bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 36
Ezekiel 36
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 35
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 37 →
1
Yawe aliniambia hivi: Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya milima ya Israeli. Uiambie isikilize maneno yangu.
2
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waadui zenu wamewazomea na kusema kwamba ninyi mumekuwa mali yao!
3
Kwa hiyo, wewe Ezekieli, toa unabii useme kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Watu wamewafanya ninyi milima ya Waisraeli kuwa tupu na kuwashambulia kutoka kila upande hata mumekuwa mali ya mataifa mengine, mukakuwa kitu cha kusimangwa na kuchekelewa kati ya watu!
4
Kwa hiyo, enyi milima ya Waisraeli, musikie neno la Bwana wenu Yawe. Anasema juu ya ninyi milima na vilima, mifereji na mabonde, jangwa tupu na miji ya matongo, na miji iliyokamatwa mateka na kuzarauliwa na mataifa yote yanayowazunguka.
5
Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wivu wangu unawaka sana. Nitayaazibu mataifa mengine na hasa watu wa inchi ya Edomu. Wao kwa furaha ndani ya moyo na mazarau walikamata hiyo inchi inayokuwa yangu ikuwe yao.
6
Kwa hiyo, ewe mwanadamu, toa unabii juu ya inchi ya Waisraeli, uiambie milima na vilima, vijito na mabonde kwamba Bwana wao Yawe anasema hivi: Ninasema kutokana na upendo wangu wenye wivu juu ya ninyi, inchi yangu, kwa sababu mumetukanwa na watu wa mataifa.
7
Bwana wenu Yawe anasema hivi: Ninaapa hakika kwamba watu wa mataifa yanayokuwa jirani yenu watatukanwa wao wenyewe.
8
Lakini juu ya milima ya Waisraeli, miti itatoa matawi na kuzaa matunda kwa ajili ya watu wangu Waisraeli, maana wao wanakaribia kurudi katika inchi yao.
9
Mimi niko upande wenu, nitahakikisha kuwa udongo wenu utalimwa na kupandwa mbegu.
10
Nitawazidisha sana Waisraeli. Miji itakaliwa, na mabomoko yatajengwa upya.
11
Nitawafanya watu na nyama waongezeke na kuwa wengi. Nitawafanya ninyi milima mukaliwe tena kama zamani. Nitawatendea mema mengi kuliko zamani. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
12
Nitawafanya watu wangu Waisraeli watembee juu yenu. Nanyi mutakuwa urizi wao, wala hamutawafanya tena wakufiwe na watoto wao.
13
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa vile watu wamesema juu yenu kwamba munakula watu, na mumeliteketezea taifa lenu watoto wake,
14
basi, sasa hamutakula tena watu wala kuteketezea taifa lenu watoto wake.
15
Sitaruhusu tena mataifa yawatukane, wala kuwazarau tena. Hamutasababisha taifa lenu kukosa. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
16
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
17
Wewe mwanadamu! Waisraeli walipoishi katika inchi yao waliichafua kwa mienendo na matendo yao. Niliyaona matendo yao kuwa sawa na mwanamuke anayekuwa muchafu wakati wa ugonjwa wake wa mwezi.
18
Niliwamwangia kasirani yangu kwa sababu ya damu waliyomwanga katika inchi na kwa sababu ya miungu ambayo kwa ajili yao waliichafua inchi.
19
Niliwasambaza kati ya mataifa, wakasambazwa katika inchi nyingine. Niliwaazibu kadiri ya tabia yao na matendo yao.
20
Hata walipokuwa kati ya mataifa walilikufuru jina langu takatifu, hata watu wakasema hivi juu yao: Hawa ndio wale watu wa Yawe, lakini wamelazimishwa kuondoka katika inchi yake!
21
Hiyo ilinifanya kuhangaika juu ya jina langu takatifu ambalo Waisraeli walilikufuru kati ya mataifa walikokwenda.
22
Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninachotaka kufanya si kwa faida yenu ninyi watu wa inchi ya Israeli, lakini ni kwa heshima ya jina langu takatifu mulilolikufuru kati ya mataifa mulikokwenda.
23
Nitalitakasa jina langu kubwa mulilokufuru kati ya mataifa. Na kwa hiyo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nitawatumia ninyi kuonyesha utakatifu wangu mbele yao.
24
Nitawaondoa ninyi katika kila taifa na kuwakusanya kutoka inchi zote za kigeni; nitawarudisha katika inchi yenu wenyewe.
25
Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.
26
Nitawapa moyo mupya na kuweka roho mupya ndani yenu. Nitauondoa kwenu moyo mugumu kama jiwe na kuwapa moyo musikilivu.
27
Nitatia roho yangu ndani yenu; nitawafanya mufuate masharti yangu na kushika maagizo yangu.
28
Mutakaa katika inchi niliyopatia wazee wenu. Mutakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
29
Nitawaokoa kutoka uchafu wenu wote. Nitaiamuru ngano iongezeke, wala sitawaletea njaa tena.
30
Nitayazidisha matunda ya miti na mazao ya mashamba kusudi musizarauliwe tena kwa ajili ya njaa kati ya mataifa.
31
Kisha mutakapokumbuka mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya, mutajichukia wenyewe kwa sababu ya maovu yenu na machukizo muliyofanya.
32
Lakini mujue kwamba sitafanya hivyo kwa ajili yenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Lakini mupate haya na kufazaika kwa sababu ya matendo yenu, enyi Waisraeli!
33
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nitakapowasafisha ninyi toka maovu yenu yote, nitaifanya miji yenu ikaliwe, nayo mabomoko yajengwe upya.
34
Inchi iliyokuwa jangwa italimwa tena, hata atakayepita huko hataiona kuwa jangwa.
35
Nao watu watasema: Inchi hii iliyokuwa jangwa, sasa imekuwa kama bustani ya Edeni, nayo miji iliyokuwa ukiwa, matongo na mabomoko, sasa inakaliwa na watu, tena inazungukwa na kuta!
36
Hapo mataifa yaliyobaki kandokando yenu, yatatambua kwamba ni mimi Yawe niliyejenga upya yaliyoharibiwa na kupanda mbegu katika inchi iliyokuwa jangwa. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo, na nitafanya hayo.
37
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waisraeli wataniomba niwafanye kuwa wengi kama kundi la kondoo, nami nitawafanya hivyo.
38
Wataniomba wakuwe wengi kama kundi la kondoo wa kutolewa sadaka, kama kundi la kondoo katika Yerusalema wakati wa sikukuu zake. Hivi ndivyo miji yenu iliyokuwa ukiwa itakavyojaa makundi ya watu. Kwa hiyo watatambua kwamba mimi ni Yawe.
← Chapter 35
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 37 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48