bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 20
Ezekiel 20
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 21 →
1
Mwaka wa saba tangu kuhamishwa kwetu, siku ya kumi ya mwezi wa tano, wazee wamoja wa Waisraeli walikuja kumwuliza Yawe shauri, wakaikaa mbele yangu.
2
Basi, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
3
Wewe mwanadamu, sema na hao wazee wa Waisraeli. Uwaambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mumekuja kuniuliza shauri? Kama vile ninavyoishi, sitakubali kuulizwa shauri na ninyi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
4
Wewe mwanadamu, uko tayari kuwahukumu watu hawa? Basi, uwahukumu. Uwajulishe mambo wazee wao waliyofanya.
5
Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nilipowachagua Waisraeli niliwaapia wazao wa Yakobo. Nilijijulisha kwao katika inchi ya Misri, nikawaapia nikisema: Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
6
Siku hiyo niliwaapia kwamba nitawatoa katika inchi ya Misri na kuwapeleka mpaka kwenye inchi niliyowachagulia, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote.
7
Niliwaambia: Mutupilie mbali machukizo yote munayoyapenda; musijichafue na sanamu za miungu ya Misri, kwa maana mimi ni Yawe, Mungu wenu.
8
Lakini waliniasi, hawakutaka kunisikiliza. Hakuna hata mumoja kati yao aliyetupilia mbali machukizo yale waliyoyapenda, wala hawakuachana na sanamu za miungu ya Misri. Basi, nikafikiri kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao wakiwa kulekule katika inchi ya Misri.
9
Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.
10
Basi, mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, nikawapeleka katika jangwa.
11
Niliwapa masharti yangu na kuwafundisha maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi.
12
Niliwapa vilevile Sabato zangu zikuwe kitambulisho kati yangu na wao, wapate kujua kwamba mimi ni Yawe ninayewatakasa.
13
Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.
14
Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.
15
Hata hivyo, niliwaapia kulekule katika jangwa kwamba sitawaingiza katika inchi niliyowapa, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote.
16
Nilifanya hivyo kwa sababu waliyakataa maagizo yangu, hawakufuata masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu; maana walijitoa kwa moyo juu ya sanamu za miungu yao.
17
Lakini nikawaonea huruma, sikuwaangamiza kule katika jangwa.
18
Niliwaonya wazao wao kule katika jangwa: Musifuate masharti ya wazee wenu, musishike maagizo yao wala musijichafue kwa kuziabudu sanamu za miungu yao.
19
Mimi Yawe ni Mungu wenu. Mufuate masharti yangu, mushike maagizo yangu kwa uangalifu.
20
Mufanye Sabato zangu kuwa takatifu, kusudi zikuwe kitambulisho cha agano langu nanyi. Hizo zitawakumbusha kwamba mimi Yawe ni Mungu wenu.
21
Lakini hata wazao wao hao waliniasi. Hawakufuata masharti yangu, hawakushika wala kutimiza maagizo yangu ambayo mutu akiyashika, ataishi. Walizikufuru Sabato zangu. Basi nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao kule katika jangwa.
22
Lakini nilizuiza mukono wangu kwa sababu ya heshima ya jina langu kusudi nisizarauliwe kati ya watu wa mataifa walioona nikiwatoa katika inchi ya Misri.
23
Hata hivyo, niliapa kulekule katika jangwa kwamba ningewapeleka katika inchi za mbali na kuwafanya waishi kati ya mataifa ya kigeni,
24
kwa sababu hawakufuata maagizo yangu, lakini waliyakataa masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu na kuziabudu sanamu za miungu ya wazee wao.
25
Tena niliwapa masharti mabaya na maagizo ambayo hayawezi kuwawezesha kuishi.
26
Nikawaacha wajichafue kwa sadaka zao za kuwatoa wazaliwa wao wa kwanza sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Hili lilikuwa pigo lao la azabu ya kutisha kusudi watambue kwamba mimi ni Yawe.
27
Sasa, wewe mwanadamu, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wazee wenu walinikufuru kila mara kwa kukosa uaminifu.
28
Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.
29
(Mimi nikawauliza: Pahali hapo palipoinuka munapokwenda panaitwa namna gani? Wao wakapaita Pahali Palipoinuka mpaka leo.)
30
Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mutajichafua kwa kufuata desturi za wazee wenu na kuviabudu vitu vinavyonichukiza?
31
Munapoendelea kutoa sadaka zenu na kuwateketeza watoto wenu kwa moto munajichafua mpaka leo hii. Nitaulizwa shauri nanyi, enyi watu wa Israeli? Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– sitakubali kuulizwa shauri nanyi.
32
Ninyi munasema ndani ya mioyo yenu: Tutakuwa kama mataifa mengine, kama makabila ya inchi ingine na kuabudu miti na mawe. Hayo munayofikiri ndani ya mioyo yenu hayatafanikiwa hata kidogo.
33
Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– nitawatawala kwa mukono wenye nguvu, kwa ukali na kuwamwangia kasirani yangu.
34
Nitawatoa kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka katika inchi mulimosambazwa kwa mukono wangu wenye nguvu, kwa ukali na kwa kasirani yangu.
35
Nitawapeleka kwenye jangwa la mataifa; na huko nitawahukumu moja kwa moja.
36
Kama nilivyowahukumu wazee wenu kule katika jangwa katika inchi ya Misri, ndivyo nitakavyowahukumu ninyi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
37
Nitawalazimisha mukuwe chini ya uchungaji wangu kila mumoja, na kuwaongoza mupate kutii agano langu.
38
Nitaondoa kati yenu waasi na wale wanaonikosea; nitawaondoa katika inchi walikokaa kama wakimbizi, lakini hawataingia hata kidogo katika inchi ya Waisraeli. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
39
Na sasa, enyi Waisraeli, Bwana wenu Yawe anawaambia hivi: Muendelee kuziabudu sanamu zenu za miungu, kama hamunisikilizi; lakini mutalazimishwa kuacha kulikufuru jina langu takatifu kwa sadaka na sanamu zenu.
40
Maana, katika mulima wangu mutakatifu, mulima murefu wa Israeli, ninyi wote watu wa Israeli mutanitumikia kule. –Ni ujumbe wa Yawe.– Huko mimi nitawapokea na kungojea muniletee sadaka na matoleo yenu bora na matoleo iliyotakaswa.
41
Kisha kuwatoa toka katika inchi ambako mumesambazwa na kuwakusanya pamoja, nitazipokea sadaka zenu zenye harufu nzuri. Nami nitaonyesha utakatifu wangu kati yenu mbele ya mataifa mengine.
42
Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowarudisha mpaka katika inchi ya Israeli, inchi niliyoapa kuwapatia wazee wenu.
43
Huko ndiko mutakapokumbuka mwenendo wenu na matendo yenu mabaya ambayo yaliwachafua; nanyi mutachukizwa kabisa kwa sababu ya maovu yote muliyotenda.
44
Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowatendea ninyi sio kulingana na mwenendo wenu na matendo yenu mabaya, lakini kwa heshima ya jina langu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 21 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48