bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 32
Ezekiel 32
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 31
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 33 →
1
Siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na mbili, mwaka wa kumi na mbili tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa kuomboleza juu ya Mufalme wa Misri. Wewe Mufalme wa Misri unajiona kuwa simba kati ya mataifa, lakini wewe ni kama mamba tu katika maji: unachomoka kwa nguvu kwenye mito yako, unayavuruga maji kwa miguu yako, na kuichafua mito.
3
Bwana wetu Yawe anasema: Nitautupa wavu wangu juu yako, nao watu watakuvua humo kwa wavu wangu.
4
Nitakutupa juu ya inchi kavu, nitakutupa chini juu ya uwanja, nitaleta ndege wote watue juu yako, na kuwashibisha nyama wote wa pori kwa mwili wako.
5
Nitasambaza nyama yako juu ya milima, na kujaza mabonde yote muzoga wako.
6
Nitaikunywesha inchi damu yako mpaka juu ya milima, mashimo yatajaa damu yako.
7
Nitakapokuangamiza, nitazifunika mbingu, nitazifanya nyota kuwa nyeusi, jua nitalifunika kwa mawingu, na mwezi hautatoa mwangaza wake.
8
Nitaifanya miangaza yote mbinguni kuwa giza nitatandaza giza juu ya inchi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
9
Nitaihuzunisha mioyo ya watu wengi, nitakapokupeleka katika utumwa kati ya mataifa, katika inchi ambazo hauzijui.
10
Nitayashitusha mataifa mengi kwa habari zako, wafalme wao watatetemeka kwa sababu yako, nitakaponyoosha upanga wangu mbele yao. Watatetemeka kila wakati, kila mutu akiogopea maisha yake, siku ile ya kuangamia kwako.
11
Kwa maana, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Upanga wa mufalme wa Babeli utakufuatilia.
12
Watu wako wengi watauawa kwa mapanga ya mashujaa, watu wa hatari kuliko mataifa yote. Watakomesha kiburi cha Misri na kuwaua watu wako wote.
13
Nitawaangamiza nyama wako wote pembeni ya muto Nili. Maji yake hayatavurugwa tena na mutu wala kwato za nyama kuyachafua tena.
14
Hapo nitayafanya maji yake yatulie na kuitiririsha mito yake kama mafuta. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
15
Nitakapoifanya inchi ya Misri kuwa jangwa na mali yake yote kunyanganywa, nitakapowaua wakaaji wake wote, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
16
Huo ndio wimbo wa maombolezo, wanawake wa mataifa watauimba, wataimba juu ya Misri na watu wake wote. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
17
Siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, mwaka wa kumi na mbili tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
18
Wewe mwanadamu! Uwaombolezee watu wengi wa Misri. Uwapeleke chini kwenye inchi ya wafu pamoja na mataifa mengine yenye nguvu, waende huko pamoja na wanaoshuka chini kwa wafu.
19
Uwaambie: Ninyi ni wazuri kuliko nani? Muende kuzimu mulalishwe pamoja na wasiomujua Mungu!
20
Wamisri wataangamia pamoja na watu waliouawa katika vita. Upanga uko tayari kuangamiza Misri pamoja na watu wake wengi.
21
Wakubwa wenye nguvu pamoja na wasaidizi wao wakiwa huko katika shimo kwa wafu watasema hivi: Wamisri wameshuka chini kwa wafu, wanalala pamoja na watu wasiomujua Mungu, waliouawa katika vita.
22
Asuria iko huko. Makaburi ya waaskari wake yanaizunguka. Wote waliuawa katika vita.
23
Makaburi yao yako sehemu za chini kabisa katika shimo kwa wafu. Waaskari wao wanaizunguka. Wote waliuawa katika vita. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima.
24
Elamu nayo iko huko. Makaburi ya waaskari wake yanaizunguka. Wote waliuawa katika vita. Wakashuka kwenye inchi ya wafu, bila kujua Mungu. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima. Lakini sasa wanapata haya yao pamoja na wale wanaoshuka katika shimo kwa wafu.
25
Elamu imelalishwa kati ya wale waliouawa katika vita. Makaburi yao yanaizunguka. Wote waliuawa katika vita, bila kujua Mungu. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima, na sasa wako wanapata haya yao pamoja na wale wanaoshuka katika shimo kwa wafu. Wanawekwa kati ya wale waliouawa.
26
Mesaki na Tubali ziko huko. Makaburi ya watu wake wote yanazizunguka. Wote waliuawa katika vita, bila kujua Mungu. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima.
27
Hawakuzikwa pamoja na mashujaa wa zamani, ambao walikwenda katika kuzimu kwa wafu wakiwa na silaha zao, mapanga yao chini ya vichwa vyao na ngao zao juu ya miili yao. Mashujaa hao walipokuwa wangali wanaishi walijaza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima.
28
Basi, ninyi Wamisri mutaangamizwa na kulalishwa kati ya wasiomujua Mungu waliouawa katika vita.
29
Edomu iko huko pamoja na wafalme wake na wakubwa wao wote. Walipokuwa wangali wanaishi walikuwa na nguvu sana, lakini sasa wamelalishwa kwa wafu pamoja na wasiomujua Mungu waliouawa katika vita.
30
Wakubwa wote wa watu wa upande wa kaskazini wako huko vilevile; hata Wasidoni wote walikwenda kujiunga na wafu. Walipokuwa wangali wanaishi, walisababisha vitisho kwa nguvu zao, lakini sasa hao wasiomujua Mungu wamelalishwa chini na haya pamoja na wale waliouawa katika vita. Wanashiriki haya ya wale walioshuka ndani ya shimo kwa wafu.
31
Mufalme wa Misri, atakapowaona hao wote atafarijika kwa ajili ya wingi wa majeshi yake yote.
32
Nilimuwezesha mufalme wa Misri aeneze vitisho katika inchi ya wanaokuwa wazima, lakini sasa yeye mwenyewe pamoja na jeshi lake lote watauawa katika vita na kulalishwa pamoja na wasiomujua Mungu, waliokufa katika vita. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
← Chapter 31
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 33 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48