bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 14
Acts 14
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 13
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 15 →
1
Paulo na Barnaba walipofika katika muji Ikonio, wakaingia vilevile katika nyumba ya kuabudia ya Wayuda. Mule wakahubiri hata kundi kubwa la Wayuda na mataifa mengine wakaamini.
2
Lakini Wayuda waliokataa kuamini walishawishi watu wa mataifa mengine na kuwasukuma kuwachukia wandugu waamini.
3
Paulo na Barnaba wakakaa Ikonio kwa muda murefu. Walisema kwa uhodari kabisa, wakimutumainia Bwana. Naye aliwapa uwezo wa kufanya maajabu na vitambulisho. Na kwa njia hiyo alihakikisha kwamba ujumbe walioutangaza juu ya neema yake ulikuwa wa kweli.
4
Watu wa muji wakatengana: wamoja walikuwa upande wa Wayuda na wengine upande wa mitume.
5
Kisha Wayuda wamoja na watu wa mataifa mengine pamoja na wakubwa wao, wakakusudia kuwatendea mitume vibaya na kuwaua kwa kuwatupia mawe.
6
Paulo na Barnaba walipotambua jambo lile wakakimbilia katika muji wa Listra na wa Derbe ndani ya wilaya ya Likaonia na katika sehemu za kandokando yake.
7
Kule wakaendelea kuhubiri Habari Njema.
8
Kule Listra kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa kiwete tangia kuzaliwa. Yeye hakuweza kusimama wala kupima kutembea.
9
Yeye alikuwa akisikiliza mahubiri ya Paulo. Paulo akamukazia macho, naye akaona kwamba kiwete yule yuko na imani ya kuweza kuponyeshwa.
10
Halafu akamwambia kwa sauti: “Simama wima!” Mutu yule akaruka akasimama na kuanza kutembea.
11
Wakati makundi ya watu walipoona jambo lile Paulo alilofanya, wakasema kwa sauti katika luga yao ya kilikaonia: “Miungu imetushukia ikiwa na sura ya kimutu!”
12
Walimupanga Barnaba jina la mungu Zeu, na Paulo jina la mungu Herme, kwa sababu yeye ndiye aliyetoa hotuba.
13
Naye kuhani wa hekalu la mungu Zeu, lililokuwa kwenye kiingilio cha muji, akaleta ngombe waliopambwa na mafungu za maua mbele ya mulango. Maana yeye pamoja na kundi la watu walitaka kuwatolea wale mitume sadaka ya nyama wenye kuchinjwa.
14
Lakini Barnaba na Paulo waliposikia habari ile, wakapasua nguo zao kwa huzuni, wakaingia haraka katikati ya kundi la watu, na kusema kwa sauti:
15
“Wandugu, kwa sababu gani munafanya mambo kama haya? Sisi vilevile ni watu, tuko sawasawa nanyi, na tunawahubiri ninyi Habari Njema kwamba muache kuabudu vitu hivi vya bure na mumugeukie Mungu mwenye uzima; yeye aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao.
16
Katika siku zilizopita Mungu aliwaachilia watu wa mataifa yote wafuate njia wanazotaka.
17
Ingawa vile hakuacha kujijulisha kwa njia ya kutenda mema. Anawanyeshea mvua toka mbingu, anawapa mavuno kwa wakati wake, anawapa chakula na kuwajaza na furaha.”
18
Ijapokuwa mitume walisema maneno haya, ilikuwa vigumu kuzuiza makundi ya watu wasiwatolee sadaka.
19
Kisha Wayuda wamoja wakakuja tokea katika muji wa Antiokia na wa Ikonio. Wakashawishi makundi ya watu wajiunge nao. Wakamutupia Paulo mawe na kumukokotea inje ya muji, wakizani kwamba amekwisha kufa.
20
Lakini wanafunzi walipokuwa wakimuzunguka, akasimama na kurudi ndani ya muji. Kesho yake yeye pamoja na Barnaba wakaenda katika muji wa Derbe.
21
Paulo na Barnaba walihubiri Habari Njema katika muji wa Derbe, na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi katika muji wa Listra, wa Ikonio na wa Antiokia ya Pisidia.
22
Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
23
Wakawachagua wazee katika kila kanisa. Na kisha kuomba na kufunga kula chakula, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana waliyemwamini.
24
Kisha wakapitia katika jimbo la Pisidia na kufika katika inchi ya Pamfilia.
25
Walipokwisha kuhubiri Neno la Mungu kwa watu wa muji Perga, wakaenda katika muji wa Atalia.
26
Na kutoka kule wakarudi mpaka Antiokia kwa njia ya chombo. Ni kule walipokuwa wameombewa neema kwa Mungu kwa ajili ya kazi ile waliyotoka kutimiza.
27
Walipofika Antiokia, wakafanya mukutano wa kanisa na kuwaelezea mambo yote Mungu aliyofanya kwa njia yao, na namna alivyowafungulia watu wa mataifa mengine mulango kusudi wao vilevile wapate kuamini.
28
Nao wakakaa kule Antiokia kwa muda wa siku nyingi pamoja na wanafunzi.
← Chapter 13
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 15 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28