bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Ezekiel 46
Ezekiel 46
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 45
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 47 →
1
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mulango wa kiwanja cha ndani unaoelekea upande wa mashariki utafungwa siku zote sita za kazi. Siku za Sabato na siku za mwandamo wa mwezi utafunguliwa.
2
Tokea inje, mufalme ataingia katika baraza ya ndani kwa kupitia kwenye mulango wa baraza hiyo. Naye atasimama karibu na nguzo ya mulango, wakati makuhani wanateketeza sadaka zake za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Kisha mufalme huyo atainama chini kwenye mulango kwa kuabudu na kisha atatoka inje. Mulango utabaki wazi mpaka magaribi.
3
Kila siku ya Sabato na sikukuu ya mwandamo wa mwezi, watu wote wataniabudu mimi Yawe mbele ya mulango.
4
Siku ya Sabato, mufalme ataleta kwa Yawe wana-kondoo sita na kondoo dume mumoja wote wasiokuwa na kilema kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto.
5
Pamoja na kila kondoo dume, ataleta sadaka ya unga litre kumi na saba na nusu, lakini pamoja na kila mwana-kondoo ataleta sadaka yoyote anayoweza. Na kwa kila sadaka ya unga, ataleta litre tatu za mafuta.
6
Wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi atatoa mwana-ngombe dume, wana-kondoo sita, na kondoo dume mumoja; wote wasiokuwa na kilema.
7
Pamoja na kila ngombe dume na kila kondoo dume anayetolewa sadaka, kunapaswa kuwa litre kumi na saba na nusu za unga, na pamoja na kila mwana-kondoo, kunapaswa kuwa chochote ambacho mufalme anatoa. Tena kwa kila sadaka ya unga, kunapaswa kutolewa litre tatu za unga.
8
Mufalme anapotoka anapaswa kutokea kwa njia ileile aliyoingilia.
9
Watu wanapokuja kumwabudu Yawe wakati wa sikukuu yoyote, wale walioingia kwa njia ya mulango wa kaskazini, watatoka kwa njia ya mulango wa kusini; na wale walioingia kwa mulango wa kusini, watatoka kwa njia ya mulango wa kaskazini. Mutu asirudi kwa njia ya mulango alioingilia, lakini atatoka kwa njia ya mulango unaokuwa mbele yake.
10
Mufalme ataingia ndani watu wanapoingia, na atatoka wanapotoka.
11
Wakati wa siku za sikukuu na siku zilizopangwa, sadaka za unga zitakuwa litre kumi na saba zikiandamana na kila ngombe dume au kondoo dume, na chochote ambacho anayeabudu anaweza kutoa kwa kila mwana-kondoo. Kwa kila sadaka ya unga atatoa litre tatu za mafuta.
12
Mufalme anapotaka kumutolea Yawe sadaka kwa mapenzi yake, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, watamufungulia mulango wa kiwanja cha ndani unaoelekea upande wa mashariki. Atatoa sadaka kama anavyofanya siku ya Sabato, na anapotoka, mulango ufungwe nyuma yake.
13
Kila siku asubui mutamutolea Yawe mwana-kondoo wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, ambaye atateketezwa kwa moto.
14
Vilevile kila siku, sadaka ya kilo mbili za unga itatolewa asubui pamoja na litre moja ya mafuta ya muzeituni yakichanganywa na unga. Inafaa kufuata maagizo za sadaka hii kwa Yawe milele.
15
Mwana-kondoo, unga na mafuta vinapaswa kutolewa kila siku asubui kwa Yawe milele.
16
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ikiwa mufalme anamupa mumoja kati ya wana wake zawadi ya sehemu ya inchi, zawadi hiyo itakuwa mali ya huyo kijana milele kama sehemu ya jamaa yake.
17
Lakini ikiwa atamupa mumoja kati ya watumishi wake sehemu yoyote ya inchi yake, zawadi hiyo itakuwa mali yake mpaka mwaka wa kuachwa huru. Kwa hiyo ndipo itamurudilia tena mufalme. Ni yeye tu na watoto wake wa kiume wanaoweza kuirizi kwa siku zote.
18
Mufalme hapaswi kunyanganya hata kidogo mali ya watu. Sehemu ya inchi yoyote anayowapa watoto wake wa kiume inapaswa kutokana na eneo lake mwenyewe. Hivyo hatawatesa watu wangu kwa kuwanyanganya urizi wao.
19
Kisha, yule mutu akanipitisha kwenye nafasi ya kupitia kuingia kwenye vyumba vitakatifu vya makuhani vinavyoelekea upande wa kaskazini, karibu na mulango wa kusini wa kiwanja cha ndani. Akanionyesha nafasi moja, upande wa magaribi wa vyumba,
20
akaniambia hivi: Hapa ndipo makuhani watakapopikia nyama ya sadaka ya malipo ya kosa, sadaka ya kusamehewa zambi, na kupika sadaka za vyakula. Kwa hiyo hawatoki inje ya baraza na chochote, kusudi watu wasijichafue kwa kugusa kitu kitakatifu.
21
Kisha akanipeleka kwenye kiwanja cha inje, akanipitisha karibu na pembe ine za kiwanja; kwa kila pembe kulikuwa kiwanja kidogo,
22
ni kusema, kwa pembe ine za kiwanja kulikuwa viwanja vine vidogo vya urefu wa metre makumi mbili na upana metre kumi na tano.
23
Kulikuwa ukuta kukizunguka kila kiwanja, na mafika mbele ya ukuta.
24
Yule mutu akaniambia: Haya ni mafika ambako watumishi wa nyumba ya Yawe watapikia sadaka watu wanazoleta.
← Chapter 45
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 47 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48