bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 17
Ezekiel 17
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 18 →
1
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Tega kitendawili, uwaambie Waisraeli fumbo.
3
Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kulikuwa tai mumoja mukubwa sana aliyekuwa na mabawa makubwa, yenye manyoya marefu mengi yenye rangi za kila aina. Tai yule aliruka mpaka kwenye mulima Lebanoni, akatua juu ya kilele cha muti wa mwerezi;
4
akavunja tawi lake la juu zaidi, akalipeleka katika inchi ya wachuuzi, akaliweka katika muji wao mumoja.
5
Kisha akatwaa kichipukizi cha mumea katika inchi ya Waisraeli, akaupanda katika udongo wenye mboleo ambako kulikuwa maji mengi.
6
Mumea ukakomaa na kuwa muzabibu wa aina ya muti unaotambaa; matawi yake yakaelekea yule tai, na mizizi yake ikaingia chini ndani ya udongo. Muzabibu ukatoa matawi na majani mengi.
7
Lakini kulikuwa tai mwingine mukubwa; alikuwa na mabawa makubwa ya manyoya mengi. Basi, ule muzabibu ulikunja mizizi yake, ukamwelekezea matawi yake, kusudi aumwangilie maji.
8
Muzabibu ulikuwa umepandikizwa penye udongo muzuri na karibu na maji mengi, kusudi upate kutoa matawi na kuzaa matunda uweze kuwa muzabibu muzuri sana!
9
Sasa Bwana wenu Yawe anakuuliza: Muzabibu huo utaweza kustawi? Hawataongoa mizizi yake na kuozesha matunda yake na matawi yake machanga kuyanyausha? Hakutahitajika mutu mwenye nguvu au kundi kubwa kuuongoa kutoka ndani ya udongo.
10
Umepandikizwa, lakini, utastawi? Upepo mukali wa mashariki unapovuma juu yake utanyauka; utakaukia palepale kwenye udongo ulikoota.
11
Kisha neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
12
Sasa uwaulize wale watu waasi kama wanaelewa maana ya mufano huo. Uwaambie kwamba, mufalme wa Babeli alikuja Yerusalema, akamwondoa mufalme na wakubwa wake, akawapeleka Babeli.
13
Kisha akachagua mutu mumoja wa jamaa ya kifalme, akafanya naye mapatano, akamwapisha kiapo cha uaminifu. Aliwaondoa wakubwa wengine katika inchi akawapeleka mbali
14
kusudi utawala huo ukuwe zaifu na ushike agano la mufalme wa Babeli.
15
Lakini yule mufalme mupya alimwasi mufalme wa Babeli kwa kuwatuma wajumbe Misri kuomba farasi na waaskari wengi. Mufalme huyo atashinda? Anayefanya hivyo na kuvunja agano lake ataweza kuepuka azabu?
16
Kama vile ninavyoishi, mufalme huyu atakufia katika inchi ya Babeli, inchi ya mufalme yule aliyemuweka kuwa mufalme, na ambaye amezarau kile kiapo na kuvunja lile agano alilofanya naye.
17
Hakika, Mufalme wa Misri pamoja na jeshi lake kubwa hataweza kumusaidia katika vita wakati Wababeli watakapomuzungushia kikingio na kuta kusudi wapate kuwaua watu wengi.
18
Kwa sababu alikizarau kile kiapo na kuvunja lile agano ambalo aliahidi kwa mukono wake mwenyewe na kufanya mambo yale yote, hakika hataokoka.
19
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, nitamwazibu vikali kwa sababu amekizarau kiapo alichoapa kwa jina langu na kuvunja agano langu.
20
Nitatandaza wavu wangu juu yake, naye atanaswa katika mutego wangu; nitamupeleka mpaka Babeli na kumuhukumu kwa sababu ya udanganyifu alioufanya juu yangu.
21
Waaskari wake hodari watauawa kwa upanga na wale watakaoponyoka watatawanyika pande zote. Kwa hiyo mutatambua kwamba ni mimi, kweli ni mimi Yawe ninayesema hivyo.
22
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitatwaa kichipukizi cha incha ya juu ya muti wa mwerezi. Nitavunja tawi changa kutoka matawi yake ya juu na kulipanda juu ya mulima murefu sana.
23
Kweli, nitalipanda juu ya mulima murefu wa inchi ya Waisraeli kusudi lichanue na kuzaa matunda. Litakuwa mwerezi muzuri, na ndege wa aina zote watakaa chini yake vilevile watajenga chicha zao katika matawi yake.
24
Halafu miti yote katika inchi itajua kwamba mimi Yawe ninaishusha miti mirefu na kuinua miti mifupi. Mimi ninakausha miti mibichi na kustawisha miti yenye kukauka. Ni mimi Yawe ninayesema hayo na nitayafanya.
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 18 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48