bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 4
Ezekiel 4
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 5 →
1
Yawe akaniambia tena: Wewe mwanadamu, twaa tofali, uliweke mbele yako na uchape juu yake muji, kama wa Yerusalema.
2
Onyesha kwamba muji ule umeshambuliwa. Utaujengea nafasi za kupandia juu ya kuta zake. Kandokando yake uweke makambi ya waaskari, na gongo ya kubomoa kuta.
3
Nawe utwae bamba la chuma. Ulisimamishe likuwe kama ukuta wa chuma kati yako na muji. Kisha utaelekezea muji huo uso wako nao utashambuliwa na utaushambulia. Hiki kitakuwa kitambulisho kwa taifa la Waisraeli.
4
Kisha, uende ulalie mbavu kwa upande wako wa kushoto. Muda wote utakapokaa katika hali hiyo utabeba uovu wa Waisraeli kama muzigo muzito.
5
Nimekupangia muda wa siku mia tatu na makumi kenda. Muda huu ni sawa na miaka ya azabu yao: siku moja ni sawa na mwaka mumoja. Utabeba azabu ya Waisraeli kwa muda huu.
6
Utakapotimiza siku hizo, utalalia kwa upande wa kuume, na hapo utabeba azabu ya watu wa ufalme wa Yuda kwa muda wa siku makumi ine; nimekupangia siku moja kuwa sawa na mwaka mumoja.
7
Kisha, utauelekea Yerusalema ulioshambuliwa kwa vita na kuunyooshea mukono mutupu na kutabiri juu yake.
8
Nitakufunga kamba kusudi usiweze kugeuka toka upande mumoja mpaka upande mwingine, mpaka wakati kushambuliwa kwa Yerusalema kutakapomalizika.
9
Wewe utwae ngano, shayiri, mahalagi, manjegere, mutama na ulezi, uvitie vyote katika chombo kimoja, ujitengenezee mukate. Mukate huo ndio utakaokuwa chakula chako wakati unapolala kwa upande mumoja, siku zote mia tatu na makumi kenda.
10
Chakula utakachokula kitapimwa, nacho kitakuwa grama mia mbili makumi tatu kwa siku; nawe utakula mara moja tu kwa siku.
11
Maji nayo utayakunywa kwa kipimo: vikombe viwili, mara moja kwa siku.
12
Utatwaa mavi ya mutu, uwashe nayo moto, upike mukate juu yake na kuukula mbele ya watu.
13
Yawe aliniambia: Vile ndivyo Waisraeli watakavyokula mukate wao muchafu wakiwa kati ya mataifa ninakowapeleka.
14
Halafu nikamwambia hivi: Ee, Bwana wangu Yawe, sijajichafua hata kidogo kwa kula nyamafu wala nyama aliyeuawa na nyama wa pori, wala sijapata kuonja nyama anayehesabiwa kuwa muchafu tangu ujana wangu.
15
Kisha akaniambia: Basi, ninakuruhusu utumie mavi ya ngombe pahali pa mavi ya mutu kwa kupika mukate wako.
16
Tena akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, mimi nitaharibu akiba ya chakula katika Yerusalema; wakaaji wake watakula chakula watakachopimiwa kwa hofu. Watakunywa maji watakayopimiwa kwa kufazaika.
17
Nitafanya hivyo kusudi wakose chakula na maji, na kila mumoja atamwangalia mwenzake kwa kufazaika; nao watakuwa zaifu kwa ajili ya azabu yao.
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 5 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48