bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 40
Ezekiel 40
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 39
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 41 →
1
Katika mwaka wa makumi mbili na tano tangu tulipopelekwa katika uhamisho, siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, siku hiyo Yawe alinijaza uwezo wake. Ilikuwa mwaka wa kumi na ine tangu pale Yerusalema ulipotekwa.
2
Basi, nikiwa katika maono Yawe akanipeleka mpaka katika inchi ya Israeli, akaniweka juu ya mulima murefu sana, na upande wa kusini kulikuwa majengo yaliyoonekana kama muji.
3
Basi, alinipeleka huko, nami nikamwona mutu aliyeonekana anaangaa kama shaba. Katika mikono yake mutu huyo alikuwa na kamba ya kitani ya kupima nayo pamoja na ufito wa kupima nao, naye alikuwa amesimama karibu na mulango.
4
Basi, akaniambia hivi: Wewe mwanadamu! Angalia vizuri na kusikiliza kwa uangalifu. Shika kwa moyo uone kila kitu nitakachokuonyesha maana umeletwa hapa kusudi nikuonyeshe kitu. Unapaswa kuwatangazia watu wa Israeli kila kitu utakachoona.
5
Basi, huko, niliona hekalu nalo lilikuwa limezungukwa na ukuta upande wa inje. Yule mutu akatwaa ufito wake wa kupima ambao ulikuwa na urefu kwenda juu wa metre tatu, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na kimo cha metre tatu na unene wa metre tatu.
6
Kisha, akaenda kwenye mulango wa upande wa mashariki akapanda juu ya ngazi naye akiwa juu akapima kizingiti cha mulango ambacho kilikuwa na upana wa metre tatu.
7
Kulikuwa vyumba vya walinzi kila upande wa nafasi ya kupitia na kila kimoja kilikuwa cha muraba: urefu metre tatu upana metre tatu. Kuta zilizotenganisha vyumba hivyo zilikuwa na unene metre mbili na nusu. Kulikuwa baraza ya urefu wa metre tatu ambao ulielekea kwenye chumba kikubwa mbele ya hekalu.
8
Yule mutu akakipima vilevile chumba hicho, nacho kilikuwa na upana wa metre ine.
9
Halafu akapima kuta zake za inje zikaonekana zina unene wa metre moja. Sehemu ya ndani ya mulango ilikuwa sehemu iliyokuwa karibu zaidi na hekalu.
10
Kulikuwa sehemu ya kuingilia iliyokuwa na vyumba vitatu vya walinzi, kila upande na vyote vilikuwa na ukubwa uleule; nazo kuta zilizovitenganisha zilikuwa na unene uleule.
11
Kisha, yule mutu akapima upana wa nafasi ya kupitia katika mulango. Upana wake ulikuwa metre sita na nusu. Ukubwa wote wa baraza ya katikati ya kupitia ulikuwa metre tano.
12
Mbele ya vyumba vya walinzi ambavyo vilikuwa muraba: metre tatu kwa tatu, kulikuwa ukuta mufupi kama kizuizi ukiwa na kimo cha sentimetre makumi tano na unene sentimetre makumi tano.
13
Yule mutu akapima hatua kutoka ukuta wa nyuma wa chumba kimoja mpaka kwenye ukuta wa nyuma ya chumba upande wa pili penye nafasi ya kupitia, akapata metre kumi na mbili na nusu.
14
Chumba cha mwisho kabisa kilielekea kwenye kiwanja. Akakipima chumba hicho nacho kilikuwa na upana metre kumi.
15
Kutoka mbele ya mulango kwenye kiingilio mpaka kwenye baraza la ndani la mulango kulikuwa metre makumi mbili na tano.
16
Kulikuwa matundu madogomadogo kwenye miimo ya inje ya vyumba vyote na hata kwenye kuta zilizotenganisha vyumba. Kulikuwa michoro ya miti ya ngazi kwenye miimo ya ndani iliyoelekea baraza la kupitia.
17
Kisha yule mutu akanipeleka mpaka katika kiwanja cha inje cha hekalu. Huko kulikuwa vyumba makumi tatu vyenye kuuzunguka ukuta wa inje na mbele ya vyumba hivyo kulikuwa sakafu ya mawe.
18
Sakafu hiyo ilitandazwa kuzunguka milango kwa kufuatana na urefu wa milango hiyo; hiyo ilikuwa sakafu ya chini.
19
Kisha, yule mutu akapima hatua ya njia iliyokuwa ikitoka kwenye kiwanja cha ndani cha sehemu ya chini ikielekea inje ya kiwanja hicho, akapata metre makumi tano.
20
Kisha, yule mutu akapima urefu na upana wa mulango wa upande wa kaskazini na kiwanja cha inje.
21
Kulikuwa vyumba vitatu vya walinzi kila upande wa mulango, vipimo vya miimo yake na nguzo yake vilikuwa kama vile vya mulango wa kwanza. Urefu wote wa ile njia ulikuwa kwa jumla metre makumi mbili na tano na upana wake metre kumi na mbili na nusu.
22
Chumba cha kuingilia na madirisha na nguzo zake, pamoja na ile miti ya ngazi iliyochorwa juu ya ukuta, vyote vilifanana na vile vya mulango wa upande wa mashariki.
23
Kutoka hapo penye njia ya kuingilia ya upande wa kaskazini na kuvuka hicho kiwanja cha ndani moja kwa moja kulikuwa njia ingine ya kuingilia iliyoelekea kwenye kiwanja cha ndani, kama ilivyokuwa upande wa mashariki. Yule mutu alipima urefu wa kutoka kwenye njia mpaka kwenye njia, akapata metre makumi tano.
24
Yule mutu akanipeleka upande wa kusini; huko nako kulikuwa mulango; alipima miimo yake na baraza na vipimo vyake vilikuwa sawa na miimo na baraza zingine.
25
Kulikuwa madirisha pande zote kama ilivyokuwa katika vyumba vingine. Urefu wake ulikuwa metre makumi mbili na tano na upana wake metre kumi na mbili na nusu.
26
Kulikuwa ngazi saba za kupandia kwenye njia hiyo ya kuingilia na kwa mwisho wake kulikuwa baraza iliokuwa inaelekeana na kiwanja. Kulikuwa michoro ya miti ya ngazi kwenye kuta za ndani zilizokuwa mbele ya njia hiyo ya kuingilia.
27
Mbele ya njia hiyo ya kuingilia kulikuwa njia ya kuingilia kwenye kiwanja cha ndani. Yule mutu akapima urefu kati ya hizo njia, akapata metre makumi tano.
28
Yule mutu akanipitisha kwenye njia ya kuingilia upande wa kusini, tukafika kwenye kiwanja cha ndani. Aliipima hiyo njia nayo ilikuwa sawa na zile njia zingine za kuingilia kwenye kuta za inje.
29
Vyumba vya walinzi, baraza, na kuta zake vilikuwa na ukubwa ule ule kama vile vingine; kulikuwa vilevile madirisha kandokando ya hiyo njia ya kuingilia na kwenye baraza. Ilikuwa na urefu metre makumi mbili na tano na upana metre kumi na mbili na nusu.
30
Kulikuwa vyumba kandokando ya hiyo njia ya kuingilia, vikiwa na urefu wa metre makumi mbili na tano na upana wake metre kumi na mbili na nusu.
31
Ile baraza ilikuwa inaelekea kiwanja cha inje. Na kulikuwa michoro ya miti ya ngazi kwenye nguzo kandokando ya hiyo njia ya kuingilia. Kulikuwa ngazi nane za kupandia kwenye mulango huu.
32
Yule mutu alinipeleka upande wa mashariki wa kiwanja cha ndani. Akaipima ile njia ya kuingilia, nayo ilikuwa na urefu kama zile njia zingine za kuingilia.
33
Vyumba vyake vya walinzi, nguzo zake za ndani pamoja na baraza vilikuwa na ukubwa kama vile vingine. Kulikuwa madirisha pande zote hata kwenye baraza na chumba cha kuingilia. Urefu wake ulikuwa metre makumi mbili na tano na upana wake metre kumi na mbili na nusu.
34
Kile chumba cha kuingilia kilikuwa kinaelekea kwenye kiwanja cha inje. Miti ya ngazi ilichorwa kwenye kuta kwenye nafasi ya kupitia. Kulikuwa ngazi nane za kupandia kuelekea kwenye mulango huu.
35
Kisha yule mutu akanipeleka kwenye njia ya kuingilia upande wa kaskazini. Basi, akaipima hiyo njia ya kuingilia, nayo ilikuwa sawa na zile njia zingine.
36
Huko nako kulikuwa vyumba vya walinzi, kuta za ndani zilizopambwa, baraza ya kuingilia na madirisha pande zote. Urefu wake wote ulikuwa metre makumi mbili na tano na upana metre kumi na mbili na nusu.
37
Ile baraza ya kuingilia ilikuwa inaelekea kwenye kiwanja cha inje; kulikuwa miti ya ngazi iliyochorwa kwenye kuta za hiyo nafasi ya kupitia. Kulikuwa vilevile ngazi nane za kupandia kuelekea kwenye mulango huu.
38
Kwenye kiwanja cha inje, kulikuwa chumba cha zaidi kilichounganishwa na njia ya kuingilia ya ndani kwa upande wa kaskazini. Chumba hicho kilikuwa kinaelekea baraza ya kuingilia, na huko walisafishia nyama waliochinjwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa nzima.
39
Halafu katika baraza karibu na njia kulikuwa meza mbili upande mumoja na zingine mbili upande mwingine. Meza hizo zilitumika kuwa pahali pa kuchinjia sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya usamehe wa zambi na sadaka ya malipo ya kosa.
40
Inje ya baraza hiyo, kulikuwa meza mbili upande mumoja na mbili upande mwingine wa njia ya kuingilia kwenye mulango wa kaskazini.
41
Meza zote ambazo zilitumiwa kwa kuchinjia nyama wa sadaka zilikuwa nane: meza ine ndani ya baraza na meza ine inje ya baraza.
42
Kulikuwa vilevile meza ine ndani ya baraza zilizotumiwa kuandalia sadaka za kuteketezwa. Meza hizo zilikuwa zimejengwa kwa mawe yaliyochongwa. Urefu wa kwenda juu wa kila meza ulikuwa sentimetre makumi tano na upande wake wa juu ulikuwa muraba wenye upana wa sentimetre makumi saba na tano pande zote. Vifaa vyote vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na sadaka zingine viliwekwa juu ya meza hizo.
43
Ndani ya baraza hilo kulizungukwa na vijiti vya kutundikia, na nyama ziliwekwa juu ya meza.
44
Inje ya njia ya ndani kulikuwa vyumba vya walinzi kwenye kiwanja cha ndani kilichokuwa upande wa kaskazini wa njia. Vyumba hivyo vilielekea upande wa kusini. Chumba kimoja kilichokuwa upande wa mulango wa mashariki kilielekea upande wa kaskazini.
45
Yule mutu akaniambia hivi: Chumba hiki kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani wanaotumika katika nyumba ya Yawe,
46
na chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wanaotumika kwenye mazabahu. Makuhani hawa ni wale wa ukoo wa Zadoki, ndio hao kati ya watu wa kabila la Lawi wanaoruhusiwa kwenda mbele ya Yawe.
47
Yule mutu akapima kiwanja cha ndani, nacho kilikuwa muraba: pande zote zilikuwa na upana wa metre makumi tano. Mazabahu yalikuwa mbele ya nyumba ya Yawe.
48
Kisha, alinipeleka kwenye baraza la kuingilia ndani ya nyumba ya Yawe. Akapima mulango, nao ulikuwa na kimo cha metre mbili na nusu na upana wa metre saba. Na kuta zake zilikuwa na unene metre moja na nusu kila upande.
49
Kulikuwa ngazi za kupandia kwenye baraza la chumba cha kuingilia, ambalo lilikuwa na urefu wa metre kumi na upana metre sita. Kulikuwa nguzo mbili, nguzo moja kila upande wa mulango.
← Chapter 39
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 41 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48