bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 42
Ezekiel 42
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 41
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 43 →
1
Kisha yule mutu alinipeleka kwenye kiwanja cha inje mpaka kwenye jengo lililokuwa upande wa kaskazini, naye akaniingiza kwenye vyumba vinavyoelekea kiwanja cha hekalu na jengo lililokuwa upande wa kaskazini.
2
Jengo hili lililokuwa upande wa kaskazini lilikuwa na urefu wa metre makumi tano na upana wa metre makumi mbili na tano.
3
Kulikuwa gorofi tatu zilizounganisha metre kumi za kiwanja cha ndani na zikielekea sakafu ya kiwanja cha inje.
4
Upande wa kaskazini wa jengo hilo, kulikuwa njia ya kupitia yenye upana wa metre tano na urefu wake metre makumi tano. Milango yake ilikuwa upande wa kaskazini.
5
Vyumba katika hatua ya juu vilikuwa vyembamba kuliko vile vya katikati na vya chini maana vilikuwa mbali zaidi.
6
Vile vyumba vya juu kabisa vilijengwa kwenye miinuko na havikusaidiwa na nguzo kama majengo mengine kwenye kiwanja cha inje.
7
Kulikuwa ukuta mbele ya vyumba kuelekea kiwanja cha inje ukiwa na urefu wa metre makumi mbili na tano.
8
Wakati vile vyumba kwenye kiwanja cha inje vikiwa na urefu wa metre makumi mbili, vile vinavyoelekea hekalu vilikuwa na urefu wa metre makumi tano.
9
Chini ya vyumba hivi kulikuwa njia ya kupitia tokea upande wa mashariki kwa mwisho wa jengo, ikiwa mutu anaingia tokea kiwanja cha inje
10
ambako ukuta wa inje unaanzia. Kwenye upande wa kusini kulikuwa jengo lingine sawa na lile lingine, si mbali na jengo la upande wa magaribi kwa mwisho wa hekalu.
11
Mbele ya vyumba hivyo kulikuwa njia ya kupitia kama ile ya upande wa kaskazini. Jengo hilo lilikuwa na vipimo vilevile kama vya lile lingine, maingilio, magawanyo na milango ilifanana na ile ingine.
12
Kulikuwa mulango chini ya vyumba kwenye upande wa kusini wa jengo, kwa mwisho wa upande wa mashariki ambako ukuta ulianzia.
13
Yule mutu akaniambia: Vyumba hivi vyote ni vitakatifu. Ndani ya vyumba hivi makuhani wanaoingia mbele ya Yawe, wanakula sadaka takatifu kabisa: sadaka takatifu kabisa na humo ndimo munamowekwa sadaka za vyakula, sadaka za kuomba kusamehewa zambi na sadaka kwa ajili ya malipo ya kosa kwa sababu pahali hapo ni patakatifu.
14
Makuhani ambao watakuwa wakitumika katika Pahali Patakatifu, wanapotaka kwenda kwenye kiwanja cha inje, ni lazima waache humo nguo zao walizovaa walipokuwa wanatumika mbele ya Yawe kwa sababu nguo hizo ni takatifu. Ni lazima wavae nguo zingine mbele ya kutoka inje ambako watu wanakusanyika.
15
Mutu yule alipokwisha kupima eneo la ndani la nyumba ya Yawe, alinitoa inje kupitia mulango wa mashariki na kulipima eneo la inje.
16
Alitwaa ule ufito wake wa kupima na kuupima upande wa mashariki, nao ulikuwa metre mia mbili makumi tano.
17
Akaupima upande wa kaskazini kwa kutumia ufito wake, nao ulikuwa metre mia mbili makumi tano.
18
Kisha akaupima upande wa kusini kwa kutumia ufito wake, nao ulikuwa metre mia mbili makumi tano.
19
Kisha akageuka na kupima upande wa magaribi kwa kutumia ufito wake, nao ulikuwa metre mia mbili makumi tano.
20
Hivyo akakuwa amepima pande zote, nazo zilikuwa metre mia mbili makumi tano kila upande. Ukuta huo ulitenganisha kati ya eneo takatifu na lile la kawaida.
← Chapter 41
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 43 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48