bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 37
Ezekiel 37
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 36
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 38 →
1
Yawe alinijaza uwezo wake mimi Ezekieli. Roho wake akanitwaa na kunipeleka katika bonde lililokuwa limejaa mifupa.
2
Basi, akanitembeza kila pahali katika bonde lile. Kulikuwa mifupa mingi sana katika bonde lile, nayo ilikuwa inakauka kabisa.
3
Yawe akaniuliza hivi: Wewe mwanadamu! Mifupa hii inaweza kuishi tena? Nami nikamujibu: Ee Bwana wetu Yawe, wewe unajua!
4
Naye akaniambia: Toa unabii juu ya mifupa hii. Uiambie hivi: Enyi mifupa yenye kukauka, musikilize neno la Yawe.
5
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitapulizia tena pumzi ndani yenu, nanyi mutaishi.
6
Nitawatia mishipa na nyama, nitawafunika ngozi na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mutaishi. Hapo mutajua kwamba mimi ni Yawe.
7
Basi, nikatoa unabii kama nilivyoamriwa. Nilipokuwa nikitoa unabii, kukatokea kelele kama ya mukwaruzo na ile mifupa ikaanza kusogeleana na kuungana.
8
Niliangalia, nikaona ile mifupa imewekewa mishipa na nyama na kufunikwa kwa ngozi. Lakini haikukuwa na uzima.
9
Halafu, Yawe akaniambia: Ewe mwanadamu, kwa ajili yangu toa unabii kwa upepo, uuambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ewe upepo kuja toka pande zote ine na kuipulizia miili hii iliyokufa kusudi ipate kuishi.
10
Basi, mimi nikatoa unabii kama alivyoniamuru, nayo pumzi ikaingia ndani yao, nayo ikapata tena uzima, ikasimama wima: kundi kubwa ajabu.
11
Kwa hiyo Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Mifupa hiyo ni mufano wa watu wote wa inchi ya Israeli. Wao, wanasema: Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yamepotea nasi tumekwisha kabisa.
12
Kwa hiyo, toa unabii, uwaambie kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Enyi watu wangu, nitayafunua makaburi yenu na kuwafufua kutoka ndani ya makaburi yenu. Nitawarudisha ndani ya nyumba zenu katika inchi ya Israeli.
13
Nanyi, enyi watu wangu, mutatambua kwamba mimi ni Yawe nitakapofunua makaburi yenu na kuwafufua kutoka ndani ya makaburi yenu.
14
Nitatia Roho yangu ndani yenu, nanyi mutaishi, nami nitawaweka katika inchi yenu wenyewe. Kwa hiyo mutatambua kwamba mimi Yawe nimesema, nami nitafanya hayo. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.
15
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
16
Wewe mwanadamu, twaa kijiti kimoja, uandike juu yake maneno haya: Kwa Yuda na Waisraeli wanaoshirikiana naye. Kisha twaa kijiti kingine uandike juu yake maneno haya: Kwa Yosefu (kijiti cha Efuraimu) na Waisraeli wanaoshirikiana naye.
17
Halafu uvitwae vijiti hivyo na kuvishikamanisha kusudi vionekane kama kijiti kimoja.
18
Wanainchi wenzako watakuuliza: Hautatuelezea maana ya jambo hilo?
19
Wewe utawajibu: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakitwaa kijiti cha Yosefu (kinachokuwa katika mukono wa Efuraimu) na makabila ya Israeli yanayoungana naye, nami nitakishikamanisha na kijiti cha Yuda kusudi vijiti hivyo viwili vifanywe kijiti kimoja katika mukono wangu.
20
Utakamata vile vijiti ulivyoandika juu yake katika mukono wako kwa jinsi kila mutu apate kuona,
21
uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawatoa Waisraeli kutoka mataifa walikokwenda; nitawakusanya toka pande zote na kuwarudisha katika inchi yao.
22
Nitawafanya kuwa taifa moja katika inchi juu ya milima ya Israeli; mufalme mumoja atakuwa mufalme wao wote. Hawatakuwa tena mataifa mawili wala hawatagawanyika tena kuwa falme mbili.
23
Hawatajichafua tena kwa kuabudu sanamu za miungu yao na kwa mambo yao ya kuchukiza wala kwa makosa yao. Nitawaokoa wasikuwe tena waasi. Nao watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
24
Mutumishi wangu Daudi atakuwa mufalme wao; watakuwa na muchungaji mumoja tu. Watayafuata maagizo yangu na kushika masharti yangu.
25
Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.
26
Nitafanya nao agano la amani, nalo litakuwa agano la milele. Nitawabariki na kuwafanya wakuwe wengi, nami nitaweka hekalu langu kati yao milele.
27
Nitaishi kati yao; nitakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wangu.
28
Nayo mataifa yatatambua kwamba mimi Yawe, nimewatakasa Waisraeli na kwamba hekalu langu liko kati yao milele.
← Chapter 36
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 38 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48