, naye alimwabudu Mungu pamoja na watu wote waliokuwa kwake. Aliwasaidia wamasikini wengi, naye alikuwa akimwomba Mungu siku zote.
3
Siku moja, ilipokuwa saa tisa ya muchana, akaona maono. Aliona waziwazi malaika wa Mungu akiingia kwake na kumwambia: “Kornelio!”
4
Kornelio akamukazia macho akiwa ameshikwa na woga, akamwuliza: “Bwana, ni nini?” Malaika akamujibu: “Mungu amesikia maombi yako na kupendezwa na misaada unayotoa kwa wamasikini, na kwa hiyo anakukumbuka.
5
Basi sasa; uwatume watu Yopa waende kumwita mutu mumoja jina lake Simoni anayeitwa vilevile Petro.
6
Anapanga kwa fundi mumoja wa kutengeneza vitu vya ngozi, anayeitwa Simoni. Nyumba yake iko pembeni ya bahari.”
7
Yule malaika aliyesema na Kornelio alipoondoka, akawaita watu wawili kati ya watumishi wake na askari mumoja mwenye kuogopa Mungu, aliyekuwa mumoja wa wasimamizi wake wa kipekee.
8
Na kisha kuwaelezea mambo yote yaliyotokea, akawatuma Yopa.
9
Kesho yake karibu na saa sita ya muchana, hao watu watatu wakafika karibu na Yopa, saa ile Petro akapanda juu ya paa kwa kuomba.
10
Naye akasikia njaa, na kuhitaji chakula. Walipokuwa wakimutengenezea chakula, akakuwa sawa amezimia.
11
Akaona katika maono mbingu imefunguliwa wazi, na kitu kimoja kinachokuwa kama nguo kubwa kikishuka, kikitelemushwa mpaka chini, kikishikwa kwenye pembe zake ine.
12
Na ndani yake kulikuwa kila namna ya nyama wenye miguu mine na wenye kutambaa pamoja na ndege.
13
Kisha akasikia sauti ikimwambia: “Petro, simama. Chinja na ukule!”
14
Lakini Petro akajibu: “Hapana, hata kidogo Ee Bwana! Mimi sijakula bado kitu chochote kisichoruhusiwa kukuliwa, wala chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu.”
15
Lakini ile sauti ikamurudilia, ikisema: “Vitu vilivyotakaswa na Mungu, usivihesabu kuwa vichafu.”
16
Nayo maneno haya yakasikilika tena mara tatu, kisha chombo kile kikanyanyuliwa mbinguni.
17
Petro alipokuwa angali na wasiwasi, naye akijiuliza juu ya maana ya maono yale, wale watu waliotumwa na Kornelio wakafika mbele ya mulango kwa maana walikuwa wamekwisha kujulishwa nafasi gani kunapokuwa nyumba ya Simoni.
18
Wakapiga hodi wakiuliza kama Simoni anayeitwa vilevile Petro anapanga pale.
19
Petro akiwa akifikiri juu ya maana ya yale maono, Roho Mutakatifu akamwambia: “Kuna watu watatu hapa wanaokutafuta.
20
Basi, simama ushuke na kwenda pamoja nao pasipo kusita, kwa maana ni mimi niliyewatuma.”
21
Halafu Petro akashuka na kuwaambia wale watu: “Ni mimi munayemutafuta. Mumekuja hapa kwa sababu gani?”
22
Nao wakamujibu: “Tumetumwa hapa na Kornelio, mukubwa wa waaskari. Yeye ni mutu wa haki na mwenye kumutii Mungu, naye anasifiwa na Wayuda wote. Malaika mutakatifu amemutokea na kumwagiza akuite ufike kwake kusudi asikie maneno utakayomwambia.”
23
Kisha Petro akawakaribisha ndani ya nyumba na kuwapangisha mule. Kesho yake Petro akafunga safari pamoja nao. Na wandugu waamini wamoja waliokaa Yopa wakamusindikiza.
24
Kesho kutwa wakafika katika muji Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwangojea pamoja na jamaa yake na warafiki zake aliowaalika.
25
Petro alipokuwa akiingia ndani ya nyumba, Kornelio akaenda kumupokea, akapiga magoti mbele yake na kumwabudu.
26
Lakini Petro akamwinua Kornelio na kumwambia: “Simama, kwa maana mimi ni mutu kama wewe.”
27
Petro akaingia ndani ya nyumba akiwa akisimulia na Kornelio, na mule akakuta watu wengi wamekusanyika.
28
Akawaambia: “Ninyi munajua wazi kama katika Sheria ya dini yetu inakatazwa kwa Muyuda kushirikiana na mutu wa taifa lingine wala kumutembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba haifai kumuhesabia mutu yeyote kuwa muchafu wala mutengwa.
29
Ni kwa sababu hii, wakati uliponitumia wajumbe, nilikuja pasipo kusita. Basi sasa ningependa kujua kwa sababu gani muliniita.”
30
Kornelio akajibu: “Kumekwisha kupita siku tatu, mimi nilikuwa nikiomba ndani ya nyumba yangu kwa saa hii hii ya saa tisa ya muchana. Mara moja nikaona mutu anayevaa nguo yenye kungaa sana, akisimama mbele yangu.
31
Naye akaniambia: ‘Kornelio, Mungu amesikia maombi yako na kukukumbuka kwa ajili ya misaada unayotoa kwa wamasikini.
32
Basi tuma watu waende Yopa kwa kumwita mutu mumoja jina lake Simoni anayeitwa vilevile Petro. Naye anapanga kwa fundi mumoja anayetengeneza vitu vya ngozi anayeitwa Simoni. Nyumba yake iko pembeni ya bahari.’
33
Na pale pale nikatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kwa kufika. Sasa sisi wote tuko hapa mbele ya Mungu kwa kusikiliza mambo yote Bwana aliyokuagiza kutuambia.”
34
Basi Petro akaanza kuhubiri, akisema: “Sasa ninafahamu kwamba Mungu hana upendeleo,
35
lakini katika kila taifa mutu yeyote anayemutii Mungu na kutenda yanayokuwa ya haki, anamupendeza.
36
Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.
37
Ninyi munajua mambo yaliyotokea katika Yudea yote, yakianzia katika jimbo la Galilaya nyuma ya mahubiri ya Yoane yaliyoelekea ubatizo.
38
Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.
39
Na sisi tuko washuhuda wa mambo yote Yesu aliyofanya katika inchi ya Wayuda na katika muji wa Yerusalema. Walimwua kwa kumutundika juu ya musalaba,
40
lakini Mungu akamufufua kwa siku ya tatu kisha kufa kwake na kumwonyesha waziwazi.
41
Hakuonekana kwa watu wote, lakini kwa sisi tuliochaguliwa na Mungu kuwa washuhuda. Ni sisi tuliokula na kunywa pamoja naye nyuma ya kufufuka kwake.
42
Akatuagiza kutangaza Habari Njema kwa watu na kushuhudia kwamba ni yeye aliyewekwa na Mungu kuwa Mwamuzi wa wazima na wafu.
43
Manabii wote wanamushuhudia Yesu kwamba kila mutu anayemwamini atasamehewa zambi zake kwa uwezo wa jina lake.”
44
Petro alipokuwa hajamaliza kusema maneno hayo, Roho Mutakatifu akashuka juu ya wote waliosikiliza mahubiri yake.
45
Na wale wanafunzi Wayuda waliofika pamoja na Petro wakashangaa sana kwa kuona kwamba Mungu ametoa zawadi ya Roho wake Mutakatifu kwa watu wa mataifa mengine vilevile.
46
Kwa maana waliwasikia wakisema kwa luga za ajabu na kumutukuza Mungu. Halafu Petro akasema:
47
“Ni nani anayeweza kuwazuiza watu hawa waliopewa Roho Mutakatifu kama sisi wasibatizwe kwa maji?”
48
Basi akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Na kisha wakamusihi Petro akae kule kwao kwa siku chache.
← Chapter 9
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 11 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28