bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 41
Ezekiel 41
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 40
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 42 →
1
Kisha, yule mutu akanipeleka kwenye baraza la ndani, Pahali Patakatifu. Akaipima nafasi iliyoelekea humo ndani, nayo ilikuwa na urefu wa metre tatu,
2
na upana wa metre tano. Nafasi hiyo ilikuwa na kuta kila upande zenye unene wa metre mbili na nusu. Akapima baraza lenyewe, nalo lilikuwa na urefu wa metre makumi mbili na upana metre kumi.
3
Kisha akaenda kwenye chumba cha ndani kabisa. Akaipima nafasi iliyoelekea huko, nayo ilikuwa na kimo cha metre moja na upana metre tatu na nusu. Nafasi hiyo ilikuwa na kuta kila upande zenye unene wa metre tatu na nusu.
4
Akakipima chumba chenyewe, nacho kilikuwa cha muraba pande zake zikiwa na upana wa metre kumi. Chumba hiki kilikuwa mbele ya baraza la katikati. Kisha, akaniambia: Hapa ndipo Pahali Patakatifu Sana.
5
Yule mutu aliupima unene wa ukuta wa nyumba ya Yawe, nao ulikuwa metre tatu. Kulikuwa mufululizo wa vyumba vidogovidogo vilivyozunguka nyumba ya Yawe, vyenye upana wa metre mbili.
6
Vyumba hivi vilikuwa katika majengo ya gorofi tatu, na kila gorofi ilikuwa na vyumba makumi tatu. Ukuta wa inje wa hekalu kila kwenye gorofi ulikuwa mwembamba kuliko ule wa gorofi ya chini, kusudi vile vyumba vikuwe imara bila kuutegemea ukuta wa hekalu.
7
Kwa upande, zile kuta za hekalu zikitazamwa kutokea inje, zilionekana kuwa na unene uleule toka chini mpaka juu. Kuelekea ukuta wa inje wa nyumba ya Yawe, inje ya vyumba, kulikuwa ngazi mbili, ambazo zilifanya ikuwe vyepesi kwenda juu kutokea gorofi ya chini mpaka ile ya juu.
8
Kisha, nikaona kwamba hekalu lilikuwa likizungukwa na sakafu iliyonyanyuliwa, nayo ilikuwa ndio musingi wa zile gorofi tatu mbele ya hekalu, kimo cha musingi wa gorofi hizo ulikuwa sawa na ule ufito wa kupimia, metre tatu.
9
Unene wa ukuta wa inje wa vyumba vya ndani ulikuwa metre mbili na nusu. Nafasi wazi kati ya vyumba vya pembeni mbele ya hekalu
10
na vyumba vya walinzi vilikuwa na upana wa metre kumi, kuzunguka hekalu.
11
Kulikuwa milango kwenye vyumba vya pembeni kutokea kwenye kiwanja, mumoja upande wa kaskazini na mwingine upande wa kusini. Na musingi uliounganishwa na kiwanja ulikuwa na upana wa metre mbili na nusu.
12
Kwa mwisho kabisa wa kiwanja, upande wa magaribi kulikuwa jengo lenye urefu wa metre makumi ine na tano na upana wa metre makumi tatu na tano. Kuta zake zilikuwa na unene wa metre mbili na nusu.
13
Yule mutu akapima upande wa inje wa hekalu nao ulikuwa na urefu wa metre makumi tano. Tokea nyuma ya nyumba ya Yawe kupitia ile nafasi ya kupitia, mpaka mwisho wake, upande wa magaribi, umbali wake ulikuwa vilevile metre makumi tano.
14
Urefu mbele ya hekalu tangu upande huu mpaka upande huu ukichanganya na ile nafasi wazi, ulikuwa vilevile metre makumi tano.
15
Yule mutu akapima urefu wa jengo mpaka magaribi pamoja na mabaraza yake pande zake zote, nalo lilikuwa na urefu wa metre makumi tano. Chumba cha kuingilia katika hekalu, Pahali Patakatifu, na Pahali Patakatifu Sana,
16
vyote vilipambwa kwa mbao tangu kwenye sakafu mpaka kwenye madirisha. Madirisha haya yangeweza kufunikwa.
17
Mpaka kwenye nafasi juu ya mulango hata kwenye chumba cha ndani na inje yake, vilevile juu ya kuta ndani ya chumba cha ndani na kwenye baraza kulikuwa michoro iliyofanana na
18
miti ya gazi na picha za makerubi. Kisha kila muti wa ngazi kulichorwa picha ya kerubi kukizunguka chumba chote. Kila kerubi alikuwa na nyuso mbili:
19
uso wa mwanadamu ulioelekea kwenye muti wa ngazi upande mumoja na uso wa simba ulioelekea kwenye muti wa ngazi upande mwingine. Hivi ndivyo ilivyokuwa kwenye nyumba nzima,
20
tangu sakafu mpaka juu ya milango kulichorwa makerubi na miti ya ngazi.
21
Miimo ya Pahali Patakatifu ilikuwa ya muraba. Mbele ya mulango wa kuingilia Pahali Patakatifu Sana kulikuwa kitu kilichoonekana kama
22
mazabahu ya mbao. Urefu wake kwenda juu ulikuwa metre moja na nusu na upana wa metre moja. Pembe zake, tako lake, na pande zake zote zilikuwa zimetengenezwa kwa mbao. Yule mutu akaniambia hivi: Hii ndiyo meza inayokaa mbele ya Yawe.
23
Kulikuwa mulango wa kuingia kwenye baraza la hekalu na mulango wa kuingia kwenye Pahali Patakatifu Sana.
24
Milango hiyo ilikuwa na sehemu mbilimbili, kwa hiyo kila mulango uliweza kufunguka katikati.
25
Kwenye mulango wa kuingilia kwenye baraza kulichorwa makerubi na miti ya ngazi kama ilivyokuwa kwenye kuta. Na kulikuwa kifuniko cha ubao kikifunika mulango kwa inje kwenye sehemu ya kuingilia ndani.
26
Pembeni ya chumba hiki, kulikuwa madirisha madogo na kuta zilipambwa kwa michoro ya miti ya ngazi.
← Chapter 40
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 42 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48