bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 22
Ezekiel 22
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 23 →
1
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Ewe mwanadamu! Uko tayari kutoa hukumu, kuuhukumu muji huu wa wauaji? Basi, ujulishe machukizo yake yote.
3
Uuambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe ni muji unaowaua watu wako mwenyewe na kujichafua kwa kufanya sanamu za miungu; kwa hiyo wakati wako wa azabu umetimia.
4
Una makosa kutokana na damu uliyomwanga. Umejichafua kwa sanamu ulizojifanyia. Umeileta siku yako ya azabu karibu nawe; siku zako zimehesabiwa. Ndiyo maana nimekufanya uchekelewe na mataifa na kuzarauliwa na inchi zote.
5
Inchi zote za mbali na za karibu zitakuchekelea. Umejipatia sifa mbaya na kujaa fujo.
6
Wakubwa wa Waisraeli wanaokuwa humo, kila mumoja kadiri ya nguvu zake anaua watu.
7
Kwako baba na mama wanazarauliwa. Mugeni anayekaa kwako ananyanganywa mali yake. Wayatima na wajane wanaonewa.
8
Wewe umezarau vyombo vyangu vitakatifu na kuzikufuru Sabato zangu.
9
Kwako kuna wanaowasingizia wengine kusudi wauawe. Wakaaji wako wanashiriki chakula kilichotolewa kwa miungu juu ya milima. Watu wako wanatenda uasherati.
10
Kwako kuna watu ambao wanalala na wake wa baba zao. Wanalala kwa kinguvu na wanawake katika siku zao za ugonjwa wa mwezi.
11
Wengine wanafanya machukizo kwa kulala na wake za jirani zao. Wengine wanalala na wake za watoto wao, na wengine wanalala na wadada zao.
12
Huko kwako kuna watu ambao wanapokea kitulizo kwa kumwanga damu. Wanakopesha kwa kudai faida ya juu, wananyanganya mali za wenzao kwa nguvu, na kunisahau mimi kabisa! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
13
Nimekunja ngumi yangu juu yako kwa sababu ya hiyo faida uliyopata kwa njia isiyokuwa ya haki na kwa mauaji yaliyofanyika kwako.
14
Utaweza kuvumilia kuwa hodari siku nitakapokushambulia? Ni mimi Yawe ninayesema hivyo na nitakayetimiza hayo.
15
Nitakusambaza kati ya mataifa na kukutupatupa katika inchi zingine. Nitaukomesha uchafu unaokuwa ndani yako.
16
Utajichafua mbele ya mataifa mengine, lakini utatambua kwamba mimi ni Yawe.
17
Tena neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
18
Wewe mwanadamu! Waisraeli wamekuwa kwangu kama takataka. Wao ni kama takataka inayobaki wakati madini ya shaba, bati, chuma au risasi yanaposafishwa.
19
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa kuwa ninyi wote mumekuwa takataka ya madini, mimi nitawakusanya pamoja katika Yerusalema.
20
Kama vile watu wanavyokusanya feza, shaba, chuma, risasi na bati katika furu wapate kuzisafisha kwa moto, ndivyo kasirani na hasira yangu vitakavyowakusanya huko na kuwayeyusha.
21
Nitawakusanya na kuwawasha moto kwa kasirani yangu; nanyi mutayeyuka mukiwa humo ndani ya muji.
22
Kama feza inavyoyeyuka katika furu, ndivyo mutakavyoyeyushwa humo katika muji. Nanyi mutatambua kwamba mimi Yawe nimeimwanga kasirani yangu juu yenu.
23
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
24
Wewe mwanadamu! Uwaambie Waisraeli kwamba inchi yao ni kama inchi ambayo haijanyeshewa, imenyauka kwa sababu ya kasirani yangu ikakuwa kama udongo bila maji.
25
Wakubwa wenu ni kama simba anayenguruma anaporarua nyama wake. Wanaua watu, wanawanyanganya watu mali na vitu vyao vya bei kali, na kuongeza hesabu ya wajane.
26
Makuhani wao wanavunja sheria zangu, na kukufuru vyombo vyangu vitakatifu. Hawapambanui kati ya vitu vitakatifu na vitu visivyokuwa vitakatifu, wala hawafundishi watu tofauti kati ya mambo yanayokuwa machafu na yanayokuwa safi. Wameacha kuzishika Sabato zangu, na kunizaraulisha kati yao.
27
Wakubwa wake wanaokuwa ndani ya muji ni kama imbwa wa pori wanaorarua nyama wao; wanaua kwa kujitajirisha kwa namna isiyokuwa ya haki.
28
Manabii wake wanaficha maovu hayo kama mutu anapotia chokaa kwenye ukuta wenye kuharibika. Wanapata maono ya uongo na kutabiri udanganyifu mutupu, wakisema “Bwana wetu Yawe anasema hivi”, wakati mimi mwenyewe sikuwaambia chochote.
29
Kila fasi katika inchi watu wanatendeana vibaya na kunyanganya kwa kinguvu. Wanagandamiza wamasikini na wakosefu, na kuwaonea wageni bila kujali.
30
Nilitafuta kati yao mutu mumoja atengeneze ukuta na kusimama juu ya nafasi iliyobomoka mbele yangu, kusudi ailinde inchi na kunizuia nisiiharibu, lakini sikumupata hata mumoja.
31
Kwa hiyo nimewamwangia kasirani yangu na kwa moto wa hasira yangu nimewateketeza kulingana na matendo yao. –Ndivyo anavyosema Bwana wetu Yawe.
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 23 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48