bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 12
Ezekiel 12
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 13 →
1
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Wewe unakaa kati ya watu waasi. Wana macho lakini hawaoni; wana masikio lakini hawasikii.
3
Wao ni watu waasi. Basi, ewe mwanadamu, ufanye kama vile unakwenda katika uhamisho: ondoka muchana wakati wanapokuwa wakikuona, ukimbilie pahali pengine. Kwenda na muzigo wako kama mukimbizi kutoka pahali unapokuwa mpaka pahali pengine wao wakikuona. Labda wataelewa, ingawa wao ni waasi.
4
Utaondoka na muzigo wako kwa wakati wa muchana, waziwazi, mbele ya macho yao. Uondoke magaribi kama vile watu wanaokwenda katika uhamisho wanavyofanya.
5
Wakiwa wanakuangalia toboa ukuta wa nyumba, upitie hapo na kwenda inje.
6
Wakiwa wanakuona, ujibebeshe muzigo wako kwenye mabega na kuondoka wakati wa giza. Funika uso wako usiweze kuona unakwenda wapi. Ndivyo ninavyokufanya kuwa kitambulisho kwa Waisraeli.
7
Basi, nikafanya kama nilivyoamriwa. Siku hiyo, wakati wa muchana, nikafunga muzigo wangu kama muzigo wa mutu anayekimbia. Magaribi nikatoboa ukuta na giza lilipokuwa likiingia, nikatoka, nikibeba muzigo wangu juu ya mabega, watu wote wakiniona.
8
Kesho yake asubui, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
9
Wewe mwanadamu! Hao waasi Waisraeli hawajakuuliza maana ya kitendo ulichofanya?
10
Uwaambie: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Neno langu hili linaelekea mambo yatakayomupata mutawala wa Yerusalema na Waisraeli wote wanaoishi humo.
11
Uwaambie kwamba wewe ni kitambulisho kwao; kama ulivyofanya ndivyo itakavyotendeka kwao: watakwenda katika uhamisho; watakamatwa mateka.
12
Naye mutawala wao atabeba muzigo wake juu ya mabega wakati wa usiku, atatoka kupitia ukuta atakaotoboa apate kutoka; atafunika uso wake kusudi asiione inchi kwa macho yake.
13
Lakini nitatandaza wavu wangu juu yake, naye atanaswa katika mutego wangu. Nitamupeleka Babeli, inchi ya Wakaldea; naye akiwa huko atakufa bila kuiona inchi hiyo.
14
Wafuasi wake wote, washauri wake na waaskari wake wote, nitawasambaza inje kila upande. Nitauchomoa upanga na kuwafuatilia nyuma.
15
Nitakapowasambaza kati ya mataifa mengine na inchi za mbali, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
16
Lakini nitawaacha wachache waepuke vita, njaa na ugonjwa mukali; kusudi hao waweze kuwaelezea watu wa mataifa wanamoishi jinsi walivyotenda mabaya. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
17
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
18
Wewe mwanadamu, kula chakula na kunywa maji yako ukitetemeka kwa hofu.
19
Uwaambie watu wa inchi hii: Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya wakaaji wa Yerusalema ambao wangali bado katika inchi ya Waisraeli: Watakula chakula chao kwa hofu na kunywa maji yao kwa kufazaika, maana inchi yao haitakuwa na kitu, kwa sababu kila mukaaji ni mutesaji mukali.
20
Miji yenye watu itateketezwa, na inchi itakuwa ukiwa. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
21
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
22
Wewe mwanadamu: Kwa nini mezali hii inatajwa katika inchi ya Waisraeli: Siku zinakuja na kupita, lakini maono ya nabii hayatimii?
23
Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema kwamba nitakomesha mezali hiyo nao hawataitumia tena katika inchi ya Waisraeli. Uwaambie kwamba wakati umefika ambapo maono yote yatatimia.
24
Maana hakutakuwa tena maono ya uongo au uaguzi kati ya Waisraeli.
25
Mimi Yawe mwenyewe nitatangaza yatakayotukia. Nayo yatatukia bila kukawia. Wakati ninyi mungali munaishi, enyi watu waasi, neno nitakalosema nitalitimiza. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
26
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
27
Wewe mwanadamu, Waisraeli wanafikiri kwamba maono yako yanahusu siku za nyuma sana, na unabii wako unahusu nyakati za mbali sana!
28
Kwa hiyo uwaambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Maneno yangu yote yatatimia sasa hivi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 13 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48