bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 31
Ezekiel 31
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 30
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 32 →
1
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa tatu, mwaka wa kumi na mumoja tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Umwambie Mufalme wa Misri na watu wake wote hivi: Wewe unafanana na nini kwa ukubwa wako?
3
Wewe ni kama muti wa mwerezi wa Lebanoni wenye matawi mazuri na majani mengi na shina refu. Kilele chake kinafika hata katika mawingu.
4
Maji yaliustawisha, vilindi vya maji viliulisha. Mito ilibubujika pahali ulipoota, ikapeleka vijito kwenye miti yote ya pori.
5
Kwa hiyo, ulirefuka sana kupita miti yote katika pori; matawi yake yalizidi kuwa mengi na makubwa, kutokana na maji mengi ndani ya mizizi yake.
6
Ndege wote waliweka chicha katika matawi yake, nyama wa pori walizalia chini yake, mataifa yote makubwa yalikaa chini ya kivuli chake.
7
Ulikuwa muzuri kwa ukubwa wake, na kwa urefu wa matawi yake. Mizizi yake ilipenya chini mpaka penye maji mengi.
8
Kati ya miti ya mierezi ya bustani ya Mungu, hakuna muti uliolingana nao, wala misunobari haikulingana na matawi yake, mibambakofi haikuwa na matawi kama yake, hata muti wowote wa bustani ya Mungu haukulingana nao kwa uzuri.
9
Mimi niliufanya kuwa muzuri kwa matawi yake mengi; ulionewa wivu na miti yote ya Edeni iliyokuwa katika bustani ya Mungu.
10
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu ulirefusha kimo chake na kufikisha kilele chake katika mawingu makubwa, ukajivunia urefu wake,
11
nitautia katika mikono ya mukubwa kati ya mataifa. Yeye, atauazibu. Nimeutupilia mbali kadiri ya uovu wake.
12
Watu wa mataifa mengine ya hatari sana, wataukata na kuuangusha chini na kuulalisha chini. Matawi yake yataanguka chini kwenye mulima na kila pahali katika mabonde; yatavunjika na kulala chini katika mitelemuko yote. Watu wote wataondoka chini ya kivuli chake na kuuacha.
13
Ndege wote watatua juu ya mabaki yake na nyama wote wa pori watakanyaga matawi yake.
14
Hayo yameupata kusudi muti wowote unaokuwa pahali penye maji usiweze kurefuka tena kwa kimo hicho wala kukifikisha kilele chake katika mawingu. Muti wowote unaokunyweshwa maji usiweze tena kufikia urefu huo. Kwa maana kila kitu mwisho wake ni kifo; hata na watu vilevile. Wote watashiriki hali ya wanaoshuka katika shimo kwa wafu.
15
Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ileile muti wa mwerezi ulipofika katika kuzimu nilitandaza giza nene juu yake, nikaufunika; mito yake niliikausha na mutiririko wa maji yake mengi nikaukomesha. Nayo Lebanoni niliiweka katika giza kwa ajili yake, na miti yote katika pori ikazimia kwa ajili yake.
16
Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa sauti ya kuanguka kwake, wakati nilipouangusha chini katika kuzimu pamoja na wale wanaoshuka ndani ya shimo kwa wafu. Nayo miti yote ya Edeni, miti mizuri na ya pekee ya Lebanoni ambayo ilimwangiliwa maji, ilifarijiwa huko chini kwa wafu.
17
Hiyo nayo ilishuka kule katika kuzimu pamoja nao, ikajiunga na wale waliofungamana nao na ambao waliikaa chini ya kivuli chake.
18
Kwa uzuri na ukubwa wa muti huo, hakuna muti wowote katika bustani ya Edeni ambao uliweza kulinganishwa nao. Sasa, muti huo ni wewe Mufalme wa Misri. Wewe utatupwa chini kwa wafu pamoja na miti ya Edeni. Utalala karibu na wale wasiomujua Mungu na wale waliouawa kwa upanga. Hiyo itakuwa hali yako ewe Mufalme wa Misri, wewe na watu wako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
← Chapter 30
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 32 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48