bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 18
Ezekiel 18
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 17
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 19 →
1
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Kwa nini munarudiliarudilia mezali hii katika inchi ya Waisraeli: Wababa wamekula matunda mabichi ya mizabibu, lakini ni meno ya watoto wao ndiyo yanaumizwa!
3
Kama vile ninavyoishi, mezali hii haitatumiwa tena katika Israeli. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
4
Mujue kwamba uzima wa kila mutu ni katika mikono yangu, ikiwa uzima wa muzazi na uzima wa mutoto. Yeyote anayetenda zambi, ndiye atakayekufa.
5
Kama mutu ni wa haki, ataishi. Mutu wa haki anatenda hivi: anafuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki, hakuli sadaka kwenye milima, haziangalii sanamu za miungu ya Waisraeli, hamuchafui muke wa jirani yake, halali na mwanamuke wakati wake wa ugonjwa wa mwezi, hamutendei mutu yeyote ubaya, anarudisha rehani, haibi, anawapatia wenye njaa chakula anawavalisha wale wanaokuwa uchi, anakopesha bila kudai faida wala kujipatia mazidio, anaepuka kutenda uovu, anaamua kwa haki kati ya mwenye kudai na mwenye kudaiwa, anafuata masharti yangu na kutii maagizo yangu kwa moyo. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
10
Lakini ikiwa mutu huyo ana mutoto ambaye anafanya mabaya baba yake asiyofanya, yule mutoto atakufa kama anafanya machukizo haya: ananyanganya, anaua, anakula sadaka kwenye milima, anamuchafua muke wa jirani yake, anawatendea wamasikini na wakosefu vibaya, anaiba, harudishi rehani, anaangalia sanamu za miungu na kufanya machukizo, anakopesha kwa kupata faida na kujitafutia mazidio. Hakika atakufa, na yeye mwenyewe atabeba lazima ya kifo chake.
14
Lakini kama mutu yule akiwa na mutoto ambaye ameona zambi ambazo baba yake alitenda, lakini yeye hatendi mabaya yale, hatakufa juu ya uovu wa baba yake. Ni mutoto anayetenda hivi: hakuli sadaka kwenye milima, haziangalii sanamu za miungu ya Waisraeli, hamuchafui muke wa jirani yake, hamutendei mutu yeyote ubaya, hakamati rehani, haibi, anawapatia wenye njaa chakula na kuwavalisha wale wanaokuwa uchi, anaepuka kutenda uovu, anakopesha bila kudai faida wala kujipatia mazidio, anatii maagizo yangu na kufuata masharti yangu.
18
Lakini baba yake, kwa sababu alilipisha bei isiyokuwa ya haki na kumwibia ndugu yake, wala hakuwatendea wandugu zake vizuri, hakika atakufa kwa sababu ya uovu wake.
19
Lakini munauliza: Kwa nini mutoto asiazibiwe kwa sababu ya zambi za baba yake? Mutoto akitenda mambo ya haki na ya ukweli, kama akiwa mwangalifu kushika masharti yangu yote, basi, huyo hakika ataishi.
20
Atakayetenda zambi huyo ndiye atakayekufa. Mutoto hatabeba uovu wa baba yake, wala baba hatabeba uovu wa mutoto wake. Uhaki wa mutu wa haki itamufalia yeye mwenyewe: na uovu wa mwovu ataubeba yeye mwenyewe.
21
Kama mutu mwovu akiachana na zambi zake zote alizotenda, kama akishika masharti yangu yote, na kutenda mambo ya haki na ya ukweli, huyo hakika ataishi, hatakufa.
22
Makosa yake yote aliyofanya hayatakumbukwa; kwa sababu ya haki yake ataishi.
23
Basi, ninafurahia kufa kwa mutu mwovu? Hapana! Mimi ninapendelea aachane na njia zake mbaya apate kuishi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
24
Lakini, mutu wa haki akiacha haki yake na kutenda uovu na kufanya machukizo yaleyale mutu mwovu anayofanya, basi, huyo ataishi? Hapana! Matendo yake yote mema aliyotenda hayatakumbukwa tena; atakufa kwa sababu ya uasi na zambi aliyotenda.
25
Lakini ninyi munasema: Matendo ya Yawe si sawa! Musikilize sasa, enyi Waisraeli: Ninachofanya mimi si sawa? Munachofanya ninyi ndicho kisichokuwa sawa.
26
Mutu wa haki akiacha haki yake na kutenda uovu atakufa kwa ajili hiyo; atakufa kwa sababu ya uovu aliotenda.
27
Lakini mutu mwovu akiachana na uovu aliofanya, na kutenda mambo ya haki na ya ukweli, huyo atayaokoa maisha yake.
28
Kwa sababu amefikiri, akaachana na makosa aliyoyafanya, hakika ataishi; hatakufa.
29
Lakini ninyi Waisraeli munasema: Anachotenda Yawe si sawa! Enyi Waisraeli, basi, ninachofanya mimi si sawa? Munachofanya ninyi ndicho kisichokuwa sawa.
30
Kwa hiyo, nitawahukumu ninyi Waisraeli, kila mumoja wenu, kulingana na mwenendo wake. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Mugeuke na kuachana na makosa yenu yasipate kuwaangamiza.
31
Mutupilie mbali zambi mulizonitendea; mujipatie moyo na roho mupya. Enyi Waisraeli, mutakufa kwa sababu gani?
32
Sifurahii kifo cha mutu yeyote. Hivyo mugeuke kusudi mupate kuishi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
← Chapter 17
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 19 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48