bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 48
Ezekiel 48
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 47
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
1
Haya ndiyo majina ya makabila na sehemu zao: Kuanzia kwenye mupaka wa kaskazini kwenye barabara ya Hetiloni mpaka kuingia Hamati hata Hazorenoni unaokuwa katika Damasiki na Hamati upande wa kaskazini na kuendelea kutoka mashariki mpaka magaribi. Eneo hilo litakuwa la kabila la Dani.
2
Eneo linalofuatana na la Dani, kutoka mashariki mpaka magaribi litakuwa la Aseri.
3
Kabila la Nafutali, litapata eneo linalopakana na lile la Aseri, kutoka mashariki mpaka magaribi.
4
Kisha eneo la kabila la Nafutali litafuata eneo la kabila la Manase, kutoka mashariki mpaka magaribi.
5
Eneo linalopakana na eneo la Manase kutoka upande wa mashariki mpaka magaribi litakuwa la kabila la Efuraimu.
6
Eneo linalopakana na eneo la Efuraimu kutoka mashariki mpaka magaribi litakuwa la kabila la Rubeni.
7
Eneo linalopakana na eneo la Rubeni kutoka mashariki mpaka magaribi litakuwa la kabila la Yuda.
8
Kisha eneo la kabila la Yuda, utatenga eneo lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na upana kama huohuo, kutoka kaskazini mpaka kusini, na urefu huohuo kutoka mashariki mpaka magaribi, sawasawa na eneo la kabila lolote. Hapo katikati ya eneo hilo patakuwa hekalu la Mungu.
9
Eneo utakalotenga kwa ajili ya Yawe litakuwa lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kwa kilometre kumi.
10
Makuhani watakuwa na eneo lao katika eneo hilo. Eneo hilo litakuwa na urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kutoka mashariki mpaka magaribi, na kilometre tano kutoka kaskazini mpaka kusini. Hekalu la Mungu litakuwa katikati ya eneo hilo.
11
Eneo hilo litakuwa kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Zadoki, ambao walinitumikia kwa uaminifu na hawakuasi wakati Waisraeli walipoasi kama Walawi walivyofanya.
12
Hilo litakuwa eneo lao takatifu kutoka katika eneo takatifu la inchi, eneo takatifu kabisa, litakalopakana na eneo la Walawi.
13
Nao Walawi, eneo lao litakuwa upande wa kusini wa eneo la makuhani. Eneo hilo litakuwa na urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kutoka mashariki mpaka magaribi, na upana kilometre tano kutokea kaskazini mpaka kusini.
14
Hakuna sehemu yoyote ya eneo hilo itakayouzishwa au kutolewa kwa mutu yeyote, kwa sababu eneo hilo ni takatifu kwa Yawe; nalo ni bora kuliko yote katika inchi.
15
Ile sehemu ya eneo takatifu iliyobaki, yenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu na upana kilometre mbili na nusu, hilo ni kwa matumizi ya kawaida ya muji: pahali pa kuishi na eneo la mashamba. Katikati yake kutakuwa muji,
16
nao utakuwa wa muraba, kila upande metre elfu mbili mia mbili na makumi tano.
17
Kuuzunguka muji, kutakuwa na eneo wazi lenye upana wa metre mia moja na makumi mbili na tano.
18
Eneo ambalo litabaki kisha kujengwa kwa hekalu, upande wa kusini wa muji, kilometre tano kwa kilometre mbili na nusu upande wa mashariki, na kilometre tano kwa kilometre mbili na nusu upande wa magaribi, litakuwa eneo la walimaji kwa wakaaji wa muji.
19
Watumishi wote katika muji wa kabila lolote la Waisraeli wanaweza kulima katika eneo hilo.
20
Hivyo, eneo lote utakalotenga, ni kusema eneo takatifu pamoja na eneo la muji litakuwa la muraba, kilometre kumi na mbili na nusu kila upande.
21
Eneo linalobaki katika pande zote za eneo takatifu na eneo la muji, ni kusema lile eneo lenye eneo muraba likiwa na kilometre kumi na mbili na nusu kwa kila upande tokea mashariki mpaka magaribi, kuelekea maeneo ya makabila, litakuwa la mufalme. Lile eneo takatifu ambamo hekalu la Mungu litakuwa katikati yake,
22
na eneo la Walawi pamoja na lile eneo la muji, yatakuwa katikati ya eneo la mufalme. Eneo la mufalme litakuwa katika mupaka wa eneo la kabila la Yuda na eneo la kabila la Benjamina.
23
Makabila yaliyobaki yatagawanyiwa maeneo yao hivi: Kabila la Benjamina litapewa eneo kutoka mashariki mpaka magaribi.
24
Eneo linalopakana na eneo la Benjamina kutoka upande wa mashariki kuelekea upande wa magaribi litakuwa la kabila la Simeoni.
25
Eneo linalopakana na kabila la Simeoni kutoka upande wa mashariki kuelekea upande wa magaribi litakuwa eneo la kabila la Isakari.
26
Eneo linalopakana na kabila la Isakari kutoka upande wa mashariki kuelekea upande wa magaribi, litakuwa eneo la kabila la Zebuluni.
27
Eneo linalopakana na kabila la Zebuluni, kutoka mashariki kuelekea magaribi, litakuwa eneo la kabila la Gadi.
28
Eneo linalopakana na kabila la Gadi kuelekea kusini, mupaka utatoka muji wa Tamari mpaka kwenye chemichemi za Meriba-Kadesi na kupitia upande wa mashariki ya Misri mpaka kwenye bahari ya Mediteranea.
29
Hilo ndilo eneo la makabila ya Waisraeli. Humo ndimo watapewa maeneo yao, kila kabila eneo lake. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
30
Muji Yerusalema utakuwa na ukuta ambao utakuwa na milango hii ya kutokea na kuingilia: Upande wa kaskazini urefu wa ukuta utakuwa metre elfu mbili mia mbili na makumi tano. Upande huo wa kaskazini
31
utakuwa na milango mitatu: mulango wa Rubeni, mulango wa Yuda na mulango wa Lawi.
32
Ukuta wa upande wa mashariki utakuwa na urefu wa metre elfu mbili mia mbili makumi tano. Upande huo utakuwa na milango mitatu: mulango wa Yosefu, mulango wa Benjamina na mulango wa Dani.
33
Ukuta wa upande wa kusini utakuwa na urefu wa metre elfu mbili mia mbili na makumi tano. Upande huo utakuwa na milango mitatu: mulango wa Simeoni, mulango wa Isakari na mulango wa Zebuluni.
34
Ukuta wa upande wa magaribi utakuwa na urefu wa metre elfu mbili mia mbili makumi tano. Upande huo nao utakuwa na milango mitatu: mulango wa Gadi, mulango wa Aseri na mulango wa Nafutali.
35
Jumla ya urefu wa kuta zote ine utakuwa ni metre elfu kenda. Jina la muji kutokea sasa na kuendelea litakuwa: Yawe Yupo Hapa.
← Chapter 47
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48