bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 26
Ezekiel 26
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 27 →
1
Katika siku ya kwanza ya mwezi, mwaka wa kumi na mumoja tangia kuhamishwa kwetu, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!
3
Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitapingana nawe ewe Tiro. Nitasukuma mataifa mengi juu yako, nao watakuja kama mawimbi ya bahari.
4
Wataziharibu kuta zako na kuibomoa minara yako. Nitafagia kabisa udongo wako na kukufanya kuwa kama jiwe tupu.
5
Utakuwa pahali penye kukauka katikati ya bahari, na wavuvi watakaushia nyavu zao hapo. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Mataifa yatakukamata mateka,
6
na miji inayokuwa jirani yako huko katika vijiji itaangamizwa. Nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.
7
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kutoka upande wa kaskazini nitamuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mufalme wa wafalme, akiwa na farasi, magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa, akuje kukushambulia.
8
Ataiangamiza miji inayokuwa jirani yako huko katika vijiji. Kisha atajenga kuta za kukushambulia, atajaza udongo kwenye kuta zako na kuweka ukuta wenye ngao kwa kukushambulia.
9
Ataweka vifaa vyake vya kubomoa mbele ya kuta zako, na kwa nyundo ataivunjavunja minara yako.
10
Farasi wa mufalme Nebukadneza ni wengi na mavumbi watakayorusha juu yatakufunika. Kuta zako zitatetemeka kwa mushindo wa waaskari wapanda-farasi na magari ya vita na ya mizigo wakati atakapoingia kwenye milango yako kama watu wanavyoingia katika muji kupitia pahali palipobomolewa.
11
Kwa kwato za farasi wake, atakanyagakanyaga barabara zako zote. Atawaua watu wako kwa upanga; minara yako mikubwa ataiangusha chini.
12
Ataunyanganya utajiri wako pamoja na biashara yako. Atazibomoa kuta zako na kuziangusha nyumba zako nzuri; mawe, mbao na udongo ulivyotumia kwa kujenga nyumba hizo watavitupa katika bahari.
13
Nitakomesha muziki wa nyimbo zako. Sauti za vinubi vyako hazitasikilika tena.
14
Nitakufanya kuwa kama jiwe; utakuwa pahali pa wavuvi pa kukaushia nyavu zao, wala hautajengwa tena. Mimi Yawe nimesema. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
15
Bwana wetu Yawe anasema hivi kwa Tiro: Wakaaji wa sehemu za kandokando ya bahari watatetemeka watakaposikia kishindo cha kuanguka kwako na mulio wa maumivu na wa watu wanaouawa.
16
Wakubwa wote wa mataifa ya kandokando ya bahari watashuka toka kwenye viti vyao vya kifalme, na kuvua nguo zao za heshima pamoja na nguo zao zilizopindwa. Kisha kujaa hofu, wataikaa chini; nao watatetemeka wakati wote na kushangaa sana juu ya hayo yaliyokupata.
17
Watakuimbia wimbo huu wa kuomboleza: Namna gani wewe muji wenye utukufu, umetoweka kutoka katika bahari! Ulikuwa na nguvu juu ya bahari, wewe pamoja na wakaaji wako, wewe uliyeletea woga juu ya wote!
18
Sasa watu wa visanga wanatetemeka kwa sababu ya kuanguka kwako; watu wa visanga katika bahari wanatishwa kwa kuanguka kwako!
19
Maana, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakufanya wewe Tiro kuwa matongo, kama miji isiyokuwa na watu, nitakapoleta juu yako maji kutoka vilindi vya bahari, na maji mengi yatakufunika.
20
Nitakuteremusha ndani ya shimo kusudi ujiunge na wale wanaokuwa huko, walioishi zamani katika dunia; utakaa kule katika matongo kwa milele. Hautakaliwa na watu milele na hautakuwa na nafasi katika inchi za wanaokuwa wazima.
21
Nitakufanya kuwa kitu cha kuogopesha na itakuwa mwisho wako; watu watakutafuta, lakini hawatakupata tena. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 27 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48