bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 28
Ezekiel 28
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 27
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 29 →
1
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.
3
Wewe unajiona mwenye hekima kuliko Danieli, unazani hakuna siri yoyote usiyoijua.
4
Kwa hekima na akili yako umejipatia utajiri, umejikusanyia zahabu na feza ukaziweka katika hazina zako.
5
Kwa werevu wako mukubwa katika biashara umejiongezea utajiri wako, ukakuwa na kiburi kwa ajili ya mali zako!
6
Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa vile unajiona mwenye hekima kama mungu,
7
basi nitakuletea watu wageni, mataifa ya hatari kuliko yote. Wataharibu utukufu wa hekima yako na kuchafua uzuri wako.
8
Watakutumbukiza chini ndani ya shimo, nawe utakufa kifo cha rafla katika kilindi cha bahari.
9
Utaendelea kujiona kuwa mungu mbele ya hao watakaokuua? Katika mikono ya hao watakaokuangamiza, utatambua kwamba wewe ni mutu tu, wala si mungu!
10
Utakufa kifo cha haya kubwa katika mikono ya watu wa mataifa. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
11
Tena neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
12
Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa maombolezo juu ya mufalme wa Tiro. Umwambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe mufalme wa Tiro ulikuwa mupaka wa ukamilifu; ulijaa hekima na uzuri kamili.
13
Ulikaa Edeni, bustani ya Mungu. Ulipambwa kwa kila namna ya mawe ya bei kali, akiki, topazi, yaspi, zabarajadi, berili, sardoniki, yakuti samawi, almasi na zumaridi. Ulikuwa na mapambo ya zahabu. Yote uliwekewa tayari siku ulipoumbwa.
14
Nilichagua kerubi kwa kukulinda, uliishi katika mulima wangu mutakatifu na kutembea juu ya mawe yanayometameta.
15
Uliishi maisha makamilifu tangu siku ile ulipoumbwa, mpaka wakati ulipoanza kufanya uovu.
16
Ustawi wa biashara yako ulikujaza ukali, ukatenda zambi. Kwa hiyo nilikufukuza kama muchafu, mbali na mulima wangu mutakatifu. Na yule kerubi aliyekulinda akakufukuzia mbali na mawe yanayometameta.
17
Ulikuwa na kiburi kwa sababu ya uzuri wako. Uliharibu hekima yako kwa sababu ya utukufu wako. Nilikutupa chini kwenye udongo, nikakufanya kuwa kitisho kwa wafalme.
18
Kwa wingi wa mabaya yako na udanganyifu katika biashara yako ulipachafua pahali pako pa kuabudia; kwa hiyo niliwasha moto kwako, nao ukakuteketeza, nami nikakufanya kuwa majivu juu ya inchi, mbele ya wote waliokuangalia.
19
Wote wanaokufahamu kati ya mataifa wameshikwa na mushangao juu yako. Umekuwa kitu cha kuogopesha, na kutoweka kwa milele.
20
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
21
Wewe mwanadamu! Ugeukie upande wa Sidona na kutoa unabii juu yake.
22
Sema hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Sidona, na kuonyesha utukufu wangu kati yako. Nitakapotimiza hukumu zangu juu yako na kukuonyesha utakatifu wangu, halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.
23
Nitakutumia ugonjwa mukali na umwangaji wa damu utafanyika katika barabara zako. Utashambuliwa kwa upanga toka pande zote na watu wako watakaouawa, watakuwa wengi. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
24
Mungu anasema: Mataifa jirani za Waisraeli ambayo yalikuwa yanawauzi hayataweza tena kuwaumiza Waisraeli kama vile kwa miiba na michongoma. Halafu watajua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.
25
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawakusanya na kuwaleta Waisraeli kutoka katika mataifa yote ambamo walisambazwa. Hivyo nitawafanya watu wa mataifa waone kwamba mimi ni mutakatifu. Waisraeli wataishi katika inchi yao ambayo mimi nilimupa mutumishi wangu Yakobo.
26
Watakaa humo kwa salama kabisa; watajenga nyumba na kupanda mizabibu. Wataishi bila hofu maana mataifa jirani zao ambayo yaliwauzi, mimi nitayaazibu. Hapo watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao.
← Chapter 27
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 29 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48