bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 30
Ezekiel 30
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 29
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 31 →
1
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Toa unabii useme hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Muomboleze na kusema: Ole kwetu siku ile!
3
Kwa maana, siku hiyo imekaribia; siku ile ya Yawe iko karibu. Hiyo itakuwa siku ya mawingu ya kutisha, siku ya maangamizi kwa mataifa.
4
Vita itakuja katika inchi ya Misri, na wasiwasi utakuwa katika inchi ya Etiopia, wakati Wamisri wengi wataanguka wameuawa, mali zao zitakaponyanganywa, na misingi ya miji yao kubomolewa.
5
Watu wote waliofungamana na Wamisri, ni kusema watu wa Etiopia, Puti, Ludi, Uarabu yote na Libya wataangamia pamoja nao.
6
Yawe anasema hivi: Wote wanaounga Misri mukono wataangamia, mashujaa wake wenye utukufu wataangamizwa, tangu Migidoli mpaka Sewene watu watauawa katika vita. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
7
Misri itakuwa jangwa kama inchi zinazokuwa jangwa na miji yake itakuwa mabomoko kama vile miji iliyoteketezwa.
8
Nitakapoiteketeza Misri kwa moto na kuvunjavunja wasaidizi wake wote, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
9
Siku hiyo, nitapeleka wajumbe kwenda kuwatisha Waetiopia wanaojizania kuwa na usalama. Watatetemeka siku Misri itakapoangamia. Kweli! Kweli siku hiyo inakuja!
10
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitamutumia Nebukadneza, mufalme wa Babeli, kwa kukomesha utajiri wa inchi ya Misri.
11
Nebukadneza mwenyewe pamoja na watu wake, taifa la hatari kuliko mataifa yote, watatumwa kuiangamiza inchi ya Misri. Watachomoa panga zao juu ya Misri na kuijaza inchi hiyo watu waliouawa.
12
Nitaukausha muto Nili na vijito vyake, na kuuzisha inchi ya Misri katika mikono ya watu waovu. Nitasababisha uharibifu katika inchi yote kwa mukono wa watu wageni. Ni Mimi Yawe ninayesema hivyo.
13
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaharibu sanamu za miungu, na kukomesha miungu ya uongo ya muji wa Nofi. Hakutakuwa mukubwa tena huko Misri. Nitasababisha hofu itawale katika inchi ya Misri.
14
Muji wa Patro nitaufanya kuwa tupu, muji wa Soani nitauteketeza kwa moto, nitauazibu muji wa No.
15
Nitamwanga kasirani yangu juu ya Sini, ile kimbilio inayotegemewa na Misri; na kuangamiza makundi ya watu wa No.
16
Nitateketeza inchi ya Misri kwa moto. Sini utashikwa na wasiwasi mukubwa, ukuta wa Nofi utabomolewa, nao Nofi utashambuliwa na waadui muchana wazi.
17
Vijana wanaume wa Oni na Pibeseti watauawa kwa upanga, na wakaaji wengine watapelekwa katika uhamisho.
18
Huko Tapanesi muchana utakuwa giza wakati nitakapovunja mamlaka ya Misri na kiburi chake kikubwa kitakapokomeshwa. Wingu litaifunika inchi ya Misri na watu wake watakamatwa mateka.
19
Ndivyo nitakavyoiazibu Misri. Na watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
20
Siku ya saba ya mwezi wa kwanza, mwaka wa kumi na mumoja tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
21
Wewe mwanadamu! Nimeuvunja mukono wa Mufalme wa Misri, nao haukutunzwa na dawa kusudi uweze kupona na kuweza kushika upanga.
22
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitapingana na Mufalme wa Misri. Nitaivunja mikono yake yote miwili, ule muzima na hata ule uliovunjika. Na upanga unaokuwa katika mukono wake utaanguka chini.
23
Nitawasambaza Wamisri kati ya mataifa na kuwaeneza katika inchi zingine.
24
Nitaitia mikono ya mufalme wa Babeli nguvu na kutia upanga wangu katika mukono wake. Lakini nitaivunja mikono ya Mufalme wa Misri, naye atalalamika mbele ya mufalme wa Babeli kama mutu aliyeumizwa vibaya sana.
25
Nitaimarisha mikono ya Mufalme wa Babeli, lakini mikono ya Mufalme wa Misri itaregea. Hapo watu watatambua kwamba mimi ni Yawe. Nitakapotia upanga wangu katika mukono wa Mufalme wa Babeli, ataunyoosha juu ya inchi ya Misri kwa kuiazibu,
26
nami nitawasambaza Wamisri kati ya mataifa mengine na kuwaeneza katika inchi zingine. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
← Chapter 29
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 31 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48