bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 29
Ezekiel 29
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 28
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 30 →
1
Siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Ugeuke kuelekea mufalme wa Misri, utoe unabii juu yake na juu ya inchi yote ya Misri.
3
Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri, wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili! Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako, kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!
4
Basi, nitakutia ndoana katika mataya yako, na kuamuru samaki wakwame katika magamba yako. Nitakuvua kutoka huko ndani ya muto.
5
Nitakutupa katika jangwa, wewe na samaki hao wote. Mwili wako utaangukia katika mbuga; wala hakuna atakayekuokota kusudi akuzike. Nimeutoa mwili wako ukuwe chakula cha nyama wakali na ndege.
6
Halafu wakaaji wote wa Misri watatambua kwamba mimi ni Yawe. Waisraeli walikutegemea wewe ee Misri, lakini umekuwa zaifu kama utete.
7
Walipokushika kwa mukono, ulivunjika na kutegua mabega yao. Walipokuegemea ulivunjika na kutetemesha viungo vyao.
8
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaleta upanga juu yako na kuwaua watu na nyama wako wote.
9
Kwa sababu umesema kwamba muto Nili ni wako, kwamba ndiwe uliyeufanya, basi, inchi yako, Misri, itakuwa tupu na jangwa. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
10
Hakika nitakuazibu wewe na mito yako; kwa hiyo nitaifanya inchi ya Misri kuwa jangwa na tupu toka Migidoli mpaka Sewene hata kwenye mipaka ya Etiopia.
11
Hakuna mutu wala nyama atakayepita huko. Haitakaliwa kwa muda wa miaka makumi ine.
12
Kati ya miji yote iliyoharibika, miji ya Misri itakuwa mitupu kwa miaka makumi ine. Nitawasambaza Wamisri kati ya watu wa mataifa mengine na kuwaeneza katika inchi zingine.
13
Lakini Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kisha ile miaka makumi ine nitawakusanya Wamisri kutoka kwa mataifa walimosambazwa.
14
Nitawafanikisha tena Wamisri. Nitawarudisha katika inchi ya Patro, inchi yao ya asili. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu,
15
ufalme zaifu kuliko falme zote; wala hawataweza kujipandisha juu ya mataifa mengine. Nitawafanya Wamisri wakuwe watu zaifu hata wasiweze kuyatawala mataifa mengine tena.
16
Misri haitakuwa tena na nguvu za kuweza kutegemewa na Waisraeli. Waisraeli watakumbuka jinsi walivyokosa kwa kutegemea inchi ya Misri. Waisraeli watatambua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.
17
Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, mwaka wa makumi mbili na saba tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
18
Wewe mwanadamu! Nebukadneza, mufalme wa Babeli, aliwalazimisha waaskari wake kufanya kazi ngumu ya kuishambulia Tiro. Vichwa vyote vya waaskari wake vilipata upaa na mabega yote yalichubuka. Lakini yeye, wala waaskari wake, hawakupata chochote kutokana na kazi hiyo aliyoifanya juu ya Tiro.
19
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitamupa Nebukadneza mufalme wa Babeli, inchi ya Misri. Atanyanganya mali yake yote, na kutwaa utajiri wa Misri kuwa mushahara wa waaskari wake.
20
Nimemupa inchi ya Misri kuwa mushahara wa jasho lake kwa maana waaskari wake walifanya kazi kwa ajili yangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
21
Siku hiyo, nitawafanya Waisraeli wakuwe na nguvu na kukuwezesha wewe Ezekieli useme kati yao. Nao watapata kujua kwamba mimi ni Yawe.
← Chapter 28
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 30 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48