bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 7
Acts 7
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 6
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 8 →
1
Halafu Kuhani Mukubwa akamwuliza Stefano: “Maneno haya wanayokushitakia ni ya kweli?”
2
Stefano akamujibu: “Wandugu zangu na wababa zangu, munisikilize! Mungu mwenye utukufu alimutokea babu yetu mukubwa Abrahamu wakati alipokuwa angali katika inchi ya Mesopotamia, mbele hajahamia katika muji Harani.
3
Mungu alimwambia: ‘Toka katika inchi yako na uache wandugu zako, uende katika inchi nitakayokuonyesha.’
4
Basi Abrahamu akatoka katika inchi ya Wababeli akaenda kukaa Harani. Kisha kufa kwa baba yake, Mungu akamuhamisha tena, akakuja kukaa katika inchi hii munayoishi ndani yake sasa.
5
Kule Mungu hakumupa Abrahamu hata sehemu ndogo ya shamba inayokuwa kama kikanyagio cha muguu kuwa urizi wake, lakini alimwahidi kwamba atamupa inchi hii kuwa urizi wake na wa wazao wake watakaoishi nyuma yake. Wakati ule, alikuwa hana mutoto.
6
Mungu alimwambia: ‘Wazao wako wataishi katika inchi ya kigeni, na kule watafanywa kuwa watumwa, nao watateswa kwa muda wa miaka mia ine.
7
Lakini mimi nitaazibu taifa lile litakalowafanya kuwa watumwa. Kisha nitawaondoa katika inchi ile, nao wataniabudu kwenye nafasi hii.’
8
Halafu Mungu akafanya agano na Abrahamu, na kitambulisho cha kuhakikisha kwamba limeshikwa kilikuwa kutahiriwa. Kwa hiyo Abrahamu akamutahiri mwana wake Isaka alipotimiza siku nane za kuzaliwa. Naye Isaka akamutahiri mwana wake Yakobo, na Yakobo akawatahiri wana wake kumi na wawili waliokuwa babu zetu wakubwa.
9
“Wale babu wakamwonea Yosefu wivu hata wakamwuzisha kuwa mutumwa katika inchi ya Misri. Lakini Mungu akamulinda,
10
akamwokoa toka katika taabu yote aliyopata. Mungu akamujalia neema, apate kupendwa na Mufalme wa Misri na kuonekana kuwa mwenye hekima mbele yake. Mufalme yule akamuweka kuwa musimamizi wa inchi yake na wa nyumba yake yote.
11
Halafu kukatokea njaa kubwa na mateso mengi katika inchi yote ya Misri na ya Kanana, nao babu zetu wakakuwa katika ukosefu wa chakula.
12
Yakobo alipopata habari kwamba kuna ngano katika Misri, akawatuma babu zetu kule mara ya kwanza.
13
Kwa safari ya pili, Yosefu akajitambulisha kwa wandugu zake, naye Mufalme wa Misri akapata kujua jamaa ya Yosefu.
14
Kisha Yosefu akatuma wajumbe kwenda kumwita baba yake Yakobo pamoja na jamaa yake yote wafike Misri. Nao wote kwa jumla walikuwa makumi saba na tano.
15
Halafu Yakobo akashuka kwenda Misri, naye akakaa kule pamoja na babu zetu.
16
Maiti zao zikapelekwa katika jimbo la Sekemu na kuzikwa katika kaburi lile Abrahamu alilonunua kwa feza kutoka kwa wazao wa Hemora.
17
“Siku za kutimiza ahadi Mungu aliyotoa kwa Abrahamu zilipokaribia, hesabu ya watu wa taifa letu kule Misri ikaongezeka hata ikazidika sana.
18
Halafu kukakuwa mufalme mwingine wa inchi ya Misri, asiyemujua Yosefu.
19
Mufalme huyo akatendea taifa letu kwa udanganyifu, akawatesa babu zetu hata akawalazimisha kuwatupilia watoto wao wachanga kusudi wakufe.
20
Na katika siku zile Musa akazaliwa, naye alikuwa mutoto muzuri sana. Alilelewa muda wa miezi mitatu katika nyumba ya baba yake.
21
Alipowekwa inje, binti ya Mufalme wa Misri akamutwaa na kumulea kama mutoto wake mwenyewe.
22
Musa akafundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri, akakuwa mwenye uwezo sana katika masemi yake na matendo yake.
23
“Wakati Musa alipokuwa na umri wa miaka makumi ine, akakusudia kwenda kuwatembelea wandugu zake Waisraeli.
24
Kule akamwona Mumisri mumoja akimutendea mumoja wa wale wandugu zake vibaya. Basi akamusaidia yule aliyeonewa; akalipiza kisasi kwa kumwua yule Mumisri.
25
Musa alizani kwamba wandugu zake wataelewa kwamba Mungu atawaokoa kwa njia yake, lakini hawakuelewa vile.
26
Kesho yake akawakutana Waisraeli wawili wakipigana, naye akajaribu kuwaamua, akiwaambia: ‘Warafiki, ninyi ni wandugu; kwa sababu gani munatendeana vibaya?’
27
Lakini yule aliyekuwa akimutendea mwenzake vibaya akamusukuma Musa pembeni akisema: ‘Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi wetu?
28
Unataka kuniua sawa vile ulivyomwua yule Mumisri jana?’
29
Kwa ajili ya maneno hayo akakimbia na kwenda kukaa katika inchi ya Midiani. Na kule akazaa wana wawili.
30
“Kulipopita miaka makumi ine, malaika wa Bwana akamutokea Musa katikati ya kichaka kilichokuwa kikiwaka moto katika jangwa karibu na mulima Sinai.
31
Musa alipoona jambo hilo akashangaa sana, naye aliposogea karibu kusudi aangalie, akasikia sauti ya Bwana ikisema:
32
‘Mimi ni Mungu wa babu zako, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.’ Musa akatetemeka kwa woga wala hakusubutu kuendelea kuangalia.
33
Halafu Bwana akamwambia: ‘Vua viatu vyako, kwa sababu hapa unaposimama ni pahali patakatifu.
34
Hakika nimeona namna watu wangu Waisraeli wanavyoteswa katika inchi ya Misri. Nimesikia kilio chao nami nimeshuka kwa kuwaokoa. Sasa kuja, nitakutuma kule Misri.’
35
“Huyu Musa ndiye yule Waisraeli waliyemukataa, wakisema: ‘Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi?’ Mungu alimutuma kuwa mukubwa na mukombozi wao, akisaidiwa na yule malaika aliyemutokea katikati ya kichaka kinachowaka moto.
36
Yeye ndiye aliyewaongoza Waisraeli toka Misri akifanya maajabu na vitambulisho katika inchi ile, na kwenye bahari Nyekundu na katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.
37
Ni yule yule Musa ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: ‘Mungu atawatumia ninyi nabii anayekuwa sawa mimi, toka katika taifa lenu.’
38
Na wakati ule kulipokuwa mukutano wa Waisraeli katika jangwa, yeye alikuwa pale pamoja na babu zetu na yule malaika aliyesema naye kwenye mulima Sinai. Na ni yeye aliyefunuliwa ujumbe wa Mungu unaoleta uzima na kuutangaza kwetu.
39
“Babu zetu hawakutaka kumusikiliza Musa, wakamukataa na kutamani kurudi Misri.
40
Wakamwambia Haruni: ‘Ututengenezee sanamu itakayotuongoza, kwa maana hatujui jambo gani lililomupata yule Musa aliyetuondoa Misri.’
41
Katika siku zile wakajitengenezea sanamu ya mwana-ngombe, wakaitambikia na kufurahia kitu hicho walichojifanyia wao wenyewe.
42
Basi Mungu akajitenga mbali nao, akawaacha waabudu nyota, jua na mwezi kufuatana na maneno haya yaliyoandikwa katika kitabu cha manabii: ‘Ninyi watu wa Israeli, si mimi muliyemuchinjia nyama na kumutolea sadaka zingine kwa muda wa ile miaka makumi ine katika jangwa.
43
Mulitembea mukibeba hema ya mungu wenu Moleki nayo sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Mulijitengenezea sanamu hizo kusudi muziabudu. Kwa hiyo nitawahamisha mbali kupita muji Babeli.’
44
“Kule katika jangwa babu zetu walikuwa na ile hema inayokuwa na vibao vya agano ndani yake. Hema ile ilikuwa imetengenezwa kama vile Mungu alivyomwagiza Musa, na mufano ule alioonyeshwa.
45
Kisha ile hema ikaachwa kwa kizazi cha babu zetu kilichofuata. Nao wakaibeba chini ya uongozi wa Yoshua mpaka waliponyanganya inchi ya mataifa yale Mungu aliyofukuza mbele ya kufika kwao. Nayo ikabaki katika inchi mpaka katika siku za Daudi.
46
Mungu akamujalia Daudi neema hata akamwomba yeye Mungu wa Yakobo ruhusa ya kumujengea nyumba.
47
Ingawa vile mwana wake Solomono ndiye aliyemujengea nyumba.
48
“Lakini Mungu Mukubwa hakai ndani ya nyumba zilizojengwa na watu kama vile inavyosemwa katika maandiko haya ya manabii:
49
‘Mbingu ni kiti changu cha kifalme, nayo dunia ni kiti changu cha kupumzishia miguu. Basi ni nyumba gani munayoweza kunijengea? Au ni nafasi gani munaweza kuniwekea makao?
50
Ni mimi peke yangu niliyeumba vitu hivi vyote!’
51
“Ninyi watu wagumu! Ninyi wenye roho ya kipagani na masikio yanayofungana! Siku zote munapingana na Roho Mutakatifu sawa vile babu zenu walivyofanya!
52
Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.
53
Mungu aliwatolea ninyi Sheria yake kwa njia ya wamalaika, lakini hamukuitii.”
54
Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.
55
Lakini Stefano akijazwa na Roho Mutakatifu, akakaza macho kuelekea mbingu akaona mwangaza wa utukufu wa Mungu naye Yesu akisimama na mamlaka karibu na Mungu.
56
Naye Stefano akasema: “Ninaona mbingu zimefunguliwa wazi, naye Mwana wa Mutu akisimama na mamlaka karibu na Mungu.”
57
Basi wale wajumbe wakafunga masikio yao, wakapiga kelele kwa nguvu na kumurukia wote pamoja.
58
Wakamukokota na kumupeleka mbali na muji na kuanza kumutupia mawe kusudi wamwue. Wale washuhuda wakavua nguo zao na kuziwekesha kijana mumoja Saulo.
59
Walipokuwa wakimutupia mawe, Stefano akaomba akisema: “Ee Bwana Yesu, pokea roho yangu.”
60
Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.
← Chapter 6
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 8 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28