bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 33
Ezekiel 33
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 32
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 34 →
1
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Ongea na wanainchi wenzako, uwaambie hivi: Kama nikileta vita katika inchi fulani, na watu wa inchi hiyo wakimuchagua mumoja wao akuwe mulinzi wao,
3
huyo anapoona waadui wanakuja, atapiga baragumu na kuwaonya watu.
4
Mutu akisikia sauti ya baragumu lakini akizarau onyo hilo, waadui wakikuja na kumwua, yeye mwenyewe atabeba lazima ya kifo chake.
5
Maana aliisikia sauti ya baragumu, akazarau onyo; basi lawama itakuwa juu yake mwenyewe. Lakini kama angejali hilo onyo, angeyaokoa maisha yake.
6
Lakini kama yule mulinzi akiona waadui wanakuja naye hapigi baragumu na watu wakikosa kuonywa juu ya hatari inayokuja, waadui wakikuja na kumwua mutu yeyote kati yao, huyo mutu aliyekufa, atakuwa amekufa kwa kosa lake. Lakini mimi nitamulaumu mulinzi kwa kifo cha mutu huyo.
7
Basi, ewe mwanadamu, nimekuweka kuwa mulinzi wa Waisraeli. Utakaposikia neno kutoka kwangu utawapa onyo langu.
8
Nikimwambia mutu mwovu hivi: Wewe mutu mwovu hakika utakufa; lakini wewe hausemi chochote kwa kumwonya aachane na mwenendo wake, yule mutu atakufa kwa kosa lake; lakini nitakulaumu wewe kwa kifo chake.
9
Lakini ukimwonya mwovu aachane na mwenendo wake, naye haachani na mwenendo wake mubaya, yeye atakufa kwa kosa lake; lakini wewe utakuwa umeyaokoa maisha yako.
10
Ewe mwanadamu! Uwaambie Waisraeli jambo hili: Ninyi munasema: Tumezidiwa na makosa na zambi zetu. Tunaregea kwa sababu yake! Tutaweza namna gani kuishi?
11
Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?
12
Basi, ewe mwanadamu, uwambie wanainchi wenzako hivi: Mutu wa haki akitenda uovu, haki yake haitamwokoa. Na mutu mwovu akiacha kutenda zambi, hataazibiwa. Mutu wa haki akianza kutenda zambi, haki yake haitamwokoa.
13
Mimi ninamwahidi mutu wa haki kwamba ataishi; lakini yeye akiamini kwamba haki yake inatosha, akianza kutenda uovu, matendo yake yote mema ya zamani hayatakumbukwa; atakufa kwa uovu wake.
14
Tena, nikimwambia mutu mwovu kwamba hakika atakufa naye akiacha zambi yake, akianza kutenda mambo yanayokuwa ya haki na sawa, hatakufa.
15
Kama akirudisha rehani na kurudisha kitu alichoiba, akifuata masharti yanayoleta uzima bila kutenda uovu, mutu huyo hakika ataishi. Hatakufa.
16
Zambi zake zote alizotenda hapo mbele hazitakumbukwa; yeye ametenda mambo yanayokuwa ya haki na mema, kwa hiyo hakika ataishi.
17
Wanainchi wenzako wanasema: Kitu anachofanya Yawe si sawa! Lakini ni wao ndio hawafanyi kitu kinachokuwa sawa.
18
Mutu wa haki akiacha haki yake, akianza kutenda uovu, atakufa kwa sababu ya uovu wake.
19
Na mutu mwovu akiacha uovu wake, akianza kutenda mambo ya haki na mema ataishi kwa sababu ya matendo yake mema.
20
Lakini, ninyi munasema: Anachofanya Yawe si sawa! Enyi Waisraeli, mimi nitamuhukumu kila mumoja wenu kadiri ya matendo yake.
21
Siku ya tano ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi na mbili tangu tulipopelekwa katika uhamisho, mutu mumoja aliyetoroka kutoka Yerusalema alikuja kwangu, akasema: Muji Yerusalema umetekwa!
22
Wakati mutu huyo alipofika, ilikuwa asubui. Jana yake magaribi Yawe alikuwa amenijaza uwezo wake nami sikuwa bubu tena, nikaanza kusema.
23
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
24
Wewe mwanadamu! Wakaaji waliobaki katika miji iliyoharibiwa katika inchi ya Israeli wanasema: Abrahamu alikuwa peke yake, hata hivyo, alipata kurizi inchi hii. Lakini sisi ni wengi; ni wazi tumepewa inchi hii ikuwe yetu!
25
Basi, uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninyi munakula nyama yenye damu, munaziabudu sanamu za miungu yenu na kumwanga damu! Munazani kwamba mutapewa inchi hii ikuwe yenu?
26
Munategemea silaha zenu, munafanya mambo ya kuchukiza na kila mwanaume kati yenu analala na muke wa jirani yake! Munazani kwamba mutapewa inchi hii ikuwe yenu?
27
Uwaambie hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, hao wanaokaa katika miji hiyo inayokuwa mabomoko, wataagamia kwa upanga; anayekuwa katika vijiji nitamutoa akuliwe na nyama wakali; na wale wanaokuwa kwa milima na ndani ya mapango watakufa kwa ugonjwa mukali.
28
Nitaifanya inchi kuwa jangwa na tupu. Nitawaua mashujaa wake wenye kiburi. Milima ya inchi ya Israeli itakuwa jangwa na hakuna mutu atakayepita huko.
29
Kweli, nitakapoifanya hiyo inchi kuwa jangwa na tupu kwa sababu ya mambo yote ya kuchukiza waliyotenda, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
30
Yawe aliniambia: Wewe mwanadamu! Wanainchi wenzako wanasema juu yako, wameikaa juu ya kuta na kwenye milango ya nyumba zao na kuambiana: Tuende kusikiliza neno Yawe alilosema!
31
Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.
32
Kwao, wewe umekuwa tu kama mwimbaji wa kubembeleza mwenye sauti nzuri ikiandamana na muziki safi! Wanayasikia yale unayosema, lakini hawatii hata neno moja.
33
Lakini hayo unayosema yatakapotukia –nayo kweli yatatukia –basi, halafu watatambua kwamba nabii amekuwa kati yao.
← Chapter 32
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 34 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48