bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 39
Ezekiel 39
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 38
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 40 →
1
Bwana wetu Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya Gogi. Useme: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Gogi mutawala mukubwa wa mataifa ya Meseki na Tubali.
2
Nitakugeuza na kukuelekezea upande mwingine na kukuongoza kutoka mbali upande wa kaskazini uende kushambulia milima ya Israeli.
3
Kisha nitauvunja upinde wako katika mukono wako wa kushoto, na mishale yako katika mukono wako wa kuume nitaiangusha chini.
4
Utakufa juu ya milima ya Israeli, wewe pamoja na makundi yako yote ya waaskari na mataifa yanayokuwa pamoja nawe. Nami nitaitoa miili yao ikuliwe na ndege wa kila aina na nyama wakali.
5
Utakufia katika pori. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
6
Nitawasha moto juu ya inchi ya Magogi na juu ya wote wanaokaa salama katika inchi za kandokando ya bahari. Nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.
7
Nitajulisha jina langu takatifu kwa watu wangu Waisraeli, wala sitaruhusu tena watu walikufuru jina langu takatifu. Nayo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe, Mutakatifu wa Israeli.
8
Siku ile ninayosema juu yake, kwa hakika inakuja. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
9
Kwa hiyo, watu wanaoishi katika miji ya Israeli watatoka na kukusanya silaha zilizoachwa na kuzichoma kwa moto. Watatumia hizo ngao, pinde, mishale, mikuki na magongo, kama kuni za kuwasha moto kwa muda wa miaka saba.
10
Hawatahitaji kuokota kuni katika mashamba, wala kukata miti katika pori, kwa sababu watazitumia hizo silaha kwa kuwasha nazo moto. Watabeba mali za wale walioteka mali zao na kuwanyanganya mali zao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
11
Katika siku ile, nitamupa Gogi pahali pa kufanyia maziko katika inchi ya Israeli, katika Bonde la Wasafiri, upande wa mashariki wa bahari ya Chumvi. Gogi atazikwa huko pamoja na kundi lake lote la waaskari, nao wasafiri watazuizwa kupita kule. Bonde hilo litaitwa, Bonde la Hamoni-Gogi.
12
Kwa kuisafisha inchi, Waisraeli watatumia muda wa miezi saba kuzika maiti hizo.
13
Watu wote katika inchi watashugulika na kuwazika. Na hilo litakuwa jambo la kuwapatia sifa, siku ile nitakapoonyesha utukufu wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
14
Kisha miezi hiyo saba, watatenga watu watakaopitapita katika inchi kwa kutafuta maiti ambazo zitakuwa bado hazijazikwa, wazizike kwa kuisafisha inchi.
15
Wanapoona mufupa wa mutu wataweka kitambulisho juu yake kusudi wale wanaozika wakuje na kuuzika katika Bonde la Hamoni-Gogi.
16
Huko kutakuwa vilevile muji utakaoitwa “Muji wa watu wengi”. Ndivyo watakavyoisafisha inchi.
17
Sasa, ewe mwanadamu, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Uite ndege wote na nyama wote wa pori wakusanyike toka pande zote na kuja kukula karamu ya sadaka ya nyama ninayowatayarishia, ambayo itakuwa kubwa sana juu ya milima ya Israeli, ambako watakula nyama na kunywa damu.
18
Watakula nyama ya mashujaa, watakunywa damu ya wakubwa wa dunia watakaochinjwa kama kondoo dume au wana-kondoo, mabeberu au ngombe dume wanono wa Basani.
19
Katika karamu hiyo niliyowafanyia watakula mafuta na kushiba. Watakunywa damu na kulewa.
20
Kwenye meza yangu, watashibishwa kwa farasi, waaskari wapanda-farasi, mashujaa na watu wote wa vita. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
21
Yawe akaniambia hivi: Nitaonyesha utukufu wangu kwa mataifa yote, na kuwaonyesha jinsi ninavyotumia nguvu yangu kwa kutimiza hukumu zangu za haki.
22
Waisraeli watajua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao, tangu siku hiyo na itakayokuja.
23
Mataifa yatajua kwamba Waisraeli walikwenda katika uhamisho kutokana na makosa yao wenyewe waliyonikosea. Waliniasi, nami nikageuka wasipate kuniona, nikawatoa katika mikono ya waadui zao wakauawa.
24
Niligeuka wasipate kuniona nikawatendea kulingana na uchafu na makosa yao.
25
Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitawahurumia Waisraeli wazao wa Yakobo, na kuwarudishia fanaka yao. Ninataka jina langu takatifu liheshimiwe siku zote.
26
Watakapokuwa wanaishi kwa usalama katika inchi yao, bila kutishwa, watasahau haya yao na uasi walionitendea.
27
Wakati huo, nitakuwa nimewarudisha kutoka kwa mataifa na kuwakusanya kutoka inchi za waadui zao na kuonyesha utakatifu wangu mbele ya mataifa mengi.
28
Kisha watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao, kwa sababu mimi niliwapeleka katika uhamisho kati ya mataifa na kuwarudisha tena katika inchi yao. Sitamwacha hata mutu wao mumoja abakie kati ya mataifa.
29
Nitakapowajaza Waisraeli Roho yangu, sitageuka tena wasipate kuniona. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
← Chapter 38
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 40 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48